Kurunzi
JF-Expert Member
- Jul 31, 2009
- 9,753
- 10,747
Aliyekuwa beki wa Yanga Abdallah Shaibu 'Ninja' jana alifanyiwa vipimo vya afya kunako klabu ya LA Galaxy inayoshiriki ligi kuu ya Marekani
Ninja alifuzu vipimo hivyo na ameanza rasmi mazoezi katika klabu hiyo iliyosheheni nyota waliowahi kutamba barani Ulaya
Wakati yuko nchini, Ninja hakuwa akipewa heshima anayostahili kwa kuonekana ni mchezaji wa kawaida sana
Wako waliombeza kuwa hakuwa beki bora aliyepaswa kuwemo kwenye kikosi cha Yanga
Lakini usajili wake kwenda LA Galaxy ni somo kwa wale wanaodharau vipaji vya wachezaji wazawa
Ninja ametua Galaxy sio kwa muujiza, bali ameweza kuwashawishi mabosi wa timu hiyo yenye nyota kama kina Zlatan Ibrahimovic
Huyu Ninja ametoka Yanga na moja kwa moja kwenda LA Galaxy, kiwango chake alichoonyesha kwenye klabu ya Yanga ndicho kilichombeba
Kupitia video zake akiwa Yanga, wazungu wamemkubali na kuamua kumsajili tena bila hata ya kumfanyia majaribio! kitu ambacho ni nadra sana kwa wachezaji kutoka nchi zetu hizi za dunia ya tatu
Winga Mrisho Ngasa aliwahi kupata nafasi ya kwenda huko Marekani lakini licha ya ubora aliokuwa nao wakati huo, alifanyiwa majaribio ambayo hata hivyo hakufanikiwa
Wakati mwingine wadau wa soka hapa Tanzania huwa tunadhani tunaufahamu sana mpira, lakini kiuhalisia hatujui kitu
Imekuwa bahati mbaya hata maamuzi mengi yanayofanywa kuanzia ngazi ya vilabu mpaka timu ya Taifa, hutokana na msukumo wa mashabiki ambao wengi wetu tunadhani tunaujua sana mpira
Ninja alifuzu vipimo hivyo na ameanza rasmi mazoezi katika klabu hiyo iliyosheheni nyota waliowahi kutamba barani Ulaya
Wakati yuko nchini, Ninja hakuwa akipewa heshima anayostahili kwa kuonekana ni mchezaji wa kawaida sana
Wako waliombeza kuwa hakuwa beki bora aliyepaswa kuwemo kwenye kikosi cha Yanga
Lakini usajili wake kwenda LA Galaxy ni somo kwa wale wanaodharau vipaji vya wachezaji wazawa
Ninja ametua Galaxy sio kwa muujiza, bali ameweza kuwashawishi mabosi wa timu hiyo yenye nyota kama kina Zlatan Ibrahimovic
Huyu Ninja ametoka Yanga na moja kwa moja kwenda LA Galaxy, kiwango chake alichoonyesha kwenye klabu ya Yanga ndicho kilichombeba
Kupitia video zake akiwa Yanga, wazungu wamemkubali na kuamua kumsajili tena bila hata ya kumfanyia majaribio! kitu ambacho ni nadra sana kwa wachezaji kutoka nchi zetu hizi za dunia ya tatu
Winga Mrisho Ngasa aliwahi kupata nafasi ya kwenda huko Marekani lakini licha ya ubora aliokuwa nao wakati huo, alifanyiwa majaribio ambayo hata hivyo hakufanikiwa
Wakati mwingine wadau wa soka hapa Tanzania huwa tunadhani tunaufahamu sana mpira, lakini kiuhalisia hatujui kitu
Imekuwa bahati mbaya hata maamuzi mengi yanayofanywa kuanzia ngazi ya vilabu mpaka timu ya Taifa, hutokana na msukumo wa mashabiki ambao wengi wetu tunadhani tunaujua sana mpira