Nisaidieni kupaza hii sauti iwafikie Wakuu wa Nchi, Sakata la bodaboda Dodoma ni zaidi ya mateso kwa vijana wetu

Nisaidieni kupaza hii sauti iwafikie Wakuu wa Nchi, Sakata la bodaboda Dodoma ni zaidi ya mateso kwa vijana wetu

Bodaboda ni janga la taifa, huwa napata taabu sana kuwatetea hasa kwenye makosa yanayohusu sheria za barabarani. LATRA inabidi waweke sheria kali sana za udhibiti wa Bodaboda ama sivyo tutavuna mabua.
 
Habari wakuu, Naandika huu ujumbe kwa maumivu makali sana, kilio simanzi na maumivu yasiyoelezeka,
Nilishawahi kuleta mada hii hapa jukwaani bahati mbaya sana haikupata wadau wengi, haikupata wachangiaji na mwisho wa siku uzi wangu ulifunikwa na nyuzi za vichekesho, vibonzo na stori za kuchekesha hii inaonesha ni kiasi gani Watanzania tusivyochukulia sereous mambo mhimu.

Leo naandika hapa nikiamini hapa jukwaani wapo viongozi mbalimbali au watu mbalimbali ambao wanaweza kuucopy huu ujumbe wangu kisha kumtumia waziri mwenye dhamana ya kulitatua hili au kwa mkuu wa Polisi Tanzania, au hata kuniwekea hapa namba ambayo anapatikana whatsup au email ili nimtumie mimi mwenyewe kero hii pengine hapo anaweza kuitatua.

Ninaamini nchi yangu na viongozi wetu hawana lengo baya kwa vijana na wanainchi wake ila kuna baadhi ya watu wanafanya haya kwa masrahi yao binafsi na chuki zao binafsi kutufanya vijana tuichukie serikali na kuona kama tunaserikali kandamizi na isiyo na huruma kwa wanainchi wake.

Mara nyingi nilishaleta malalamiko ya Polisi Kituo kikuu Dodoma (Dodoma centro police) kuwatesa na kuwanyanyasa madereva bodaboda na hata kuwapiga vijana makofi kwa makosa yasiyokuwa na sababu, na ikiwa bodaboda anakamatwa kwa kosa la trafic case kuna haja gani ya kumpiga kumdhalilisha na hata kutumia lugha za kashfa na matusi kwa kijana ambae anatafta riziki?

Kumekuwa na tabia ya Polisi kukamata bodaboda na kumtaftia makosa mengi kisha kumtoza shilingi elfu kumi kwa kila kosa 10,000/=, hapa utakuta Bodaboda amejumlishiwa makosa 10 na anatakiwa kulipa laki moja,

Sasa hapo kijana wawatu anadaiwa rejesho na boss pikipiki ya mkataba kila siku rejesho, na ikikamatwa kama hana hela hapo pikipiki inaenda kupakiwa kituoni na hapo kijana wawatu haingizi chochote na pikipiki inasoma rejesho zikipita siku5 maboss wanachukua pikipiki yao hapo kijana wawatu kala hasara maana pikipiki za mikataba huwa kuna kiasi wanatanguliza ko ikichukulia hapo kijana kala hasara.

Maana kwa sasa Kituo cha police Dodoma wanategemea mapato kutoka kwa bodaboda, vijana ambao kwa changamoto za kazi zao hata shilingi elfu 10 kwa siku wanaingiza kwa mbinde.

Nizaidieni kusambaza huu ujumbe huu.
Wewe bodaboda wa Dodoma mjini halafu huielewi ofisi ya waziri wa mambo ya ndani hapo Dodoma?

Anza kupeleka malalamiko yako kwa mkuu wa wilaya yako, kama hujasikilizwa nenda kwa mkuu wa mkoa, kama hujasikilizwa nenda kwa waziri.

Au nenda moja kwa moja kwa waziri, usipeleke malalamiko ya mdomo tu kote unakopita, peleka kwa barua pia/ Na uwe na kopi iliyosainiwa na anaeipokea.

Ajabu hii.
 
Wewe bodaboda wa Dodoma mjini halafu huielewi ofisi ya waziri wa mambo ya ndani hapo Dodoma?

Anza kupeleka malalamiko yako kwa mkuu wa wilaya yako, kama hujasikilizwa nenda kwa mkuu wa mkoa, kama hujasikilizwa nenda kwa waziri.

Au nenda moja kwa moja kwa waziri, usipeleke malalamiko ya mdomo tu kote unakopita, peleka kwa barua pia/ Na uwe na kopi iliyosainiwa na anaeipokea.

Ajabu hii.
Ajabu ipi? Inatakiwa muelekeze hivi mimi kutokutambua kama ilipaswa niandikie mkuu wa wilaya barua sikulitambua lakin pia nje ya kulitambua bado napata mazingira magum namna ya kumfikia na kumkabidhi barua yake
 
Wewe bodaboda wa Dodoma mjini halafu huielewi ofisi ya waziri wa mambo ya ndani hapo Dodoma?

Anza kupeleka malalamiko yako kwa mkuu wa wilaya yako, kama hujasikilizwa nenda kwa mkuu wa mkoa, kama hujasikilizwa nenda kwa waziri.

Au nenda moja kwa moja kwa waziri, usipeleke malalamiko ya mdomo tu kote unakopita, peleka kwa barua pia/ Na uwe na kopi iliyosainiwa na anaeipokea.

Ajabu hii.
Hiyo kopi inasainiwa na nani na barua inapita wapi na wapi hebu nifafanulie niandike maana ni zaidi ya mateso kwa vijana mimi sio bodaboda japokuwa mara nyingi ninatumia usafiri wa pikipiki kwa shughuli zangu na hizi adha wenyeji wa dodoma mjini wote hasa wafanyabiashara na wakazi wa majengo wanaijua vzuri sana,mimi hapa nimejitolea kuwapazia sauti kwa kuwa bodaboda ni maisha niliwahi kupitia hata kabla sijawa katika maisha niliyonayo sasa
 
Ajabu ipi? Inatakiwa muelekeze hivi mimi kutokutambua kama ilipaswa niandikie mkuu wa wilaya barua sikulitambua lakin pia nje ya kulitambua bado napata mazingira magum namna ya kumfikia na kumkabidhi barua yake
Pole sana.

Haya anzia kama nilivyokuelekeza. Utaleta mrejesho ulipofikia.
 
Hili kweli liangaliwe polisi Dodoma mjini wanakela sana
Hili la polisi ni Tanzania nzima watu wanalalamika. Ndiyo maana kwengine wanjichukulia sheria mkononi kuwatandika na kuwachomea vituo.


Jeshi la polisi linatakiwa lifanyiwe mabadiliko makubwa sana.
 
Hawa jamaa acha tu, ...hapohapo police central Dodoma wana mradi wao mpya huu uko hivi, usiku wakiwa patrol hasa siku zinapochezwa game UEFA champions league zile za late night wanakwenda na karandinga lao maeneo ya mabanda wanakoonesha mpira (hasa mailimbili kwa mudy na chang'ombe) wanalitegesha karandinga mlangoni halafu wanashuka na kuingia ndani ya banda inapigwa ambush wote mnaingia ndani ya karandinga then mnapelekwa central na kuandikiwa makosa ya uzururaji, hapo inabidi muanze taratibu za kutoka kila mtu kivyake, hapo ndipo maokoto yanapoanza na si chini 40k
Wanakera sana asee
 
Back
Top Bottom