Nisaidieni, Akili yangu ipo kama imefungwa

jakaeama

Member
Joined
Jul 12, 2013
Posts
23
Reaction score
2
Ni kuhusu masomo yangu!
Nimejawa na hofu inayonifanya niishi bila raha yaani natetemeka kila wakati,moyo unauma na wakati mwingine nashindwa kupumua vizuri!
Hofu yenyewe inanifanya ninachokisoma sikielewi yani nashika daftari tu huku naliangalia,mawazo mengi ya kufeli huko mbeleni yanakuja kila siku!
Naamua niondokane na hali hii lakini nimeshindwa kujibadilisha!
Ninapowaona wengine wanasoma lakini mimi ndo mawazo yakufeli yanavyothibitika
Nahitaji ushauri! Wenu
Kama kunamtu anayemjua mtaalamu wa saikolojia anisaidie nimpate maana akili yangu imekua kama "vile imefungwa na haitaki kutoka katika kifungo hicho"
Msaada na ushauri wenu unahitajika!
 
Upo kidato cha ngap? then unasoma bording au day school sema na jinsia yako na wapi ulipo wat wakusaidie
 

Pole sana. Kama unaamini tafuta mtumishi wa Mungu akufanyie maombi. Si kawaida hiyo. Shetani yuko kazini. Fanya haraka sana.
 
Pole sana dogo...

Inasikitisha sana, mtu anakuja mahali ambapo at the back of his mind anajua atapata msaada, lkn anaambulia fedheha na kejeli. Kwanini tunakosa utu, hata kama huna msaada, try to feel you're wearing his boots...

Madani, dogo hiyo hali ni kawaida, tena kawaida sana hasa pale unapohisi upo nyuma ya menzako, unaona wenzio wanajua vingi wakati wewe hata vichache huna. Ni kawada sana dogo just feel normal.

Hii hali ilinikuta nikiwa level kama yako, nakumbuka siku ya kwanza naingia darasani nakuta kila mtu anasoma, tena intensively. Nikashtuka sana, nikajiuliza sana, hawa jamaa wanasoma nini??? Kila nikijaribu kusoma najihisi very inferior, mbaya zaidi akatokea jamaa m1 akaenda mbele akaanza kuvunja pindi na kugonga maswali ya review. Nikipomuuliza jirani yangu pembeni, kama walishawahi kufundishwa?? Alinishangaa sana, akaniuliza, wewe tangu umalize o'levo ulikua unafanya nini?? Wenzio tumeshapiga mapindi, wengine hata syllabus tushacover... hii ilinishtua sana, kila nilipojaribu kusoma msuli haukupanda, nikajihisi sistahili kusoma any more, roho ya kufail ikanijaa, nilikosa amani + nguvu, ulikua ni wakati mgumu sana, nilihisi sitasaidika...At last, my fortune was out of the blue, would you trust me,X marked the spot, more higher even over the top frontrunners...

Kijana, niPM. Nitakusaidia kadri ya uwezo wangu. Hope kila kitu kitakaa sawa.
 
ONTARIO msaidie kijana ,mimi mwenyewe nimeguswa jinsi yeye anavopata wakati mgumu

 
Last edited by a moderator:
Hiyo ni dalili ya msongo wa mawazo yaani depression. Kama uko dar jaribu kuwana wataalam wa afya ya akili pale muhimbili
 
PCM mkuu!

I expected this.Tatizo la madarasa ya PCM ni kwamba kuna watu huwa wanapenda sifa,wanapenda waonekane wao wapo fiti na wamecover vitu vingi ila mwisho wa siku matokeo ya necta ndio jibu.

Binafsi ilinikuta na ilikuwa moja ya sababu ya mimi kutoenda shule ya serikali niliyochaguliwa baada ya kumaliza olevel,maana wenzangu tuliochaguliwa wote walikuwa wanakata mapindi na nikikutana nao wananitisha tu ila mwisho wa siku wote tulikutana UDSM kozi moja

Wasikutishe ndugu,wao wametangulia tu kwa mbwembwe lakini wewe una miaka miwili mbele ambayo inatosha kabisa kukufanya uwe fiti tena zaidi yao,jiwekee ratiba yako,Ingia darasani msikilize mwalimu na fuata ratiba yako ya kujisomea,usiwafuate wao.Chukulia hiyo kama fulsa ya wewe kuwa na watu waliokutangulia hivyo watumie pale utakapo kwama.
 
Kuna watu humu ndani mna roho mbaya jamani mtu kuomba ushauri ni kejeli na kashfa
Mmh. .matatizo ni kwa kila mtu dogo pole sana
Mwombe Mungu
Fanya discussion na wenzio
Relax unapoona umechoka
 
Mdowangu usipanic, mi najua watu wanaokupa stress ni hao waliokava topics! Sasa wewe usitake kusoma kwa kushindana nao, wewe nenda taratibu, unaweza ukawatumia wakupush kidogo!! Pia kipindi cha likizo jitahid kusoma tuition usitegemee walimu kila kitu. Siri ya pcm ni kukava mapema na mazoezi ya kila siku.
Halafi acha nikupe siri nyingine, kama hukupata msingi mzuri kwenye baadhi ya maeneo kwenye pcm o'level, jitahid upate mtu akuelekeze vizuri usione aibu, manake adv.level hasa sayansi masomo yake yanahitaji msingi mzuri wa o'levl.

Pcm bila stress inawezekana.

Ni pm for financial assistance if you don mind.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…