Ndio maana wasukuma wakienda mijini wanateseka sana..ugenini wewe jilie zako nje ukija homu unagusa tonge moja tu ya kuzugia.Huu ugeni jamani,
Nipo ugenini hapa nilipofikia nimejitahidi nisiwe nakula bure, nimefika ijumaa na Ile Ile ijumaa nilileta mafuta ya kula Lita 3.
Hapo hapo nikanunua na nguruwe kilo 2, huwa sipend Sana free lunch. Sasa bana hapa nilipo wanapika msosi kidogo sana yaani daah sijui ndo walivozoea.
Daah nakula slow slow Ila sishibi. Ijumaa na jumamosi nimekula sahani mbili tu yaani mchana napiga chenga, sipendi kuhudhuria kila mida ya misosi.
Sasa Leo jioni (muda si mrefu sijaanza kuandika hii post) Wife wa jamaa wakaleta msosi kama kawaida yao kidogo sana. Nimekaa nazuga zuga naangalia TV uvumilivu ukanishinda nikaona ngoja nimege ugali.
Nikakata nusu, maana nilijua tupo wawili mi na jamaa mwenye nyumba. Nikahisi wife wa jamaa na mdogo wake wanakula uko jikoni. Ile nimekata nusu naona wife wa jamaa na mdogo wake nao Wanakuja daah!
Basi shem ikabidi azuge kama kashiba. Mdogo wa Shem ndo akakata Ile nusu, uliobaki ndo jamaa kala. Nimejisikia vibaya mno natamani niondoke Lee. Yaani jumatatu naona mbali.
Good recommendation. [emoji122][emoji122][emoji122]Hiyo imenikutaga aisee, nilienda kwa jamaa alikomalia kweli nistay kwao kipindi nafuatilia mambo flani hv mkoa ule, sasa chakula daah ani inabidi nile taratibu ili tuondoke wote mezani, na pia ni kiduchu yani kale kaugali daaah!![emoji29] nilikua nakaza moyo sana[emoji28]
Sasa ajabu zaidi ikitokea nimetoka misere na mwana tukiingia mahali kula alikua analalamika kwann nisile kutosha home na wakati kinachotengwa ni kidogo sana pale mezani
Aisee alipokuja mkoani kwangu, nyumbani alijishtukia mwenyewe[emoji28] maana ile msosi najipigilia mezani ni ya kufa mtu, akaanza kusema daah inawezekana kule ulikua hushibi kaka, nisamehe bure, nikawa namvungia tu namwambia amna nimeanza speed ya kula karibuni tu, ila kiuhalisia nilikua nasongolewa na njaa mpaka nakula mgahawani
Mimi nafikiri mgeni akija hebu chakula kipikwe cha kutosha siku za mwanzoni then angalia speed yake ya kula unamkadiria kama ni mlaji unaenda nae sawa na kama sio mlaji unapunguza kipimo cha diko ili kuepuka uharibifu ila ni vizuri kumkarimu mtu chakula afurahie aisee....
Ushauri mzuri sanaZuga kula, then kashibe hotelini
Nyanda za juu kusini. IringaKusini gan yenye misosi maan npo huku 5years chakula ni shda familia zinakula milo mi2 had mmoja baada ya msimu wa korosho
30% wanalima mahind na wakulima wachache sana wenye uwezo wa kuvuna magunia ya mahindi 7+
Huku n njaaa
Nashukuru Wadau kwa michango yenu
Ila nipo mtwara ndani ndani , kwanza ni kijijin hakuna gest kbsa,Cha pili migahawa imefungwa maana wengi hapa wamefunga si mnajua huu mwezi wa Ramadhani,
Pale sokon Kuna watu jion wanauza uji na ftali ,
Ila apo wanapo uza Kuna duka la dawa la huyu dada nilipofikia na anauza mdogo wake , Jana nimeenda nikaona nikinywa uji dogo atakuja kuchoma nikala chungwa moja,
Daah yan
Ukienda ugenini kale kitaa achana na msosi wa shikamoo shemeji.Huu ugeni jamani,
Nipo ugenini hapa nilipofikia nimejitahidi nisiwe nakula bure, nimefika ijumaa na Ile Ile ijumaa nilileta mafuta ya kula Lita 3.
Hapo hapo nikanunua na nguruwe kilo 2, huwa sipend Sana free lunch. Sasa bana hapa nilipo wanapika msosi kidogo sana yaani daah sijui ndo walivozoea.
Daah nakula slow slow Ila sishibi. Ijumaa na jumamosi nimekula sahani mbili tu yaani mchana napiga chenga, sipendi kuhudhuria kila mida ya misosi.
Sasa Leo jioni (muda si mrefu sijaanza kuandika hii post) Wife wa jamaa wakaleta msosi kama kawaida yao kidogo sana. Nimekaa nazuga zuga naangalia TV uvumilivu ukanishinda nikaona ngoja nimege ugali.
Nikakata nusu, maana nilijua tupo wawili mi na jamaa mwenye nyumba. Nikahisi wife wa jamaa na mdogo wake wanakula uko jikoni. Ile nimekata nusu naona wife wa jamaa na mdogo wake nao Wanakuja daah!
Basi shem ikabidi azuge kama kashiba. Mdogo wa Shem ndo akakata Ile nusu, uliobaki ndo jamaa kala. Nimejisikia vibaya mno natamani niondoke Lee. Yaani jumatatu naona mbali.
Umeandika vizuri tu na umeeleweka safi. HIYO FAMILIA NZURI SANA, MPAKA NATAMANI NINGEKUWA MIMI NIMEPITA HAPO. KWAKUWA HUJATAJA MKOA SIO MBAYA UNGETAJA INGEKUWA POA ILI SIKU NIKIKATIZA HUKO NIKAWASALIMU.Mwaka jana kuna project nilienda kufanya mkoa fulani hivi ya kama wik mbili nilipofika nikapokelewa na mwenyeji wangu. Basi baada ya stori mbili tatu nikamwambia anipeleke Lodge nzuri. Jamaa akaniambia Lodge ya nini wakati home kwake kuna chumba cha wageni. Nikakataa lkn jamaa akasisitiza niende nikaona isiwe case. Nikajiongeza tukapitia kwa mangi nikafungasha haswa vitu vya ndani mamichele,unga wa ngano mafuta,tambi na mazaga zaga kibao nikamuuliza kama ana frigi akasema anayo tukapitia na buchani kununua nyama na masoseji. Basi tukafika home tukapokelewa na mke wake na watoto wake wanne wawili wa kike wawili wa kiume. Kesho yake nikaanza mishe. Yaani wale watu ni wakarimu ajabu. Shemeji kila asubuhi baada ya heavy breakfast kabla sijaondoka ananiuliza nikirudi nitapendelea kula nini,wale watoto wa kike asubuhi wananiambia niwatolee nguo chafu wafue. Mi ni Mkristo na wao ni Waislamu safi lkn awajawahi kunistrict kupiga mambo yetu yale. Tukienda bar na yule jamaa mi nakamatia vitu yeye anacharaza zake Redbull tukiondoka tunachukua nyama ya mbuzi kilo tunarudi home tunakula na familia yake fresh tuu. Siku ya kuondoka ilivyofika hakuna aliyekuwa anataka niondoke na walihuzunika sana hadi kulia. Mpaka leo ni kama ndugu zangu kabisa wananitembelea na familia yangu huwa tunafunga safari kwenda kuwatembelea. Sorry kwa uandishi mbovu.
Unaweza kutafuta pesa ukiwa na njaa?Mnawaza kula kula tu ukiwa na pesa hata njaa usikii we ni choka mbaya tafuta pesa utakuja kuniambia
Huyu kuku usimnunuwe ushanunua kitimoto inatosha.Ndugu kama ulivosoma post sipend vitonga , huku mtwara vijijini hakuna gest kbsa na Kuna ishu muhimu ilinileta ,
Nachangia Sana na Leo nanunua kuku , cpendi vitonga
Kitimoto alivyo mtamu unaanzaje kula nyama mbili tu? Si kutafutiana. lawama?πππJapo kwenye kitimoto pamekukera mgeni alikuwa muungwana ππ
Niliwahi kumtembelea shangazi yangu Dar kiukweli nilishangaa. Unakuta msosi unaopikwa mtam sana ila mdogo ilibidi baada ya kula natoka kwenda kitaa kujaziaKusema kweli mjini hasa Dar watu wanakula share ndogo sana. Chakula kinapikwa hadi unajiwazia kweli hiki watu wanashiba? Ila ndio life la town!!
Mama ana Roho ya utakatifu kabisa. Naambieni wazazi Wetu, bibi na Babu wa ZETU ni watakatifu maana walikuwa na ukarimu mkubwa sana. Walitunza misitu, wakapata Mvua nyingi na kulima mazao Kwa wingi hivyo kuwa na chakula Cha kutosha. Ila sikuhizi tunaiga uzungu kuliko kawaida, tumekata misitu, Mvua tabu, mazoa Kidogo. Sasa chakula tunakula Kwa kujilamba tu. [emoji120][emoji120][emoji120]kuna sisi tulio kulia maisha ya kula kila mda tukifika sehem ya bajet bajet hatukai tuna lala mbereee
nakumbuka tuu zamani tulipokuwa wadogo home
maziwa yakumwaga
matunda kamayote
nyama ya kuku usiseme
mahindi
yani unakuta namsosi wakutosha unapikwa tunakula na kusaza
Hadi leo nyumba ambayo chakula hakibaki naiona ina mapungufu
mama alituambia msimalize chakula chote lazima kibaki kidogo anaweza kuja mtu mwenye njaa Kali mkashindwa kumsaidia japo tonge moja na akawafia
tenga msosi mtu ale aache kikibaki kesho kinapaswa watu wananywea chai