nisaidieni jaman kuhusu hii mimba

nisaidieni jaman kuhusu hii mimba

asante watu8 nilikuwa natafuta ilo neno ss halikunijia kwa wakati ikabidi nipachike hilo
 
Last edited by a moderator:
Pole sana ila hakuna sababu ya kuanza kusikitika kabla ya kujua nini kinachoendelea katika ujauzito wenu. Cha muhimu kama nilivyokushauri mapema leo ni kuwaona wataalamu bila kuchelewa. Kama hutajali tufahamishe madaktari wanasemaje kuhusu kiumbe mtarajiwa. Kila la heri.

Asante ndugu kwa ushauri sijui kwa nn karudi yasinge nitokea haya jamani furaha yote ya ujio wa mume wangu imeniisha kwa kweli.
 
Asante Mungu,asante jf nimekwenda hospital nimepiga utra sound mimba haijatoka.nimepewa dawa na kuelezwa cha kufanya.Asanten kwa kunitia moyo.Mungu awabariki ila wanasema ukipata tatizo kama hilo unachotakiwa kuwahi hospital.
 
hongera my dia
pole sana kwa hali iyokupata usiku
Asante Mungu,asante jf
nimekwenda hospital nimepiga utra sound mimba haijatoka.nimepewa dawa na
kuelezwa cha kufanya.Asanten kwa kunitia moyo.Mungu awabariki ila
wanasema ukipata tatizo kama hilo unachotakiwa kuwahi hospital.
 
19 Sept Ulitueleza kuwa mimba yako ni ya mwezi mmoja unusu, na hapa waeleza kuwa tar 6 Oct utatimiza miezi mitatu...
Mbona kama unatuzingua akili zetu we mwanamke? Tokea tar 19 hadi hiyo tar 6 huo muda hata ujumlishe vipi hauwezi tengeneza mwezi mmoja unusu ili kufanya ujauzito wako uwe wa miezi mitatu.

Anyway, mjamzito kutokwa damu si jambo la kawaida na yakupasa ufike hospitali mapema kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Kuna sababu kadhaa ambazo huweza kupelekea mama mjamzito kutokwa na damu nyepesi 'spotting'.

1. Ngono 'Sex'
Wakati wa ujauzito damu nyingi huwa inakimbilia kuelekea shingo ya kizazi 'cervix'. Hivyo hupelekea ukuaji usio wa kawaida wa 'cervix' na hii kuna uwezekano ikasabisha damu ndogo kutoka wakati wa kungonoka.

2. Miscarriage au Ectopic Pregnancy
Kama kutokwa huko kwa damu kuliambatana na hali yoyote ya maumivu ya tumbo 'maumivu kama yale ya MP'...basi kuna uwezekano mimba ikawa imeharibika au mimba imetungwa nje ya mji wa mimba.
Karibia robo ya wanawake wajawazito hutokewa na hii hali na nusu ya wanawake hawa huishia kuwa na 'miscarriage'.

3. Infections
Wakati mwingine kutokwa na damu nyepesi ambayo haihusiani na hali ya ujauzito husababishwa na vaginal infections mathalani 'yeast infection', 'bacterial vaginosis' au hata magonjwa mengine ya zinaa 'STD's'.
Maambukizi haya hupelekea kuvimba au kuwa na hali ya uwasho kwa shingo ya uzazi, na kama mama mjamzito atafanya ngono kuna uwezekano wa kutokwa na damu nyepesi.

Ushauri;
Nenda hospitali wakufanyie vipimo kadha wa kadha ili kutambua ni nini haswa chanzo cha hali hiyo.
tehe..tehe... uko juu na kazi yako unakumbuka hata tarehe? kiukweli jamii forum ni zaidi ya familia zetu wapo watu wanaweza kujitoa kwa shida za wengine kutoka rohoni mwao gooood!
 
Kwenda hosp ni lazima na muhimu sana. Ukiwa mjamzito hata ukioma tone tu la damu si dalili nzuri. Hata kama itakua haojatoka kuna uwezekano unahitaji ushauri wa ki Dr. how uende nayo hali yako. Pole sn anyway.
 
Asante Mungu,asante jf nimekwenda hospital nimepiga utra sound mimba haijatoka.nimepewa dawa na kuelezwa cha kufanya.Asanten kwa kunitia moyo.Mungu awabariki ila wanasema ukipata tatizo kama hilo unachotakiwa kuwahi hospital.

Zingatia hayo uliyoelezwa huko...
 
Mama kaa bedrest. Kma unataka mtoto pumzika kusex. Nayenyewe ni kaz hyo.
 
Asante ndugu kwa ushauri.jamani kama nimekosea cku nisamehe kuchanganyikiwa huku kama nilisema mwezi 1 na nusu nilikosea ilikuwa miwili na nusu kwenda mitatu.sina mama jaman ndo mana kila kitu nakimbilia humu,asante.

Umenigusa sana, Mwenyezi Mungu akusaidie kunusuru mimba yako
 
Back
Top Bottom