Nipo ugenini, wanapika chakula kidogo mno

Nipo ugenini, wanapika chakula kidogo mno

Huu ugeni jamani,

Nipo ugenini hapa nilipofikia nimejitahidi nisiwe nakula bure, nimefika ijumaa na Ile Ile ijumaa nilileta mafuta ya kula Lita 3.

Hapo hapo nikanunua na nguruwe kilo 2, huwa sipend Sana free lunch. Sasa bana hapa nilipo wanapika msosi kidogo sana yaani daah sijui ndo walivozoea.

Daah nakula slow slow Ila sishibi. Ijumaa na jumamosi nimekula sahani mbili tu yaani mchana napiga chenga, sipendi kuhudhuria kila mida ya misosi.

Sasa Leo jioni (muda si mrefu sijaanza kuandika hii post) Wife wa jamaa wakaleta msosi kama kawaida yao kidogo sana. Nimekaa nazuga zuga naangalia TV uvumilivu ukanishinda nikaona ngoja nimege ugali.

Nikakata nusu, maana nilijua tupo wawili mi na jamaa mwenye nyumba. Nikahisi wife wa jamaa na mdogo wake wanakula uko jikoni. Ile nimekata nusu naona wife wa jamaa na mdogo wake nao Wanakuja daah!

Basi shem ikabidi azuge kama kashiba. Mdogo wa Shem ndo akakata Ile nusu, uliobaki ndo jamaa kala. Nimejisikia vibaya mno natamani niondoke Lee. Yaani jumatatu naona mbali.

Ondoka tu, maana ungeweza kwenda kula tu huko nje.
 
Pigia salute kwa mwamba🫡 so unashangaa!!, hata mi kwangu sipendagi marafki urojo urojo yan mtu tonge mbiri ananawa hua siwaelewi kabisa, mtu unagonga ugari robo(minimam) mlo mmoja, pembeni upaja wa kuku na hips zake, supu bakuri la pembeni af mboga za majani pale unamalizia na juice af unamwita wife aje akunawishe, unawasha fen unangalia taarifa ya habari, sasa mwizi aje ajikatize usiku namyonga na[emoji123] sihami MBEYA🫶
Bangi zinachangi sana kufanya watu kula sana
 
Huu ugeni jamani,

Nipo ugenini hapa nilipofikia nimejitahidi nisiwe nakula bure, nimefika ijumaa na Ile Ile ijumaa nilileta mafuta ya kula Lita 3.

Hapo hapo nikanunua na nguruwe kilo 2, huwa sipend Sana free lunch. Sasa bana hapa nilipo wanapika msosi kidogo sana yaani daah sijui ndo walivozoea.

Daah nakula slow slow Ila sishibi. Ijumaa na jumamosi nimekula sahani mbili tu yaani mchana napiga chenga, sipendi kuhudhuria kila mida ya misosi.

Sasa Leo jioni (muda si mrefu sijaanza kuandika hii post) Wife wa jamaa wakaleta msosi kama kawaida yao kidogo sana. Nimekaa nazuga zuga naangalia TV uvumilivu ukanishinda nikaona ngoja nimege ugali.

Nikakata nusu, maana nilijua tupo wawili mi na jamaa mwenye nyumba. Nikahisi wife wa jamaa na mdogo wake wanakula uko jikoni. Ile nimekata nusu naona wife wa jamaa na mdogo wake nao Wanakuja daah!

Basi shem ikabidi azuge kama kashiba. Mdogo wa Shem ndo akakata Ile nusu, uliobaki ndo jamaa kala. Nimejisikia vibaya mno natamani niondoke Lee. Yaani jumatatu naona mbali.
Hii mambo huwa inategemea na mwanaume wa familia kumpush mkewe., maana mke anaweza kuwa hajiongezi kulingana na idadi ya watu waliopo., mnaweza kuwa mmezoea kupika chakula cha watu watatu wakaongezeka wageni watatu, obvious kipimo kitaongezeka ila ukikuta mke anapika ratio ile ile wakati watu wameongezeka hapo lazima kuna watu watateseka kimoyomoyo.
 
Imagine mtu anaenda kununua nyanya mbili, kitunguu kimoja, mafuta ya jero, hoho moja, karoti moja, dagaa wa buku na unga nusu na robo.

Unadhani kuna nini hapo? Hongera mkuu kama hujawahi ona au kuishi namna hiyo.
Ukiwa maduka ya Mangi hayo mambo ya kawaida.
Anatumwa mtoto anunue mafuta ya 500
Unga Robo 3
 
Aisee hii iliwahi kunikuta kota za maafisa wa polisi Nyamkazi Bukoba ile familia ilikuwa inapika chakula kidogo sana nakula sishibi alafu ukimaliza kula unapewa maji ya bariiiidi sasa njaayake usipime ,jicho linanitoka kila nkitaka kutoroka nkale mgahawani watoto wa pale wananifata naishia kuzunguka nao na kurudi,,,nilivyorudi nyumbani nikaulizwa unaumwa nikasema hapana,,ila nikawa nakula kuliko kawaida mzee akasema huyu alikuwa na njaa ikabidi nisimulie,,,maisha ya mjini ni ya kipumbavu mno unakuwa jehanamu kabla hujafa!!
Tatizo ulienda kwa watu masikini, kimasikini
 
Solution ni kuacha kufikia kwa watu. Kwanza kufikia kwa watu unabadili utaratibu wao wa maisha. Ni heri upange ratiba zako ufikie lodge ufante yako usepe
Haya mambo yamepungua sana siku hizi, baada ya simu kuja hivyo mtu anafanya mawasiliano kujuliana hali.
Hospital za Rufaa Kanda nazo zimesaidia watu kutorundikana kwa watu

Shule kila sehemu zimesaidia watu kutoenda kwa watu
 
Nyumba zina utaratibu na nyingine ni vituko kwenda mbele mpaka dhambi, niliwahi kutembelea familia moja, nilichoona sikukipenda kabisa, wakati wa kula wote tulikaa mezani lakini msichana wa kazi anakaa jikoni na kula huko na kibaya zaidi kama Kuna kitu kimekosekana anaitwa akilete, I didn't like it na baadaye wakati na mwenyeji wangu peke yetu I confronted him na nilimsema bila kujali, aliahidi kubadili ule utaratibu
 
Back
Top Bottom