Nisaidieni, mwanangu anaumwa!

Gagurito

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2011
Posts
5,600
Reaction score
806
Siku 5 zimepita sasa alikuwa anasumbuliwa na mafua na kikohozi kidogo. leo katapika tukampeleka hospital, huko kapimwa kaoneka na malaria, pia aliongezwa drip ya maji.

Tupo nyumbani bado hajatulia kama kawaida, tatizo hataki kula na ananyonya kidogo. Akilala anajinyonga nyonga, hatulii. Anaumri wa mwaka na miezi 3 sasa, ni binti. Je hapa tatizo ni nini? Nini tiba yake? Ushauri please.
 
Kwanza pole sana na Mungu amjalie mtoto wako apone haraka.

Mie nakushauri umpeleke kwa daktari wa watoto haraka sana hili akafanyiwe uchunguzi zaidi na kupewa dawa.

Umri huo ni vigumu sana kutoa ushauri wa juu juu.

Kila la kheri.
 
Nakushaur rud h'tal waangalie na vipimo vingine kama u.t.i inasumbua sana watoto ukiona bad tafuta mama mtu mzima anayejua dawa za watoto yawezekana ukawa mchango au ukaptula
 
Nenda kwa dokta wa watoto
 
Asanteni, kama nilivyosema, hana joto ila ni mnyonge na kila akijalibu kula anatapika.
 
Pole sana. Kama walivyoshauri wengine, mpeleke kwa kwa dokta wa watoto. Kwa kuongezea, usikose kumwambia dokta kuhusu matibabu aliyopata na alipata lini. Ni vizuri ikiwa utaonyesha vyeti vyake kama unavyo, ili kuthibitisha unachosema. Kwa matibabu ya mtoto, mimi niko tayari kuonekana mjinga ili nisifanye kosa isije ikanigharimu. Afya ya mtoto naiweka mbele.

Usisahau kumwomba Mungu kwa ajili ya afya ya binti yako (ninaamini hivyo). Kila la heri mkuu.
 
Pole sana. Mmerudi hospitali? Manake usifanye uzembe.
 
Pole sana. Mmerudi hospitali? Manake usifanye uzembe.

Haya yote yametokea jana na usiku wa jana mchana (kuamkia leo) aliwekewa drip hospital leo ndio tutarudi.
 

Asante kwa ushauri mkuu. Naufanyia kazi.
 
Mpeleke pale Kinondoni B dispensary, omba kumuona dr. Anton ni mzuri sana kwa watoto hope atapata nafuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…