Nipo kwenye haya mahusiano nisiyoyaelewa

Nipo kwenye haya mahusiano nisiyoyaelewa

Sharobaro la jf

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2020
Posts
237
Reaction score
325
Kiukweli mapenzi yanauma sana jamni acheni tu, kuna mwanamke nipo nae sasa tuna miezi mitatu, tulikutanaga instagram ndipo tukawa tunawasilana hadi baadae tulipoingia kwenye uchumba, bahati nzuri tunakaa mtaa sio mbali mbali, yeye yupo kihonda mimi nipo msamvu na uwa tunakutana mara kwa mara ila sasa hatujaonana mda mrefu zaidi ya kuwasiliana tu kwa simu, sasa kinachoniumiza ni kumuona huyu mtu kabadilika ghafla, inabidi kila siku mimi ndie wa kumuanza kumtafuta, nisipomtafuta yeye wala hanitafuti, nimejukuta mimi tu ndio wa kutetea penzi langu na yeye wala hajali, anaweza kukaa wiki nzima asikutafute hadi umuanze, binafsi nimejitahidi kuwa mvumilivu nikahisi huenda labda ananipima uvumilivu wangu lakini naona kama nakata tamaa, kweli nampenda ila dharau alizoanza kunionyeshea ndio zinanivunja moyo,
Naombeni ushauri?
 
Jaribu kuongea nae mueleze unavyojisikia lkn usiwe kiviilee utajishusha hadhi!
Pia jaribu kunogesha mawasiliano yenu awe nashauku nawe usikute bado mpaka leo unamuuliza kwenu kuna mbwa😅
Kabla hujamuuliza umemkwaza nini fikiria we mwenyewe umekosea wapi.. ukiona hana sababu yenye mantiki bro anza kujiandaa kaa mguu nje mguu ndani
 
Back
Top Bottom