Nimekupenda bureIla mikoa ya huku mnapitia magumu, kwetu tangu tukiwa watoto ukipika chakula lazima uweke cha mgeni na cha watoto watakacho kula saa 12 jioni ili wasisinzie bila kula usiku.
Mpaka leo huwezi kwenda mama yangu jion saa 10 usikute chakula.
Tukila mchana lazima kitolewe cha kuku, mbwa, kilichobaki kinatunzwa jikoni kwa ajili ya mgeni akija gafla. Hii ratiba ni almost kila siku.
Embu tuseme hii life ni la kijijini.
Huku mjini ndio kuna bajeti lakini mimi nikipika chakula napika changu tu ila.mboga lazima iwe nyingi ili mgeni akitokea nimsongee hata ugali.
Nyie watu wengine ni wachoyo hivi mwanaume anaweza kula ka ugali kadogo kama ngumi?
Yani kuna familia za ajabu sana mkuu. Walinikomalia tena shemeji ndio kanikazania kwa kua nilikua mgen ikabidi tu nifuate maelekezoHuo sio ustaarabu kwa mgeni. Kwa kawaida sisi unapomkaribisha mgeni kula unaenda nae mezani unamfunulia mahotpot ikiwezekana unamuonesha na maji ya kunawa tena unaanza kupakua mwenyeji, hiyo inampa confidence mgeni ajikadirie yeye kulingana na mwenendo wa mwenyeji wake.
Sasa wao wakakuacha ukafanya makamuzi mwisho lazima ujihisi fedheha
Aisee Kuna watu Wana roho mbaya,[emoji23][emoji23]Inanikumbusha mwaka 2012 nilipata kazi Singida, nikafikia kwa mtoto wa mjombaake mama.
Alikuwa ni mshkaji wa miaka kama 35 or 38 hivi.
Dah, mwamba alikuwa anapika wali robo. Mimi nishazoea kufukia mzee,nikamwambia aka sema niwe napika mimi nkasema poa.
Nikanunua vyakula,nikawa napika kilo nzima jioni mahesabu na kesho tunywee chai ila kila nkiamka asubuhi nakuta ubwabwa umelowekwa ila yeye keshatoka.
Nikajua yeye ndo anaefanya hivyo akishakula,nkaona so kesi nkaanza kula mgahawani tuu kibishi.
Kuna wengine sio life style ni uchoyo tuu wa asili.
Na hapo ulipo itakuwa huyo mke wa jamaa ndo anasauti hapo ndani,so anaamua atakavyo.
Acha kabisa na chalii alikuwa akiona wageni ndo hapapikwi chochotee.Aisee Kuna watu Wana roho mbaya,[emoji23][emoji23]
Good hapo ulicheza sanaKuna siku nilienda mkoa flani sasa ile ndugu wanakufosi unafikiaje Lodge na sisi tupo? nikaona sio kesi acha nifikie kwao nikawa natoka usbh narudi usiku siku ya kwanza wakaleta chapati mbili mbili na maharage na chai nikasema poa sio mbaya labda uzungu kesho tena ivo ivo na siku ya tatu vile vile nikaaaga inabidi kesho twende wilayani sina uhakika kama tutarudi au tutalala huko huko, asbh nikatoka na begi langu nikahamia Lodge mbali kidogo na wanapoishi nimekaa siku tatu sasa siku moja jioni nazungukia bar za pale mjini nikakutana na baba mwenye nyumba akashtuka upo ikabidi nizuge ndio tumeingia muda huu tunatafuta chakula tuendelee na safari.
Kijana unakula msosi heavy kama wa komandoo mafunzoni 😅Kuna kipindi nilitoka jkt hapo Kabuku Tanga nikaona sio kesi wacha nipitie hapo DSM kwa anko, ile nimefika siku ya kwanza jioni hivi aunt anaanza kuandaa Mchele Anko akamwambia ongeza kipimo ( maana tunafahamiana vizuri na anko amewahi kaa home enzi hizo anasoma). Sasa wakati wa kula aunt akataka anipakulie msosi ndipo anko akasema wewe mke wangu hebu tujipakulie sisi yeye atajikadiria kwa namna awezavyo. Kufupisha stori nikajikadiria nikapiga mpaka nikashiba nikamuacha shangazi akitumbua macho kwa namna haamini kilichotokea kwwnye hotpot.
Dsm kumbe life tight hvyo?Mtu unakula ugali kama ngumi ya mtoto na dagaa tatu mchuzi ndoo ya maji ....harafu ukiwa Kwa bed unataka kupiga goli 3 ,na upelekee moto ,my friend utaendelea kujiona huna nguvu ,kumbe hata nguvu za kawaida tu huna ....
Watu dsm wanashinda njaa kiasi kwamba wanakosa hata nguvu za kuongea ,..
Umenifanya nicheke sana kiongozi. Umetoa uzoefu wako kaka.Kuna siku nilikuwa na wageni Fulani watasha sehemu Fulani, wao wanakula Kidogo sana, Mimi nikamsoma dereva maana mswahili mwenzangu, yeye anajifanya anazuga alafu anaaga anaenda kufata vocha aloo Kumbe anaenda kwenye mgahawa wa karibu na kupiga mapigo ya kibongo. Niliunga tela fasta siku inayofata nikamwambia na Mimi nataka nitume M-pesa sehemu akaniambia njiani asee Mimi huwa sishibi hiyo misosi nikamwambia sio peke yako, alicheka sana. Nikaagiza ugali sahani mbili chap, dereva alicheka sana. Hii ndio mipango. [emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23]Umenikumbusha kuna rafiki yangu anatoka mwz kajaa dar kakaribishwa na mtoto wa babaake mdogo wajumuike pamoja lunch. msosi katwanga wotee na kuacha kijispece cha jion punde si punde familia ikajumuika na madogo wa shule wamefika toka shule kwenye mahotpot hola mwambaa kakomba na matonge hadi vile vmchuzi vya pembeni lile toto la form one likaanza kulia et leo halijala kitu chochote school af msosi umeisha wotee jamaa alijisikia vibaya sana alijua et ilikuwa ni kwaajiri yake mgeni ikabdi avunge akawaachia 50000 mpka leo anasemaga mie siwezi kula na watu wa dar niwachoyo Sana akifikaga dar anakuja kajipanga Sana huwa anakupigia simu upo wapi njoo sehemu flan uone wanaume tunavyokula mwambaa kufuta kuku mzmaaa ni sekunde tuu tenaa huku anakupigisha story
Huyo nae kazidi, kuku mzima peke yake hiyo ni kufuru.Umenikumbusha kuna rafiki yangu anatoka mwz kajaa dar kakaribishwa na mtoto wa babaake mdogo wajumuike pamoja lunch. msosi katwanga wotee na kuacha kijispece cha jion punde si punde familia ikajumuika na madogo wa shule wamefika toka shule kwenye mahotpot hola mwambaa kakomba na matonge hadi vile vmchuzi vya pembeni lile toto la form one likaanza kulia et leo halijala kitu chochote school af msosi umeisha wotee jamaa alijisikia vibaya sana alijua et ilikuwa ni kwaajiri yake mgeni ikabdi avunge akawaachia 50000 mpka leo anasemaga mie siwezi kula na watu wa dar niwachoyo Sana akifikaga dar anakuja kajipanga Sana huwa anakupigia simu upo wapi njoo sehemu flan uone wanaume tunavyokula mwambaa kufuta kuku mzmaaa ni sekunde tuu tenaa huku anakupigisha story
[emoji23] NimechekaaaFirst appointment tangu nilipangiwa Pwani, kutokana na bajeti finyu niliyokuwa nayo sikula chochote njia nzima mpaka nafika
Miaka hiyo hakukuwa na bodaboda hivyo kushuka stendi nikaelekezwa tu kwa mwenyeji wangu. Alikuwa mzee maarufu sana hiyo mitaa, nikatembea mwendo wa dakika kumi nikafika. Ilikuwa kwenye saa nane hivi
Nikakuta wako mesi wanagonga wali maharagwe na samaki, nikakaribishwa kwa bashasha sana lakini nikazuga nimeshiba sana maana njiani gari ilisimama mahali tukala ( najuta kufanya vile)
Ningekuwa nafahamu taratibu za watu ningekubali kula siku ile, lakini bila kujua nilijipa moyo kwamba jioni nitakula nishibe maana nilikotoka nilikuwa nimekunywa chai rangi na andazi moja tu asubuhi
Yule mzee alikuwa mkarimu na mtu wa story sana kwahiyo mchana wote tulishinda hapo kwake upenuni mpaka jioni alipoenda msikitini
Sasa mimi njaa inauma mida inasogea kigiza kinaingia ila sioni harakati zozote za maandalizi ya dinner ( ilikuwa familia ya watu watano baba, mama, mabinti wawili na kijana wa kiume)
Nikajipa moyo kwamba pengine kilipikwa na cha jioni ule mchana.. Kufika saa mbili usiku mzee akarudi na mkate! Kwa mawazo yangu ulikuwa kwa ajili ya kesho asubuhi
Dakika chache baada ya mzee kurudi nikaitwa ndani kwa ajili ya dinner..! Lahaula rasuli! Dinner ilikuwa kikombe cha chai ya rangi na silesi mbili za mkate[emoji23]
Kwanza nilidhani tunapasha matumbo joto halafu mahanjumati yaja.. Pengine misamaki tasi, kolekole, pweza wa kubanikwa chapati na mkate wa kumimina ama kiporo cha mchana! Naona kila anayemaliza ananyanyuka mezani.. Nilikuwa wa mwisho
Hakuna kitu kinatesa kama njaa ya ugenini..!!!