sindani,
Pole kwa tatizo lako,
Tatizo la vivimbe/uvimbe huwapata wanawake katika rika mbalimbali, hata hivyo uvimbe/vivimbe hivi hutegemeana na aina yake mfano, vivimbe vyenye majimaji, vivimbe vigumu, saratani n.k Hata hivyo vyote hivi husababisha maumivu ya tumbo/kiuno, n.k Dalili nyingine ni pamoja na kukosa siku (kwa usahihi), maumivu makali sana wakati wa hedhi, kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi n.k
Sasa kwa kutegemea vipimo mbali mbalimbali mfano picha za sauti (Ultrasound Sonograghy) inaweza kubaibisha shida hasa ni nini, vile vile Upimwaji wa vichochezi (Hormones), hutofautisha chanzo cha tatizo, n.k
Matibabu hasa hutegemeana na chanzo cha tatizo ni nini, dawa nyingine mfano dawa za maumivu, ushauri, n.k husaidia.
Sasa, kulingana na maelezo yako hapo juu (ingawa si Toshelezi), kuna umuhimu wa kutumia dawa za maumivu, lakini ni vyema ukaonana na daktari kwanza! Pili endelea kuangalia mabadiliko ya mwili mfano, mzunguko wa siku zako, wingi/uchache wa damu wakati wa mzunguko, maumivu mf. ya tumbo, maziwa, n.k.
Mwisho, jaribu kutumia lugha inayoeleweka sidhani kama kuna haja ya kufupisha neno lililo fupi tayari, si watumiaji wa jukwaa wote ni vijana/ufahamu sawa na wewe..Wakati fulani lugha/maandishi mengine yanachefua (mf. Cjua, xaxa, n, yan, n.k) haya na mengine mengi yanakatisha tamaa kusoma maelezo hadi mwisho kutokana na aina ya uandishi.(I stand to be corrected).
Nakutakia Afya njema.