Nini utokea uendapo kwa mganga

Nini utokea uendapo kwa mganga

The redemeer

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2025
Posts
1,497
Reaction score
2,681
CHUKUA CHAKULA KITOKACHO SIRINI

Makala hii imeandaliwa na
Creezle Farey
☎📞+255789407381

NINI kinafanyika na kutokea unapokwenda kwa mganga na kuchanjwa chale inayotoa damu yako ?
Iko hivi...
Mganga ni kuhani wa madhabahu fulani itendayo kazi kwa masharti
Na miongozo ya miungu itawalayo eneo husika.
Yeye ni msimamizi na mtendaji mkuu katika mwili
Akipokea oda ama maelekezo tokea DIMENSION za miungu rohoni
Katika kanda za Ancestors mizimu..

Yeye ndie muunganishi kwa kutumia dawa na maneno anayeweza kuiunganisha nafsi ya mtu aliyemfuata
Kwa mizimu fulani...

SASA kinachotokea ni HIKI apa.
Bana mganga Mimi nimekuja nina shida fulani.!
Labda kwetu hatupati watoto, sasa naomba unisaidie.
Atakujibu hakika hapa umefika na haja yako itatatuliwa ipasavyo.

Unaitwa nani?
Naitwa fulani.!

Atakachofanya
Nikukuchanja ama kukuagizia kitu kama mnyama mwenye kutoa uhai yaani (Damu)
Kwanini damu?
Damu kwasababu haifi,italia usiku na mchana juu ya tatizo husika

Sasa basi
Baada ya kukuchanja atasema kwa lafudhi na lugha usiyoijua wewe mhusika ama mhitaji....

Mfano:
Kupitia damu hii naisogeza nafsi ya Jarred Mawi
Naomba mizimu ya fulani mumsaidie kupata mtoto,kwa maana huko kwenu tumesikia hamruhusu kupata watoto kwasababu zenu binafsi.
Sasa kupitia damu hii mpatie mtoto...
Kwa masharti mtakayompatia....nayeye
Atatekeleza na asipotekeleza mtamtenda mtoavyo nyie masharti...

SASA
Kule rohoni au kwenye dimension za kiungu,
Ile mizimu inakwenda kwenye mizimu ya koo nyingine kutatua haja
Yako,
Tena kwa masharti....
Mfano: Tunakupatia mtoto wetu,akawe kutokea kiunoni mwako
Lakini atapitia mlango fulani(mwanamke)
Maana yake kuna mwanamke mwingine ataletwa katika mazingira mengine tofauti na mkeo,au hata mkeo
Na utatenda hivi na hivi,
Siku usipotenda kufa na ufe...
Utashangaa kweli umetenda vile vile
Utapata mtoto, lakini huyo mtoto ametolewa mahali pengine utashangaa hata tabia zake sio za huko kwenu kabisa🥁
Na siku ikitokea umejikoroga katika masharti
Unashitukia uko barabarani chini ya matairi ya scania

SIJUI UNANIELEWA.:?

Kupitia dawa na damu yako uchawi au nguvu hasi
Zinakuwa tayari nafsini mwako ....
Ndio
Unaweza pata kuumwa kichwa bila sababu,
Kuhisi unatembelewa na vitu nafsini huvioni,
Wala huwezi kuvishika,
Kuota ndoto za hovyo hovyo
Na kusumbuka rohoni....

Kama unayaona hayo,na kutembelewa na vitu nafsini ujue uko katika hali hiyo,na nguvu hasi ziko ndani yako

KATIKA ukombozi wa nafsi
Hiyo itesekayo
SOMO LITAENDELEA..........
 
Acha kubwabwaja , Ongea upewe connection ujionee maajabu ya mimea na miti tuliyopewa na mwenyezi Mungu, na ujionee namna watu walivyo na maarifa ya haya mambo.
 
Maisha ya shirki hutesa watu kupitia ahadi, maagano na masharti. Watu wamekuwa watumwa kiroho na kimwili. Hii inatokana na kuendelea kukumbatia mambo ya kipuuzi na yasiyo na tija kwenye maisha yao.

Siku Waafrica watakapoamua kujitambua, ndipo Dunia itaanza kuwa sehemu salama ya kuishi.
 
Back
Top Bottom