Nipeni ushauri kutokana na uzoefu wenu katika ujenzi

Nipeni ushauri kutokana na uzoefu wenu katika ujenzi

Mkuu ukitaka ujenzi wewe anza tu hela ikiwa mikononi majanga hayeshi bora ujenge sasa kabla jinsia nyengine ikataka nusu yake.
Ushauri mzuri sana huu umempa!! Ujenzi wa kudunduliza unakula nafasi ya kufanya na mambo mengine ya dharula. Majanga kwa mtu mweusi hayajawahi kuisha
 
Mkuu nyumba ya vyumba vinne ni kubwa sana. Jenga ya vyumba vitatu kimoja self na viwili vya kawaida. Ila kama kipato chako kina mtiririko mzuri jenga hiyo ya vyumba vinne (vitatu self na kimoja cha kawaida).
Hawa ndio wanaotuachia mapagala mjini hapa

Hawataki kuhesabu gharama ma uwezo wao
 
Lengo ni kwamba nahitaji kuanza ujenzi.

Ila mpaka sasa nime save 5ml, ila nina uhakika wa kusave laki 6 kila mwezi.

Nahitaji kujenga nyumba ya kawaida tu iwe na vyumba vinne je naweza kuanza taratibu au niendelee tu kujichanga.

Site ni DSM maeneo ya chamazi.. Nipeni uzoefu wenu wadau
Tafuta ramani kisha utapata makadirio ya mahitaji, anza kukusanya material taratibu ukimaliza jenga kwa awamu kulingana na uwezo wako.
 
Nimeanza ujenzi wa vyumba vitatu(nyumba ya kawaida tu) msingi tu nimetumia mil1.5 nimenunua na tofali za kupandishia hadi lenta mtonyo umekata navuta pumzi

Ningeanza na iyo mil5 kama wewe ingebaki kupaua na bati
 
KUjenga ni timing tu kama unaweza anza kidogo dogo usisubiri upate mamilion vingnevyo hutaweza kujenga anza na msingi kwanza tulia then ukipata ela unaendelea
 
Hujasema 5m hizi unazipata katika kazi, biashara au shughuli yako ni Nini? Ili tukupe ushauri Kulingana na kipato chako.

Kama ni biashara sikushauri kwenda kuzika hizo pesa ulipo ni mbali sana na uhalisia wa unachokitaka. Nina nyumba ya vyumba nne imenicost zaidi 50m vinginevyo uwe unataka nyumba za kiswahili ambazo hazifuati kanuni za ujenzi.

Hebu ona kipato chako 600k x 12= 7.2m. Tufanye assumption utajenga nyumba isiyokamilika, lakini itakuruhusu kuhamia ya vyumba nne kwa 30m. Maana yake una miaka nne mbele ya kukamilisha mradi wako. Ndiposa nakushauri Kama hiyo unayotoa ni sehem ya mtaji usijaribu kuitoa kwa sasa, huenda nyumba hiyo itakufilisi na biashara yakko yote kwa tamaa ya kutaka kuona inaisha. Ujenzi usipokuwa mzoefu na hela za mawazo unafilisi utabaki na nyumba au watoto hawaendi chooni.

Kama ni mfanyakazi na hujui chochote nje ya kazi Basi nenda kazike hizo hela. Lakini Kama ungekuwa mtu mwerevu kwa namna yoyote ningekuambia hizi 5m ukizungusha baada ya mwaka zitakupa 5m nyingine. Iko hivi Kama utaweza kuzalisha faida ndogo tu ya 500k kwa mwezi kutoka kwa hiyo 5 bhasi toa hizo faida ingiza mdogo mdogo kwenye ujenzi baada ya mwaka utakuwa umebakiwa na mtaji na ujenzi unaendelea.

Huu ni ushauri wangu Kulingana na uzoefu wangu ktk ujenzi, biashara mtaani, kazi serikalini. Kila la kheri.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
Tukiassume nyumba itakamilika kwa 50m

Kwa hiyo ina maana atahitaji 8 yrs kuimaliza

Basi sio maamuzi mazuri kwa sasa
 
Back
Top Bottom