davejillaonecka
JF-Expert Member
- Oct 17, 2018
- 697
- 749
Mzee alikua lijendi haswaaaHata na mimi nashukuru nilizaliwa familiya ilokuwa na uwezo wa kilisha mtaa mzima so ishu ya vyakula nyumbani ni tangu tukiwa wadogo.
Nakumbuka tukiwa wadogo baba akiwa hai, kwanza akitoka safari anachinja ng'ombe kijiji kizima wakija kumsalimia wanakula na nyama wanabeba.
Akitoka safari chakula kinapikwa kuanzia asubuhi hadi jioni yaani kila anekuja kumsalimia baba lazima ale.
Maisha ya mama baba akiwa hai ni full time jikoni na wafanyakazi wawili
Nyumbani wageni ni full time na wengine wanalala mpaka baba akisafiri tena ndo mama anapumzika.
wabibi, baba akifika kila jion wanafata mafuta ya taa na sukali hao wote lazima waondoke wamekula, chakula kikiisha lazima mama apike kingine hata kama ni usiku.
Nyumba yenye chakula cha kutosha haikosi wageni na wafanyakazi wa kutosha. Kwetu kulikuwa kama sherehe most of the times.
Siku baba yangu amefariki watu wazee kwa vijana walilia sana. Msiba ulimaliza zaidi ya mwezi na zilichinjwa ngombe zaidi ya 10 sikumbuki idadi maana tulikwa nazo kama 300 hivi.
Kama una uwezo lisha watu washibe ili ukifa tupate na machozi ya kukulilia.
Msibani kwa baba watu walikuwa wanalia hivi:,
Wazuri hawadumu, tulikula bure, nyama tulipewa bure, sukari bure mafuta bureee, wewe mtoto nini kimekupata? Wanapiga geneza wamama, amkaaaaa sisi tunakula wapi? Amkaaa watoto wetu wanalipiwa na ada na nani? fulani amkaaaaaaa. Loh nimekumbuka mbali.
Kwani lazima ule ww ushawaletea zawadi na umeona msosi mdogo ikifika mida ya jioni tafuta sehemu kula kitimoto yako kilo na ndizi mbili ukisindikiza na coke ya baridiiiii mchana tafuta hata mama lishe kula wali wako hapo nyumbani wana bajeti zao temana nao kabisa.Huu ugeni jamani,
Nipo ugenini hapa nilipofikia nimejitahidi nisiwe nakula bure, nimefika ijumaa na Ile Ile ijumaa nilileta mafuta ya kula Lita 3.
Hapo hapo nikanunua na nguruwe kilo 2, huwa sipend Sana free lunch. Sasa bana hapa nilipo wanapika msosi kidogo sana yaani daah sijui ndo walivozoea.
Daah nakula slow slow Ila sishibi. Ijumaa na jumamosi nimekula sahani mbili tu yaani mchana napiga chenga, sipendi kuhudhuria kila mida ya misosi.
Sasa Leo jioni (muda si mrefu sijaanza kuandika hii post) Wife wa jamaa wakaleta msosi kama kawaida yao kidogo sana. Nimekaa nazuga zuga naangalia TV uvumilivu ukanishinda nikaona ngoja nimege ugali.
Nikakata nusu, maana nilijua tupo wawili mi na jamaa mwenye nyumba. Nikahisi wife wa jamaa na mdogo wake wanakula uko jikoni. Ile nimekata nusu naona wife wa jamaa na mdogo wake nao Wanakuja daah!
Basi shem ikabidi azuge kama kashiba. Mdogo wa Shem ndo akakata Ile nusu, uliobaki ndo jamaa kala. Nimejisikia vibaya mno natamani niondoke Lee. Yaani jumatatu naona mbali.
Chief kitimoto kilo nzima na ndizi unaikandamiza yote?Kwani lazima ule ww ushawaletea zawadi na umeona msosi mdogo ikifika mida ya jioni tafuta sehemu kula kitimoto yako kilo na ndizi mbili ukisindikiza na coke ya baridiiiii mchana tafuta hata mama lishe kula wali wako hapo nyumbani wana bajeti zao temana nao kabisa.
Mimi nilikua nikienda kwa shangazi yangu asubuhi natoka nachukua mikate miwili mmoja wa kwao mmoja wangu nanunua na blueband au peanut butter nikifika muda wa chai naiweka yote mezani wanaanza kuleta bajeti eti mmoja ubaki hapo ndipo nawaambia huu nakula mwenyewe ili nisiharibu ratiba zenu huo kuleni nyie mwanzo walipata tabu ila walizoea mchana natoka nikirudi jioni napitia sehemu ya nyama au kuku naagiza chakula najipigia nikirud home nimeshiba nagusa gusa vijiko viwili nalala nikiwa njema kabisa. Kama huna hela kufa njaa tu hamna namna
Na coke ya baridiiiii kama barafuChief kitimoto kilo nzima na ndizi unaikandamiza yote?
AiseNa coke ya baridiiiii kama barafu
Usishangae ukiamua kula haramu basi kula kweli sio unaonja onja vinyama vinaishia kwenye menoAise
Doh!Huu ugeni jamani,
Nipo ugenini hapa nilipofikia nimejitahidi nisiwe nakula bure, nimefika ijumaa na Ile Ile ijumaa nilileta mafuta ya kula Lita 3.
Hapo hapo nikanunua na nguruwe kilo 2, huwa sipend Sana free lunch. Sasa bana hapa nilipo wanapika msosi kidogo sana yaani daah sijui ndo walivozoea.
Daah nakula slow slow Ila sishibi. Ijumaa na jumamosi nimekula sahani mbili tu yaani mchana napiga chenga, sipendi kuhudhuria kila mida ya misosi.
Sasa Leo jioni (muda si mrefu sijaanza kuandika hii post) Wife wa jamaa wakaleta msosi kama kawaida yao kidogo sana. Nimekaa nazuga zuga naangalia TV uvumilivu ukanishinda nikaona ngoja nimege ugali.
Nikakata nusu, maana nilijua tupo wawili mi na jamaa mwenye nyumba. Nikahisi wife wa jamaa na mdogo wake wanakula uko jikoni. Ile nimekata nusu naona wife wa jamaa na mdogo wake nao Wanakuja daah!
Basi shem ikabidi azuge kama kashiba. Mdogo wa Shem ndo akakata Ile nusu, uliobaki ndo jamaa kala. Nimejisikia vibaya mno natamani niondoke Lee. Yaani jumatatu naona mbali.
Daaah mmechafukwa aiseUsishangae ukiamua kula haramu basi kula kweli sio unaonja onja vinyama vinaishia kwenye meno
Hii ilishanikuta, tulikuwa na jamaa yangu Dar. Aisee katika maisha yangu sijawahi kula kijiko kimoja Cha wali.
Nikajiuliza hii ni kutufukuza au ni nini, kibaya zaidi tulienda kumsalimia tu mchana. Chakula kilicholetwa Cha watu wazima watano, Kwa hakika, mtoto wa miaka SITA hashibi.
Mpaka Leo sijawahi PATA jawabu ya kile kitendawili.
Aseeh sisi kwetu mgeni haendi peke yake mezani anaenda na mwenyeji wake. Yan hiyo inamfanya anajisikia comfortable kuliko kumuacha peke ake. Sio ustaarabu kabisaYani kuna familia za ajabu sana mkuu. Walinikomalia tena shemeji ndio kanikazania kwa kua nilikua mgen ikabidi tu nifuate maelekezo
Kilichotokea ndio hicho wanabaki kushangaa tu .
Hahaa.. eti hapa katikati[emoji23][emoji23]Si shangaz yetu yan mke wa uncle ulikuwa ukitoka kujisavia chakula unakatwa jicho hilo haroo nilikaa nao miezi mitano nikaenda kupambana mbele huko, watu wa hapa katikati hapa kama enaenda Kilimanjaro kabla hujafika kwa wapare, hapa katikati kidogo wanasifika kwa uchoyo coz chakula kwao wanaona dili sana kwa kuwa watokea sehem msos wa shida. Utawasikia, mtamisamehe,mtamiona,
Sasa kuku mzima anakushinda nini?Huyo nae kazidi, kuku mzima peke yake hiyo ni kufuru.
Aiseeeee...nimecheka Kwa sauti Hadi wananishangaaHuu ugeni jamani,
Nipo ugenini hapa nilipofikia nimejitahidi nisiwe nakula bure, nimefika ijumaa na Ile Ile ijumaa nilileta mafuta ya kula Lita 3.
Hapo hapo nikanunua na nguruwe kilo 2, huwa sipend Sana free lunch. Sasa bana hapa nilipo wanapika msosi kidogo sana yaani daah sijui ndo walivozoea.
Daah nakula slow slow Ila sishibi. Ijumaa na jumamosi nimekula sahani mbili tu yaani mchana napiga chenga, sipendi kuhudhuria kila mida ya misosi.
Sasa Leo jioni (muda si mrefu sijaanza kuandika hii post) Wife wa jamaa wakaleta msosi kama kawaida yao kidogo sana. Nimekaa nazuga zuga naangalia TV uvumilivu ukanishinda nikaona ngoja nimege ugali.
Nikakata nusu, maana nilijua tupo wawili mi na jamaa mwenye nyumba. Nikahisi wife wa jamaa na mdogo wake wanakula uko jikoni. Ile nimekata nusu naona wife wa jamaa na mdogo wake nao Wanakuja daah!
Basi shem ikabidi azuge kama kashiba. Mdogo wa Shem ndo akakata Ile nusu, uliobaki ndo jamaa kala. Nimejisikia vibaya mno natamani niondoke Lee. Yaani jumatatu naona mbali.
Swala sio life la town ishu ni kipato ,kuna watu wako town wanakula msosi heavy na wengine wako village msosi kiduchuKusema kweli mjini hasa Dar watu wanakula share ndogo sana. Chakula kinapikwa hadi unajiwazia kweli hiki watu wanashiba? Ila ndio life la town!!
Na kwa nini ule kuku mzima mara moja, tena mwenyewe? Huo ni ulaku tu hakuna kingine...Sasa kuku mzima anakushinda nini?