dr namugari
JF-Expert Member
- Nov 19, 2022
- 10,466
- 18,206
Bonge moja la comment.. shukrani sana mdauKm mzunguko wa biashara ni mzuri chukua mchina kwanza for at least 2yrs then anza kuchanganya na scania ilimchina akianza choka scania anakubeba mzigo unakua na kitu kinaitwa business continuity
Kwa hiyo kiongozi katika hili naomba ushauri wa best truck na best trailer..Kachumbari ya magari haitakiwi hasa kwa mazingira yetu ya bongo ambapo kupata spare part original au best aftermarket ni mtihani,
Lakini tatizo kubwa kwa wasafirishaji wa Tanzania ni kuwa hawajui jinsi ya kuspecify gari kutokana na kazi walizo nazo mkononi, Naona mtoa mada pia anastruggle na tatizo hilo, kazi aliyonayo mkononi ni Congo migodini, kule kunahitaji gari heavy duty, yenye retarder , sio lazima iwe double diff , a tag unit with high range hub reduction diff ipo vizuri na ni nyepesi kuliko double diff .p 360 kama unaipeleka kolwezi basi angalau iwe ya south Africa , sio Uk.
Tatizo pia lipo kwa wanaouza hayo magari , hapa naongelea saab scania, wao gari mpya zao zipo well speced kwa mazingira yetu, ila mitumba wanaleta pusher trucks (mid lift), pusher trucks by default ni gari za kazi laini laini, ukishaanza kuipeleka kolwezi R450 pusher , unachezea pesa yako tu maana gharama lazima ziwe juu, kuanzia brake maintanace hadi drive train.
Nimefurahi kusikia kuhusu mpango wako wa kuanzisha kampuni ya usafirishaji wa mizigo kwenda nchi jirani kama DRC, Zambia, Burundi, Rwanda, na kadhalika. Kwa upande wa gari, nashauri kuwa ununue Scania badala ya Howo au Faw, kwa sababu kwa mujibu wa utafiti wako wa awali, Scania inadumu kwa miaka saba hadi nane wakati Howo inadumu kwa miaka mitano tu. Ingawa gharama ya ununuzi wa Scania ni kubwa, inaweza kuokoa gharama ya mafuta, ambayo ni karibu Tsh 600,000 ($200), kutokana na ufanisi wake wa matumizi ya mafuta.Habari natumaini wakongwe mko vizuri
Nina mpango wa kuanzisha kampuni ya usafirishaji nikiwa na mpango wa kusafirisha mizigo kutoka nchini kwenda nchi jirani kwa maana DRC, Zambia, Burundi, Rwanda n.k
(Transit)
Katika kuuliza uliza nimekutana na mawazo makuu mawili ambayo yamekuwa yakinipa mawazo nikaona ni vyema niilete kwenu kwa majadiliano wakongwe
WAZO LA KWANZA
Wazo la kwanza ni kuchukua lori 0 Km kutoka kwa wachina aidha Howo au Faw
WAZO LA PILI
Wazo la pili ni kichukua scania used kutoka saab scania ambapo pale naweza kupata P360 iliyosimama
Trip ni kusafirisha makontena kuelekea maeneo kama vile Congo Kolwezi, Likasi, Lubumbash, Kasumbalesa, Lusaka, Rwanda, Burudi na Malawi
Hivyo basi nataka kujua gari sahihi ambalo wakongwe mtanishauri ninunue kutokana na aina ya safari zangu hizo
Tayari Agent yupo ambaye uhakika wa kutupa tenda za kusafirisha ni uhakika
Kwa kuanza tuna mpango wa kuanza na magari sita (06) lakini upo uwezekano wa kununua mpaka kumi na mbili (12)
UTAFITI WANGU WA AWALI
Gharama za mchina na Scania hazitofautiani sana mathalan kwa mfano ukienda kwa Dr Howo pale kurasini gari N7 na tella lake ambazo ni 0 Km ni $81,000 wakati saab scania used p 360 ni Tsh 150M , ukichukua na tella la superdol na bima na kila kitu ni kama 250M ambayo ni $106,000
MANUNUZI
Mchina:Truck and trailer (both brand new) $81,000
Scania : Used and trailer (brand new) $106,000
MAFUTA
Kwa upande wa mafuta wachina kwenye mafuta wako vizuri kwa maana trip ambayo scania atatumia lita 1900 mchina anaweza kutumia lita 1700 hiyo lita 200 unakuwa umeokoa ambayo ni takribani laki sita (600,000)
Kwa maana mchina gharama za ununuzi ziko chini, uendeshaji ziko chini ila hazidumu sana kwa maana baada ya miaka yako mitano gari kwisha kazi
Ila scania gharama za ununuzi ziko juu, uendeshaji, iko juu ila zinadumu hadi miaka saba hadi nane..
Naileta hii mada kwenu kwamba je niingie kwa mchina au niingie kwa msweeden?
WHY SAAB SCANIA NA SIO KUAGIZA SCANIA KUTOKA UINGEREZA
Watu wamenishauri kuagiza scania gharama haitofautiani iwapo ukaenda kununua saab scania lakini haina guarantee unaweza agiza gari kutoka UK used limetembea km 400,000 ukaanza safari kufika chalinze tu ngoma imesizi, hapo uneshapokea mzigo wa mtu ni lazima ufanye engine overhaul na mambo mengine mengi
Hapo unakuta unapoteza mpaka 9 M kwa engine na fundi etc
Lakini pia kwa upande wa kichina ni kwamba madereva wazuri wanazikimbia sababu ya aina ya magari kiafya sio rafiki kwao hivyo ukiwa na scania kama p360 ni rahisi kupata madereva wazuri kwani talent pool ya madereva wanaotaka kuendesha hizo p360 ni kubwa pia
Hivyo basi naomba kuuliza kwa gari 6 mpaka 12, agent tayari kashakuwa spotted anaweza kutupa kazi trip ni za kwenda Congo Kolwezi, Likasi, Lubumbash, Kasumbalesa, Lusaka, Rwanda, Burudi na Malawi je nishukue mchina au niingie kwa m sweeden naomba kujua sana sana technical know hows za hizi chuma mbili
Maana kuna watu wanashauri kuwa ni bora mchina na wengine wanashauri ni bora m sweeden used
Tayari eneo ambalo nitalifanya kama yard nimesha li spot ambapo ni Kibaha kwa mathias itakapokuwa makao makuu na main yard ya chuma kwa maana agent akikamilisha kila kitu chuma zinaamsha toka kibaha kwenda bandarini kupakia kisha kuamsha...
Natanguliza shukrani
C.T.UView attachment 2566531View attachment 2566532
Wanasema hizi howo N7 siti zimeboreshwa ila ngoja nitafuatilia zaodiChukuwa scania mkuu utaleta mrejesho hapa parts zake zipo rundo na zina mafundi wazoefu sana, pia nakupa ujanja mara ununuapo gari za kichina badili sit ya dereva ndiyo inayoumiza kwa kweli.
Shukrani sana Mkuu kwa hiyo ni focus sana sana na euro 3 si ndio eeehMkuu ushauri wangu kwa structure ya kazi zako na huko unakokwenda , nakushauri gari ya kichina,
Sipendi gari ya kichina na kupata madereva ni ngumu sana kwa sasa , kwa sababu as they become popular nowadays watu wanafahamu mengi kuhusu hizo gari , kiukweli sio rafiki wa afya kwa dereva , na zinachosha sana, yes zinatumia.mafuta vizuri lakini zikiwa mpya tu, zikichoka zipo vibaya ,
Kwa nini sikushauri scania japo naipenda sana , !!, sababu nimeona unafocus kwenye mtumba wa Uk, kama unaweza nenda botswana ,namibia au south africa huko utapata scania za kwenda nazo kolwezi.
R450 mtumba wa uk inakuja na diff yenye ration 2.92, hii ni diff ya mbio sio kupanda milima , R460 ya south ni euro 3 na inakuja na diff yenye ratio 3.08.hii ni diff ya milima sio.mbio, ndio maana ukiilazimisha r450 ya mtumbaipande milima kwa uwezo wa engine lazima utaoverhaul engine mapema
Best trailer tafuta double tires on air suspension , preferably with bendix or wabco Abs systemKwa hiyo kiongozi katika hili naomba ushauri wa best truck na best trailer..
Tafuta Euro 3 ! Kwa kuwa mafuta tunayotumia bado yana sulpbur content kubwa , Trucks za euro 5 na6 zinatumia ultra low sulphur diesel, huku hatuna hiyo , ndio sababu cha kwanza huwa zinazingua sensors ni nyingi na ukishawekandiesel yetu matatizo yanaanza , wich is the reason why hata ukiwa na pwaa yako scania Tanzania hawezi kukuagizia gari mpya yoyote ya euro 6, maana anajua hataweza kukupa warranty na litakusumbua .Shukrani sana Mkuu kwa hiyo ni focus sana sana na euro 3 si ndio eeeh
KUlima ni Rukwa mzee, Ruvuma kanunue vitalu vya makaa ya mawe ndo habari ya mjini.Achana na biashara pasua kichwa..twende zetu Ruvuma tukalime..
Nipe ABC mzee..ni kule Kitai?KUlima ni Rukwa mzee, Ruvuma kanunue vitalu vya makaa ya mawe ndo habari ya mjini.
cheza bingo hiyo ukibutua ni mpunga wa kula hadi unaiaga dunia .ukifeli unalima mahindi.
RUvuma yote inasemekana ni reserve ya makaa, cheza kamari yako vizuri,Nipe ABC mzee..ni kule Kitai?