Nini uhusiano wa utoaji mimba na figo kufeli?

Miss Natafuta

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2015
Posts
27,031
Reaction score
49,928
Leo nimemkumbuka classmate wangu tukiwa first year akapata mimba akatoa sijui ilitokea nini aliumwa sana figo zikafeli, RIP my dear.

Wa pili huyu tulimaliza chuo vizuri akapata na kazi miezi miwili tu job kumbe alitoa mimba nae figo zikafeli na ini. RIP.

Wa tatu huyu nae tulishakaa mtaani alikuwa na maisha mazuri tu, miaka 33 nae sijui alikuwa hamjui muhusika akaona isiwe kesi, figo nae zikafeli. RIP.

Naombeni kuuliza kuna connection gani ya mimba na figo?
 
Tuwasubiri wataalam wa afya
 
akili yako imejijengea dhana hizo bila uchunguzi. mbaya na majibu ukajipa.
sijui unaulizia nini wakati umeshajitengenezea jibu kutokana na mawazo yako.
hata ahe dkt akupe elimu kwa conxlusion yako hii hutoelewa.

kutia mimba sio kufel figo.
kutoa mimba kupo kivyake na kufeli figo kupo kivyake.
 
Mbona wanaotoa mimba wengi wanapata hizo complications
 
NADHANI hutokana na sumu inayokuwa imemdhuru kwa wakati ule kwasababu mimba nyingi hutolewa kwa njia ya Induced Abortion kwahiyo kutokana na overdose huathiri figo na ini labda hizi ndio huweza kupelekea chronic progression ambayo baadae huwaletea failures
 
Ok
 
Hatari Sana Lakini Hili Jambo Ni Funzo
 
sababu za haraka haraka.
1. Hao walikuwa na matatizo ya figo tangu zamani, ni vile tu mwili haukuwa stressed before ndio maana hawakuwa na dalili.

2. Utoaji mimba usio salama(septic abortion), ilipelekea maambukizi(infections)

3. Kupoteza damu nyingi. kiasi cha damu kinachozunguka kwenye kwenye mishipa (circulatory volume) kikipungua sana ghafla, figo ndio za kwanza kuanza kuathitirika, baada ya hapo inafuata moyo na ini.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hatari Sana
Hili Jambo Ni Kulichulia Seriously Yaani Kuliepuka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…