Nipo ugenini, wanapika chakula kidogo mno

Nipo ugenini, wanapika chakula kidogo mno

Kila mtu kakomaa mjini bajeti mjini bajeti.

Huo ni mji gani wa kuishi kama huwezi mudu chakula?
Yes, mjini hatuna mashamba so ni mwendo wa budget tu. Vipato havizunguki 30days unadhani watu wanafanyaje zaidi ya kuishi kwa strict budget?
 
Sasa wanakuaje mabonge vile kama hawashibi vizuri?
Junk foods mkuu, mtu akipata 2500 anaenda kibanda chips anakula chips yai na pepsi yake unadhani habongeki?

Japo binafsi naona matumbo yetu yanahitaji kiwango kidogo, as wengi hatufanyi kazi za nguvu. Ndio mana sahani moja mtu yupo sawa tu, wakija kutoka vijijini wanapata shida coz wamezoea kazi ngumu na misosi mingi.
 
Huu ugeni jamani,

Nipo ugenini hapa nilipofikia nimejitahidi nisiwe nakula bure, nimefika ijumaa na Ile Ile ijumaa nilileta mafuta ya kula Lita 3.

Hapo hapo nikanunua na nguruwe kilo 2, huwa sipend Sana free lunch. Sasa bana hapa nilipo wanapika msosi kidogo sana yaani daah sijui ndo walivozoea.

Daah nakula slow slow Ila sishibi. Ijumaa na jumamosi nimekula sahani mbili tu yaani mchana napiga chenga, sipendi kuhudhuria kila mida ya misosi.

Sasa Leo jioni (muda si mrefu sijaanza kuandika hii post) Wife wa jamaa wakaleta msosi kama kawaida yao kidogo sana. Nimekaa nazuga zuga naangalia TV uvumilivu ukanishinda nikaona ngoja nimege ugali.

Nikakata nusu, maana nilijua tupo wawili mi na jamaa mwenye nyumba. Nikahisi wife wa jamaa na mdogo wake wanakula uko jikoni. Ile nimekata nusu naona wife wa jamaa na mdogo wake nao Wanakuja daah!

Basi shem ikabidi azuge kama kashiba. Mdogo wa Shem ndo akakata Ile nusu, uliobaki ndo jamaa kala. Nimejisikia vibaya mno natamani niondoke Lee. Yaani jumatatu naona mbali.
😂😂😁😁😁😁😁😁, labda huwa hawafanyi kazi ngumu.., halafu we kumbe unabeba zege
 
Yes, mjini hatuna mashamba so ni mwendo wa budget tu. Vipato havizunguki 30days unadhani watu wanafanyaje zaidi ya kuishi kwa strict budget?
Sijawahi ona hiyo ya chakula kinatolewa kwa uchache kiasi hicho
 
Mtu unakula ugali kama ngumi ya mtoto na dagaa tatu mchuzi ndoo ya maji ....harafu ukiwa Kwa bed unataka kupiga goli 3 ,na upelekee moto ,my friend utaendelea kujiona huna nguvu ,kumbe hata nguvu za kawaida tu huna ....

Watu dsm wanashinda njaa kiasi kwamba wanakosa hata nguvu za kuongea ,..
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
[emoji23][emoji23][emoji23] familia ikiwa kubwa hizo ndio mbizu za cuba, ajabu sasa hao wenye mji asubuhi anapita sehemu anapiga mchemsho wake, mchana anaoita shishi food anapiga makange yake ya kuku, mda wa kurudii nyumbani anapitia chips nyama anapitiliza chumbani, wanakuja yeye na mkewe wanashiba vizurii Sana, badae wanatoka chumbani wanakuja sitting room kujumuika na nyie wageni ndugu na jamaa mliokimbilia mjini kwa mjomba kudadeki kilo moja ya wali mnakula watu kumi na nyama nusu[emoji23][emoji23][emoji23]

Yani jumba zuri, magari nk wenye afya nzuri ni baba na mama Ila kuanzia watoto wamekonda balaa kumbe ni lishe duni
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
Kuna jamaa tulikua tunaishi magetoni nyumba moja yeye anakaa chumba kinachofata baada ya changu..huyo jamaa alikua anaweka bajeti ya mwezi mzima anatumia laki 1 tu kwa chakula
Anaweza akanunua nyama robo akaikaanga akala hata siku 3 anachukua finyango mbili anamix na spinach/chainizi/sukumawiki anasonga na ugali anakula
Sasa mtu kama huyu akija kua na familia atakua na bajeti kali sana
Huyu kaanza mazoezi ya family budget mapema sana [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom