Nipunguze nini kwenye gari yangu ibaki na uzito wa kg 600? Hadi hapa nimeshanyofoa spea tairi!

Nipunguze nini kwenye gari yangu ibaki na uzito wa kg 600? Hadi hapa nimeshanyofoa spea tairi!

Toa upepo kwenye magurudumu yote, ng'oa side mirror zote, kisha pima uzito! Kama bado rudi utuambie bado ngapi
 
Ndugu mleta mada nimepitia uzi wako kwa makini na nimeelewa vizuri shida ulio nayo

Katika gari yoyote ile kitu kinachoongeza uzito kwa kiasi kikubwa kuliko vyote ni injini, hivyo tafuta fundi mwenye uzoefu na ufunguaji wa injini atoe injini yote kwenye gari.

Hapo Utakua umepunguza zaidi ya kilo 500 kwenye gari lako na tatizo lako litakua limeisha

Kila rakheri

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ondoa interior body panels, ondoa AC, dashboard, ondoa sound proofing materials zote kwenye hood.

Then badilisha vioo weka vya kevlar, weka carbon fibre hood, bumpers, Then weka light weight racing wheels.

Ondoa seat zote bakiza ya dereva tu.

Sent using Mikoyan MiG-29
 
kuNa mambo mengine tuwe serious mtu akitaka msaada tumpe majibu mazuri......by the way Mimi ni fundi mzoefu wa magari hilo tatizo lako ni dogo wewe nenda kwa fund wa magari mwambie atoe mfumo wote wa break alafu washa gari yako nenda mpaka speed 120 alafu uta nipa mrejesho kama tutaonana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utapiamlo hauwakumbi watoto tu kuba utapiamlo wa akili pia hasa kwa watu wazima.
 
Wadau, kama kichwa cha habari kinavyojieleza. Ninajitahidi kupunguza uzito wa gari yangu toka 960kg angalau ifike 600kg!

Nia na madhumuni ya kutaka kupunguza uzito, kwanza ni kuiwezesha gari iwe nyepesi ili niweze kuendelea kuruka kwenye matuta kwa urahisi.
Pili, ni kupunguza kiwango cha wese ambacho gari inakula.

Ninapofika kwenye matuta, huwa sipendi jinsi gari inavyodunda, sasa kuhakikisha hilo nimeshaanza na kung’ofoa spare tairi kitu ambacho kimeniwezesha niweze kupunguza uzito, kwa takribani 30kg.

Sasa baada ya hapa sioni tena kitu kingine cha kung’ofoa. Sijui ning’ofoe difu!, makochi ya nyuma au?

Embu manaofahamu magari naombeni ushauri wenu. Nitazitoa wapi hizi kg mia tatu ili gari ibaki na uzito wa kg 600?

Dah! Jinga mwezangu, wewe huna shule ya kukuelimisha duniani. Tukutane ahera. Mimi natangulia.
 
Nilidhani waliotoroka Milembe wote walikamatwaga kumbe wengine bado wako humu wanakoment
 
Back
Top Bottom