Nipepo au ni uraibu? Anaomba msaada

Nipepo au ni uraibu? Anaomba msaada

Laswell

Senior Member
Joined
Feb 23, 2024
Posts
144
Reaction score
191
Salaam wanajukwaa. Jamaa yangu amepatwa na tatizo ambalo yeye mwenyewe halielewi na hata Mimi aliyenisimulia nimeshindwa kumuelewa ndomana nimelileta kwenu. Iko hivi, huyu rafiki ni mtumishi wa umma kwa zaidi ya miaka 10 sasa.

Pamoja na mshahara anaopata anajitahidi kupambana nje yakazi na maisha yake sio mabaya, anajiweza. Tatizo lake limeanza rasmi mwezi July mwaka Jana na limemporomosha kiuchumi vibaya kiasi sasa amechanganyikiwa.

AVIATOR! mwanzo aliponitajia hiki kitu sikumwelewa kwani nilikuwa sijui kabisa.Alijaribu kunifafanulia mwisho nikaelewa nimchezo Fulani jamiii ya betting wenyewe wanaita kandege. Jamaa yangu anacheza huo mchezo na kwa wiki anaweza apoteze zaidi ya laki6!

Anadai amefikia kiwango Cha kuuza mali zake kutokana na madeni aliyokopa nakuyaelekeza kwenye mchezo huo.Tumeshauri njia nyingi zakuacha hadi akaamua kuharibu Simu yake ili asiingie mtandaoni lakini Bado mwamba ametengeneza na amerudi mchezoni.

Ana ofisi flan ya huduma za stationary ila wateja wakitanguliza pesa jamaa anaziweka kwenye kindege analiwa kinachobaki ni kusumbuana na wateja.

Najua betting Ina kula na kuliwa lakini kwa uliwaji huu na Bado anaendelea kucheza nahisi(nahata yeye)anaamini Kuna jambo nyuma.Anasema akishika tu pesa mkononi wazo lakwanza linamjia nikucheza kindege,Zikiisha anabaki na majuto huku akijiapiza hatarudia tena.

Ana mke na watoto,ila kwa Hali ilivyo ndoa ipo mashakani.Nifupishe tu kwakusema jamaa anahitaji msaada wa kutoka kwenye huo mchezo kwani anahisi Kuna mchezo kafanyiwa na sio akili zake.

Wakati Fulani niliingia jukwaa la wazee wakubeti hapa hapa JF nikaulizia ili nijue betting za kindege zinakuwa na madhara kama hayo kwa watu wote au Kuna kitu sio bure.

Uwezo wangu na ndugu wengine wakumshauri aache umeshindikana kwani Jana tu katoka kuliwa laki4 .
 
Salaam wanajukwaa. Jamaa yangu amepatwa na tatizo ambalo yeye mwenyewe halielewi na hata Mimi aliyenisimulia nimeshindwa kumuelewa ndomana nimelileta kwenu. Iko hivi, huyu rafiki ni mtumishi wa umma kwa zaidi ya miaka 10 sasa. Pamoja na mshahara anaopata anajitahidi kupambana nje yakazi na maisha yake sio mabaya, anajiweza. Tatizo lake limeanza rasmi mwezi July mwaka Jana na limemporomosha kiuchumi vibaya kiasi sasa amechanganyikiwa. AVIATOR! mwanzo aliponitajia hiki kitu sikumwelewa kwani nilikuwa sijui kabisa.Alijaribu kunifafanulia mwisho nikaelewa nimchezo Fulani jamiii ya betting wenyewe wanaita kandege. Jamaa yangu anacheza huo mchezo na kwa wiki anaweza apoteze zaidi ya laki6! Anadai amefikia kiwango Cha kuuza mali zake kutokana na madeni aliyokopa nakuyaelekeza kwenye mchezo huo.Tumeshauri njia nyingi zakuacha hadi akaamua kuharibu Simu yake ili asiingie mtandaoni lakini Bado mwamba ametengeneza na amerudi mchezoni.Ana ofisi flan ya huduma za stationary ila wateja wakitanguliza pesa jamaa anaziweka kwenye kindege analiwa kinachobaki ni kusumbuana na wateja. Najua betting Ina kula na kuliwa lakini kwa uliwaji huu na Bado anaendelea kucheza nahisi(nahata yeye)anaamini Kuna jambo nyuma.Anasema akishika tu pesa mkononi wazo lakwanza linamjia nikucheza kindege,Zikiisha anabaki na majuto huku akijiapiza hatarudia tena. Ana mke na watoto,ila kwa Hali ilivyo ndoa ipo mashakani.Nifupishe tu kwakusema jamaa anahitaji msaada wa kutoka kwenye huo mchezo kwani anahisi Kuna mchezo kafanyiwa na sio akili zake. Wakati Fulani niliingia jukwaa la wazee wakubeti hapa hapa JF nikaulizia ili nijue betting za kindege zinakuwa na madhara kama hayo kwa watu wote au Kuna kitu sio bure. Uwezo wangu na ndugu wengine wakumshauri aache umeshindikana kwani Jana tu katoka kuliwa laki4 .
Wabongo bwana...kwa hiyo yeye anadhani amerogwa 🤣🤣🤣🤣
Mbona sie tunazika mamillion ya pesa kila mwaka kwenye mbususu na hatudhanii hayo mambo ya kurogwa
 
Huyo anao uraibu uliokubuhu, akumbuke hatokaa apate faida kwenye huo mchezo.

Huyo jamaa yako ni fala sana unachezaje makamari mpaka mkeo, ndugu na jamii inajua? Huyo ndio haaminiki tena mpaka aache na ithibitike kaacha. AVIATOR isikie tu usiombe uingie kwenye uraibu wake ni hatari sana.
 
Nadhani, sio kawaida ila anatakiwa apate saikologisti ampe elimu na ikishindikana kabisa anatakiwa amrudie mungu wake coz kamali isha ingia kwenye damu, roho ya umaskini inamtafuta
Hali nimbaya mkuu
 
Huyo anao uraibu uliokubuhu, akumbuke hatokaa apate faida kwenye huo mchezo.

Huyo jamaa yako ni fala sana unachezaje makamari mpaka mkeo, ndugu na jamii inajua? Huyo ndio haaminiki tena mpaka aache na ithibitike kaacha. AVIATOR isikie tu usiombe uingie kwenye uraibu wake ni hatari sana.
Hata Mimi nilimuona fala na uzri nayeye mwenyewe Huwa anajiona fala akifikiria yanayomtokea. Issue nikwamba anatokaje huko asiendelee kuwa fala?
 
Unakwama wapi ndugu mtumishi?😏
1000017392.jpg
 
Hata Mimi nilimuona fala na uzri nayeye mwenyewe Huwa anajiona fala akifikiria yanayomtokea. Issue nikwamba anatokaje huko asiendelee kuwa fala?
Pole mkuu,mwambie atafute kitu kingine au hobby ya kufanya, kwa mfano kilimo shambani, muda ule anaokaa idle na kuwaza ku bet atumie kufanya hio hobby mpya...abadilishe mazingira kama kazini kwake kunamruhusu akae idle then atoke hapo....
 
Huyo rafiki yako ambae ni mtumishi wa umma ni wewe usione aibu kwa wanaume wenzio ...

Tulishacheza sana baada ya kuishiwa hela za kuchezea na ndo tukaacha...

Sure pekee ni Odds 10 unaweka elfu 10 ...hayo mengine ...
Nikitegemea San mchango kama huu
Huyo rafiki yako ambae ni mtumishi wa umma ni wewe usione aibu kwa wanaume wenzio ...

Tulishacheza sana baada ya kuishiwa hela za kuchezea na ndo tukaacha...

Sure pekee ni Odds 10 unaweka elfu 10 ...hayo mengine ...
Nilitegemea San comment kama hii kwani ndivyo wengi tulivyo hapa JF.Mtu anapowasilisha changamot zamtu mwingine inaonekana niyeye ila akieleza mafanikio na utajiri wa mtu mwingine hapo comments zitamhusu mlengwa moja kwa moja.Ningesema Kuna jamaa yangu tajiri Wala usingethubutu kusema huyo jamaa nimimi. Anyways,tufanye nimimi mwenye hyo shida....naomba msaada wako mkuu
 
Back
Top Bottom