Nioe mke mwingine?


Hiyo red acha kuwa tegemezi hataki kusaidia maana yake nini??
Hiyo blue wewe huna msimamo wakati anampeleka wakwake international kulikuwa hakuna makubaliano? Mawasiliano kati yako na yeye ni ziro
Hiyo zambarau mikutano gani hiyo inayoambatana na vinywaji sijawahi sikia (wewe ni mlalamishi sana)

Ki ukweli ni hoja nzito mkuu, lakini imekuwa bahati kuwa umekwisha ijibu kwamba

Acha uongo juzi QT mara ushajua lugha ngumu hivyo?

Nashukuru sana kwa michango yenu, imekuwa ya manufaa sana kwangu.

Lugha gongana hapa

Ni kweli usemayo lakini jamani hivi kweli mimi sina haki ya kuliwazwa katika magumu haya?!,

Malalamiko again and again

Ahsante sana kwa mchango wako na ushauri wako mzuri,

Umeshatoa uamuzi na inaonyesha tayari una mahusiano mengine



Upewe mtaji wa biashara na mwanamke?? Na unalalamika hadharani aibu gani hii.
Wewe umeshaamua kuoa ndo maana unataafuta attention hapa jamvini

BTW: Uamuzi ni wako.

Kwa ushauri wangu ni kwamba stand as a man na acha kucomplain kama mtoto mdogo eti mwanamke anakunyanyasa mara anakunyima mtaji mara anasomesha wakwake international mara anarudi usiku yaani yote haya naona ni malalamiko matupu na wewe unaonyesha dhahiri ni MARIOO acha hiyo tabia kuwa mwanaume mtimilifu unalalamika kutotunzwa na mwanamke nimeshangaa sana. Im sory to say that.

Good day my brother
 

As woman nakushauri muache huyo mkeo ataua ur self esteem, achana naye chukua mwanao jipange upya. Maana hapo si anakuumiza ww tu pia fikiria psychological effect kwa mwanao. Ataanza wa kwako anavaa za Kariakoo na wa kwake mama's pride n.k. We should learn to understand and accept when things are over. Fanya kazi kwa bidii kuendesha maisha ila huyo sasa siyo class yako! period. Ni ukweli mgumu kuubali but that is it. Sijui niseme ni ver natural mwanamke hawatakiwi kuhead family kwenye issue ya finance sijui tukoje ila haikai poa ila a man akihead in every thing its ok as iliandikwa 'utazaa kwa uchungu' na 'utakula kwa jasho' Mwanamke ni mzuri kama head wa family in single parent home. Akina marioo hawana say yoyote kwa wanaowatunza she can do any f..ck na waishia ndiyo madam, if nawe umeamua uwe hivyo well n good if nt move on. Dah I hate kina marioo sometimes hata having them on bed is an issue, I feel like u dont belong thr u belong to ur class. The best way kuearn heshima ya mtt wa kike outsmart her in cash! period unaweza ukawa darasa la saba na yeye ni professor akakuamkia asubuhi! Kuna msemo mmoja na ninaamini ni ukweli ' every woman is a golddigger' basi tu mazingira sijui na heshima ya jamii inatufanya tunapretend. Wanaolea kina marioo utawasikia saloon wanalalamika tu yaani me nina mume suruali tu, or me nina mme jina n.k
 
kaka tulia kwa makini sana kabla hujafanya maamuzi yoyote yale,kwanza fanya juhudi sana ya kutafuta kazi kila siku.endelea kumpa mapenzi ya nguvu mkeo na watoto wote bila kuonyesha hasira yoyote.tafuta siku moja ambayo ni ya mapumziko umwambie mkeo una maongezi naye nje ya hapo nyumbani na utafute mahali patulivu sana na ongea nae kwa utaratibu juu ya tabia zake jinsi ambavyo zinaweza kuhatarisha ndoa yenu.baada ya hapo ukiona hakuna mabadiliko basi ni PM nitakupa mkakati mwingine lakini usijaribu kuoa mwanamke mwingine wala usiwaze jamabo hilo
 

Sina uhakika kama hii ni mlimazunzu versus Mulama au ni kutafuta namna ya kumpa ufumbuzi mulama kwenye matatizo yanayomsibu?!, ebu tuelewane kitu kimoja mtu anapolalamika manake ana tatizo linalotaka utatuzi kupitia watu wengine yaani yeye ameshindwa kupata ufumbuzi yeye kama yeye.

Au wewe unachangia mada za wenye amani na furaha wasio na matatizo ya kulalamikia?! sitaki ni kuhukumu lakini nadhani wewe umeshindwa kuwa na hekima ya kutambua nini uzungumze na kwa wakati gani au pengine coprehension (lucid) ni tatizo katika masuala ya kijamii.

Pendekezo: Ndugu Moderator kama inawezekana uwa consult wataalamu wa IT ili kwamba avatars za memeber ziweze ku reveal jinsia na umri wa mtu, uzoefu wangu wa siku chache jamvini humu unaonesha wakati mwingine hoja nzito zinajadiliwa inappropriately kutokana na factors kama vile immaturity au gender biase!

Pole mlimazunzu kama nitakuwa nimeku offend.
 

Ahsante sana morio kwa ujumbe mzuri, pia ujumbe wako huu nau dedicate kwa mlimazunzu!

Pamoja na hayo jamani ningependa tuliweke wazi publicly kwamba wanawake are meant kutokusaidia wanaume hata kama pesa au maendeleo wameyapata kupitia kwa mwanaume!

Na kwamba mwanaume akiwa na pesa ampe mwanamke kama kifaa anachonunua kwa matumizi ya kumtumikia au kumfurahisha sio? Inashangaza kuona kwamba mwanaume akiwa na pesa anaweza kumchukua au kumuoa mwanamke yeyote bila kujari class yake, kumbe mwanamke akiwa akiwa juu ya mwanaume kipesa au kimaendeleo anakuwa hamstahili!

Sorry nimekuwa tempered kidogo, acha niishie hapa.
 

We jamaa hebu ongea na mkeo muelewane muyaweke mambo yawe sawa acha kuwa na hasira wewe ni mwanaume unamshindwaje mkeo lakini??
Au unamuogopa?? si uongee nae muelewane lkn naona kama mawasiliano ndani yako na yeye kama not reachable haiwezekane ushindwe kuzungumza nae na unaishi nae siku zote.

Pole sana mkuu kwa yaliyokupata
 
Desidii,
Yakimwagika hayazoleki!!, mnapoanza mapenzi ni matamu kama asari yakiisha?.......!
 
elewa mada wewe Rosemarie, usikurupuke kujibu tu. anauliza aoe mwingine nakumuacha huyu wa sasa kwa sbb hafai sasa.....
 
elewa mada wewe Rosemarie, usikurupuke kujibu tu. anauliza aoe mwingine nakumuacha huyu wa sasa kwa sbb hafai sasa.....

Ahsante mkuu, naona hawa wanajibu bila kufikiri!
 
Usije kumwacha bila kumtandika, piga mno! Mitama, vichwa na ngumi za uso! Ndiyo umwache na ukomae yeyw ndiyo aondoke sio wewe.
Usiogope kina Mandela waliacha wake zao na bado wanaheshimika...piga chini usaha huo...
 

Ndugu Mulama kwa hilo kwenye Blue hutafanikiwa kamwe FYI humu watu wana ID kibao za kike na kiume pia so hiyo ngumu Mkuu.

Pole lakini na samahani kama nimekukwaza.

Off topic: Umefikia wapi na mkeo umesema nae au ndo aje sasa? By the time naona kama mambo yanazungumzika tu hayo madogo sana hakuna kinachoshindikana chini ya jua bana hebu tupe feedback basi.
 

Nimekusoma sawasawa Mkubwa pole kama nilikukwaza kwa post yangu
 
Usije kumwacha bila kumtandika, piga mno! Mitama, vichwa na ngumi za uso! Ndiyo umwache na ukomae yeyw ndiyo aondoke sio wewe.
Usiogope kina Mandela waliacha wake zao na bado wanaheshimika...piga chini usaha huo...

Wewe lazima utakuwa mtani wangu ngumi, mtama na kumtandika umekuwa bondia wanawake hawapigwi siku hizi
 

Wewe lazima utakuwa mtani wangu ngumi, mtama na kumtandika umekuwa bondia wanawake hawapigwi siku hizi

Nyie watu wawili mnanichanganya sana.......

Miandiko yenu imefanana sana.....nyie mapacha?
 
Ndg yangu Bwn Mulama pole saana kwa masaibu yote yaliyo kukuta, bila shaka ni ujumbe mzuri na umefika kwa wahusika. Ila Ndg pomoja na maelezo na maushauri mengi uliyopewa; mimi nazungumza from experience. Kwanza umri wa mwanamke wa kuishi akiwa bado beautiful and atractive ni mdogo saana hasa kama anajihusisha na mambo ya pombe na anasa!!! Mwanaume umeumbwa na Mungu kwa makusudi yake kabisa, anakuhitaji uwe mvumilivu saana utumie akili. Ila kwa sasa kwa ajili ya haya magonjwa nishida kidogo. Kama nyumba mnayoishi ni ya familia, inatakiwa uwe mjinga ili usipote kila kitu hata maisha yako!!!!!! Kama mnapanga basi jaribu kujiweka kando lakini usimuache haraka wala usioe maana mnayo familia ya kuilea. Changa akili tafuta kazi za kufanya uweze kuchangia ingawa kidogo kwenye matumizi nyumbani. Uvumilie na kuonyesha kuwa bado unampenda, baada ya muda fulani atajirudi atatambua kosa lake na mtaanza upya maisha yenu ya ndoa. Peleka kesi yako kwa Mungu yeye hapendi watu watengane, bali shetani anataka watu waachane awatumie kama mandondocha. Tuliza akili zako maana Mungu anataka tuishi na wake zetu kwa akili!!!!!!!!!!
 
Mtaji unao huo mwili wako, we lialia ndani tu shauri yako, body hilo mali adimu.... ushaelewa vibaya hahahaha unaweza kuwa bauncer wa macelebrity au night club lol acha kulalama ingia mtaani mulama
 
Pole sana kakangu, huyo ameshapoteza mapenzi na wewe kwa hayo mafanikio ambayo wewe ndo sababu. Jaribu kukaa naye chini na kumwelekeza na ikiwezekana mkumbushe mlikotoka. Ikishindikana hapo naona mambo ni magumu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…