justine lowasa
JF-Expert Member
- Aug 30, 2016
- 727
- 794
Wakuu Wasalaam!
Natumai mnaendelea vyema na Ujenzi wa Taifa letu tukufu. Leo napenda kuwajulisha rasmi azma yangu ya kugombea Ubunge katika Jimbo la Same Magharibi kwa tiketi ya Chama Changu cha CHADEMA .
Mimi Fredrick Justine ambaye ni Mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mwenye kadi ya uanachama namba 222111 nilitangaza nia hiyo tangu tarehe 20 March 2020 kwakumuandikia barua katibu wa Kanda ya Kaskazini kama utaratibu wa Chama ulivyotuelekeza.
Katika barua yangu, nilimjulisha katibu wa kanda kwamba,
“Nimefikia uammuzi huu baada yakujipima na kuona natosha kuwatumikia ndugu zangu wa Same na umma wa Watanzania, huku moyo wangu ukiwa umejaa shauku kubwa nikitamani kuiona Tanzania, nchi tuipendayo kwa moyo wote inapata ustawi na kuendeleza matamanio, matarajio na ndoto za watu wake, kuanzia ngazi ya mtaa hadi taifa kwa ujumla"
Pia niliendelea kwa kumuandikia katibu wa Kanda.
“Katika kuwapatia maendeleo endevu wananchi wa Same yatupaswa kuwa na Taifa linalosimamia uhuru na haki za watu, utawala wa sheria, uhuru wa vyombo vya habari,na demokrasia ya kweli inayowapa wananchi mamlaka kuhusu mustakabali na mwelekeo wa nchi kupitia chaguzi za viongozi zilizo huru na za haki.
Pia, nilieleza namna nilivyojipanga kushirikiana na viongozi wengine watakaochaguliwa kuunda serikali katika kusimamia utatuzi wa kero mbali mbali zinazowakabili wananchi wa Same katika sekta ya Afya, Elimu, Kilimo, Ufugaji na utatuzi wa migogoro ya Ardhi baina ya wafugaji na wakulima inayowakabili wananchi katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Same Magharibi.
Mbali na mambo hayo pia nilieleza endapo ntapata ridhaa ya Chama na wananchi ntashirikiana kwa karibu na wadau wa elimu na wanaharakati wa masuala ya Elimu kuishinikiza serikali kutoa Elimu bila ubaguzi hususani kwa watu wenye mahitaji maalum na mabinti wanaopata ujauzito wakiwa mashuleni ili kuwapa fursa ya kujiendeleza na kufikia malengo yao bila kukwamishwa na sheria, kanuni au matamko kandamizi.
Naombeni ushirikiano wenu katika safari hii muhimu kwa ustawi wa Taifa letu, Mungu Awabariki wotee [emoji120].
Fredrick Mbwambo Justine.
Natumai mnaendelea vyema na Ujenzi wa Taifa letu tukufu. Leo napenda kuwajulisha rasmi azma yangu ya kugombea Ubunge katika Jimbo la Same Magharibi kwa tiketi ya Chama Changu cha CHADEMA .
Mimi Fredrick Justine ambaye ni Mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mwenye kadi ya uanachama namba 222111 nilitangaza nia hiyo tangu tarehe 20 March 2020 kwakumuandikia barua katibu wa Kanda ya Kaskazini kama utaratibu wa Chama ulivyotuelekeza.
Katika barua yangu, nilimjulisha katibu wa kanda kwamba,
“Nimefikia uammuzi huu baada yakujipima na kuona natosha kuwatumikia ndugu zangu wa Same na umma wa Watanzania, huku moyo wangu ukiwa umejaa shauku kubwa nikitamani kuiona Tanzania, nchi tuipendayo kwa moyo wote inapata ustawi na kuendeleza matamanio, matarajio na ndoto za watu wake, kuanzia ngazi ya mtaa hadi taifa kwa ujumla"
Pia niliendelea kwa kumuandikia katibu wa Kanda.
“Katika kuwapatia maendeleo endevu wananchi wa Same yatupaswa kuwa na Taifa linalosimamia uhuru na haki za watu, utawala wa sheria, uhuru wa vyombo vya habari,na demokrasia ya kweli inayowapa wananchi mamlaka kuhusu mustakabali na mwelekeo wa nchi kupitia chaguzi za viongozi zilizo huru na za haki.
Pia, nilieleza namna nilivyojipanga kushirikiana na viongozi wengine watakaochaguliwa kuunda serikali katika kusimamia utatuzi wa kero mbali mbali zinazowakabili wananchi wa Same katika sekta ya Afya, Elimu, Kilimo, Ufugaji na utatuzi wa migogoro ya Ardhi baina ya wafugaji na wakulima inayowakabili wananchi katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Same Magharibi.
Mbali na mambo hayo pia nilieleza endapo ntapata ridhaa ya Chama na wananchi ntashirikiana kwa karibu na wadau wa elimu na wanaharakati wa masuala ya Elimu kuishinikiza serikali kutoa Elimu bila ubaguzi hususani kwa watu wenye mahitaji maalum na mabinti wanaopata ujauzito wakiwa mashuleni ili kuwapa fursa ya kujiendeleza na kufikia malengo yao bila kukwamishwa na sheria, kanuni au matamko kandamizi.
Naombeni ushirikiano wenu katika safari hii muhimu kwa ustawi wa Taifa letu, Mungu Awabariki wotee [emoji120].
Fredrick Mbwambo Justine.