Niite Sukari Yenu, ni sukari yenu hivo hivo. Nililazimisha nipendwe na kila mtu darasani, ilikua chuo tupo first year ndio tumepanga tukutane wote for the first time tujuane na mipango mikakati maana ilikua ngumu kumtambua mtu unayesoma naye Degree Program moja coz firsr year wote wa school ya business studies tulikua tunachanganyika na kushare course.
Kila mtu akawa anajitambulisha na anasema wishes, ambitions n.k kwa muda wote atakao kuwa chuo, wengine wanatia mbwembwe kibao. Kama kawaida mademu wengi wanafeel shy. Patamu hapo.
Ikafika zamu yangu, nikasimama, nikakohoa kidogo. Nikijifanya kama kuna kitu nawaza hivi, nikaongea kwa lafudhi ya Kipemba, yakhee mi naitwa Sukari Yenu. Watu eeh? Nikarudia...class ya watu 78 ikaburst into laughter.
Jamaa mmoja akanikazia, bro kuwa serious kuna kundi la madem wakamkazia yeye kwamba kwanini anasema mi sipo serious.
Niliiteka hadhira yote na nikawa kama comedian hivi. Wavulana wengi wakawa hawalipendi hilo jina lakini ndio ilikua njia rahisi ya kunikumbuka. Na nashukuru lilienea sana kwa mademu hasa kule hostel zao mpaka kuna siku nilikuta ubishi mkali. Kuna demu mmoja alikua anajua jina langu halisi akawa anawaambia wenzake wanamkatalia wanakomaa mi naitwa Sukari hivyo hivyo. Ilikua balaa...nilikua maarufu ghafla kuliko first year yeyote huku nikichagizwa na kuwasolvia solvia maswali mademu.
Lengo langu siku ile ya kujitambulisha lilikua kuwaambia mi ambition yangu ni kupendwa na kila mtu. Kwa hiyo mimi ni Sukari Yenu. Vicheko vilitawala mpaka sikutaja jina langu halisi.
Pale Ubungo kuna bar inaitwa Yenu....sjui ni registered name. I wish nisajili kitu yangu binafsi e.g company niite hivyo hivyo Yenu.
Tchao,
Sukari Yenu.