SoC03 NISHATI MIX-Mashine ya kuzalisha umeme pamoja na gesi kwa kutumia Plastiki na Uchafu unaooza

SoC03 NISHATI MIX-Mashine ya kuzalisha umeme pamoja na gesi kwa kutumia Plastiki na Uchafu unaooza

Stories of Change - 2023 Competition
Sawa Ila kama umelenga mtu
Mmoja mmoja, kunahitaji jitihada za zaidi kuwa persuade kutokana na attitudes zetu.

Sijui Km ni wazo la kitoto Ila Ningependa kuona investor mkubwa kama serikali inunue machine zako na kuzisambaza , uingie contract ya kutengenezea Ama kuiuzia serikali lol.
Kweli kabisa ,kubadilisha attitudes za watu ni kazi moja kubwa zaidi kuelekea commercialization..Nawakaribisha investors pia kwa ajili ya scale up ya mradi.
 
Unaweza ipata kwenye page zetu mtandaoni ,au kwenye page ya ITV utaikuta (nishatimix)
Pia napenda kujua specifications za power output ya mashine yake. Inatoa kw ngapi za umeme au gas kiasi gani kwa dakika au saa?
 
Pia napenda kujua specifications za power output ya mashine yake. Inatoa kw ngapi za umeme au gas kiasi gani kwa dakika au saa?
Kuna models tatu...nishati plus(5kW) ,nishati mix (3kW )na nishati min (1kW)...specifically with varying engines .
 
Iyo mashine unayo ni yako au ni wazo?
Kama ni yako kaa ukijua siku ukishinda kwa kudanganya watu JF watakwambia uthibitishe kwa kuja au kuwapeleka eneo ilipo iyo mashine utawapeleka??

Kama ni wazo..Sio wazo geni hii ni BIOGAS ambayo hata mshana aliandika uzi wake kwenye shindano la 2021 ambapo hata top 20 uzi haukuingia

Ujaeleza inatumia nguvu gani kujiesha..

Umeelezea faida..Hasara Zake JE

Usituchoshe sawa?

Aisee
Utauuwa, inatosha, mwache

Nimewahi kufanya internship kwenye kiwanda kikubwa kinachozalisha umeme kwa kutumia takataka.
Kiwanda kilikuwa kikubwa ambacho malori ya uchafu yanapishana

Sasa kwa umbo la hiyo machine, kuweza kutoa nishati zote hizo pamoja na mabaki mbadala kama matofali ya mkaa, hata mabeberu wenye elimu yao tunayoisoma hawajafikia huko
Hatujaona ni wapi anaeleza ni nishati gani inatumika kubadilisha hizo takataka kuwa nishati mbabadala
Je ni umeme, au ni nini kinaendesha huo mtamba wake utakao weza kufikia au kupita 500 degree celcius mpaka kufanya mchakato wa pyrolysis utokee ?
Tunahitaji aje atupe jibu?
Na atuambie efficient yake tujue kama ina faida ya anachokisema

1687472794785.png
 
Aisee
Utauuwa, inatosha, mwache

Nimewahi kufanya internship kwenye kiwanda kikubwa kinachozalisha umeme kwa kutumia takataka.
Kiwanda kilikuwa kikubwa ambacho malori ya uchafu yanapishana

Sasa kwa umbo la hiyo machine, kuweza kutoa nishati zote hizo pamoja na mabaki mbadala kama matofali ya mkaa, hata mabeberu wenye elimu yao tunayoisoma hawajafikia huko
Hatujaona ni wapi anaeleza ni nishati gani inatumika kubadilisha hizo takataka kuwa nishati mbabadala
Je ni umeme, au ni nini kinaendesha huo mtamba wake utakao weza kufikia au kupita 500 degree celcius mpaka kufanya mchakato wa pyrolysis utokee ?
Tunahitaji aje atupe jibu?
Na atuambie efficient yake tujue kama ina faida ya anachokisema

View attachment 2665860
Asante kwa Maoni Yako Mr..
Naomba nianze kwa kukwambia kuwa hii ni new innovation na ipo kwenye stage ya testing ,hatufanyi kitu chenye kishafanywa na mtu na sisi tuna hatimiliki ya hii innovation ,na actually kinachokupa wasiwasi ndo power ya innovation hii kwasababu ni kitu kipya kwako na jamii kwa ujumla..
Pili kuhusu heat source ,Kuna employed system ya induction together with Biochars action kutokana na raw materials(blocks) ambazo hutoa steam to foster heating.
Kuhusu efficiency kwenye last update kwenye testing sites ,ipo 83%efficient ambayo tunategemea baada ya testing, last modifications itakuwa more efficient .
Lastly mradi huu umeanza 2020, prototype ya kwanza 2021 na upo chini ya uangalizi wa na ukaguzi wa chuo kikuu UDSM ...kama utakuwa na worries zaidi unaweza pitia social media zetu au fika katika banda la UDSM kwenye 47th DIFT (Sabasaba ) exhibition yanayoanza tarehe 28.
Karibu sana kwa Maoni zaidi !!
 

NISHATI MIX-Mashine ya kuzalisha umeme Pamoja na Gesi Kwa kutumia Plastiki na Uchafu unaooza
(Imeandikwa na L.Buberwa)

View attachment 2650421
UTANGULIZI

Taka
kwenye mazingira ni tatizo kubwa linaloikabili Dunia Hii leo. Kuna aina mbalimbali za uchafu au taka zilizopo kwenye mandhari yetu kama, taka za plasitiki, taka za kikaboni(organic wastes), taka za elektroniki, taka za kioevu(sewage) na nyinginezo. Taka za Plastiki Pamoja na taka za kikaboni ndizo zilizopo kwa kiasi kikubwa kwenye mazingira yetu yanayotuzunguka.
Hata hivyo, matumizi makubwa ya plastiki yameleta madhara makubwa kwa mazingira yetu. Plastiki inachukua muda mrefu kuoza, na kusababisha uchafuzi wa mazingira kwa njia mbalimbali, ikiwa ni pamoja na; Uzalishaji wa gesi chafu, Uchafuzi wa maji, Uharibifu wa mazingira ya ardhini, athari kwa viumbe hai na Uchafuzi wa hewa; kwa kutoa kemikali hatari na sumu ambazo zinachangia uchafuzi wa hewa na matatizo ya afya kwa binadamu pale zinapochomwa.

Kutokana na taka za Plastiki na uchafu unaooza kuwa changamoto kubwa inayoikabili Tanzania, Africa na Dunia kwa ujumla; kupitia Makala hii nimeelezea jinsi nilivyoweza kuchanganya Ubunifu na Teknolojia, kupata suluhisho la kipekee kwa uchafu na nishati kwa ujumla kwa kubuni na kutengeneza kifaa au mashine inayoitwa NISHATI-MIX.

MASHINE YA NISHATI-MIX
NISHATI-MIX
ni mashine inayozalisha umeme pamoja na gesi ya kupikia kwa kutumia plastiki na uchafu unaooza. Mashine hii ya kuvutia inatoa suluhisho la ubunifu kwa matatizo mawili: uchafuzi wa mazingira na upungufu wa nishati, ambayo ni matatizo yanayoikabili jamii ya watanzania ,waliopo mijini pamoja na vijijini kwa ujumla.

TEKNOLOJIA NA MUUNDO WA NISHATI-MIX

Nishati-Mix ni mashine iliyoundwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa na michakato miwili inayosaidia kubadilisha taka za plastiki na uchafu unaooza kuwa vyanzo vya nishati mbadala. Michakato hiyo huitwa "pyrolysis,” Pamoja na ‘’gasification’’ambapo taka huchomwa bila oksijeni,na kuchakatwa na hatimaye kuzalisha mafuta mazito(liquid fuel) Pamoja na gesi. Kifaa hicho kina sehemu kadhaa muhimu:
  • Mfumo wa Kuchoma: Taka za plastiki na uchafu unaooza huingizwa kwenye mfumo wa kuchoma. Hapa, joto kali hutumika kuchoma taka hizo bila kuwepo kwa hewa.
  • Mfumo wa Pyrolysis:Taka zilizochomwa huingia kwenye mfumo wa pyrolysis ambapo mafuta mazito na gesi hutokea. Mafuta mazito yanaweza kutumiwa kama nishati mbadala kwa ajili ya kuzalisha umeme au kwa ajili ya matumizi ya viwandani. Gesi inayozalishwa inaweza kutumiwa kwa kupikia, kuendesha mtambo, au hata kuzalisha umeme.
  • Mfumo wa kutengeneza gesi (gasification);Mfumo huu umeungana na mfumo wa pairolisisi Taka za kikaboni (zinazooza) baada ya kuchakatwa huingia kwenye mfumo huu na husaidia uzalishwaji wa gesi na uhifadhi wa gesi kwa ajili ya matumizi mbalimbali.
  • Mfumo wa Uchujaji:Mfumo huu hutumiwa kuondoa uchafu wowote uliobaki kutoka kwenye mafuta mazito na gesi ili kuhakikisha kuwa nishati inayozalishwa ni safi na salama kwa matumizi,na kuhakikisha hakuna uchafuzi wowote kutoka kwenye mashine.
  • Mfumo wa umeme: mfumo huu umeundwa na sehemu ya injini ,ambayo huweza kutumika kuzalisha nishati ya umeme .

View attachment 2650426
Kielelezo namba 1: muundo wa nishati-mix
View attachment 2650431
Kielelezo namba 2:muonekano wa NISHATI-MIX

MALIGHAFI ZINAZOTUMIKA.

NISHATI MIX hutumia malighafi taka, ambazo ni plastiki Pamoja na taka zinazooza pekee katika kuzalisha umeme na gesi.
Taka hizi zikusanywa, zinaandaliwa na kusagwa na pia kuunganishwa kutengeneza vipande vidogo vidogo (blocks) kwa kilo, vyenye uzito mbalimbali .Vipande hivi ndivyo huingizwa kwenye mashine kwa ajili ya kuzalisha nishati ya umeme pamoja na gesi.

View attachment 2650427
Kielelezo namba 3: malighafi taka katika vipande

UMUHIMU WA NISHATI-MIX

Nishati-Mix ina umuhimu mkubwa katika jamii yetu kwa sababu zifuatazo:

  • Kupunguza Uchafuzi wa Mazingira: Kwa kutumia Nishati-Mix, taka za plastiki na uchafu unaooza ambao ungekuwa chanzo cha uchafuzi wa mazingira sasa unageuzwa kuwa vyanzo vya nishati safi. Hii inapunguza kiwango cha taka zinazoelekezwa kwenye dampo la taka na kusaidia kulinda mazingira yetu.
  • Kuongeza Upatikanaji wa Nishati: Nishati-Mix ina uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha kuendesha shughuli mbalimbali pamoja na gesi, vyanzo viwili muhimu vya nishati. Kwa kuwa inatumia taka za plastiki na uchafu unaooza, kuna chanzo cha nishati kinachopatikana karibu na maeneo mengi. Hii inaleta faida kubwa kwa maeneo yasiyo na upatikanaji wa nishati ya kawaida.
  • Kupunguza Utegemezi wa Nishati ya Mizani: Nishati-Mix inachangia kupunguza utegemezi wa jamii kwa vyanzo vya nishati ya mizani kama mafuta ya petroli na gesi asilia. Hii inasaidia kupunguza gharama za nishati na kuongeza uhuru wa nishati kwa jamii.
  • Kuboresha Maisha ya Jamii: Kwa kuzalisha umeme na gesi, Nishati-Mix inatoa fursa za kuboresha maisha ya watu. Umeme unahitajika kwa ajili ya taa, kupasha joto, na kuendesha vifaa vya umeme, wakati gesi inaweza kutumika kwa kupikia. Hii inasaidia kuongeza ufanisi na kuboresha maisha ya watu.


HITIMISHO
Nishati-Mix
ni hatua muhimu kuelekea maendeleo endelevu na matumizi bora ya rasilimali zetu za asili na ni wazo zuri kutumia mashine kama NISHATI-MIX, ambayo inaonyesha uwajibikaji na nia ya kudumisha utawala bora kwa njia mbili: kwanza, kwa kuchangia katika kupunguza uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na plastiki na taka nyingine; na pili, kwa kutoa nishati mbadala ambayo inaweza kuwa na athari nzuri kwa jamii.

Kwa kutumia vifaa kama NISHATI-MIX unaweza kuchangia katika jitihada za kupunguza matumizi ya vyanzo vya nishati ya kisasa ambayo inaweza kusababisha uchafuzi wa mazingira na mabadiliko ya hali ya hewa. Kwa kugeuza plastiki na uchafu wa mazingira kuwa nishati mbadala, unaweza kupunguza athari za uchafuzi wa mazingira na kuchangia katika kuhifadhi rasilimali za asili.

Mashine hii haijaingia sokoni, lakini ipo kwenye hatua za mwisho za majaribio katika sehemu mbalimbali ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Hivyo basi kupitia Makala hii naendelea kuhamasisha na kuomba ushirikiano katika kupigana na changamoto za plastiki na uchafu kwenye mazingira kwa ujumla, na Pia kuomba taasisi na mashirika mbalimbali kuunga mkono bunifu ambazo zinalenga maendeleo ya nchi yetu ya Tanzania katika nyanja mbalimbali.
 

NISHATI MIX-Mashine ya kuzalisha umeme Pamoja na Gesi Kwa kutumia Plastiki na Uchafu unaooza
(Imeandikwa na L.Buberwa)

View attachment 2650421
UTANGULIZI

Taka
kwenye mazingira ni tatizo kubwa linaloikabili Dunia Hii leo. Kuna aina mbalimbali za uchafu au taka zilizopo kwenye mandhari yetu kama, taka za plasitiki, taka za kikaboni(organic wastes), taka za elektroniki, taka za kioevu(sewage) na nyinginezo. Taka za Plastiki Pamoja na taka za kikaboni ndizo zilizopo kwa kiasi kikubwa kwenye mazingira yetu yanayotuzunguka.
Hata hivyo, matumizi makubwa ya plastiki yameleta madhara makubwa kwa mazingira yetu. Plastiki inachukua muda mrefu kuoza, na kusababisha uchafuzi wa mazingira kwa njia mbalimbali, ikiwa ni pamoja na; Uzalishaji wa gesi chafu, Uchafuzi wa maji, Uharibifu wa mazingira ya ardhini, athari kwa viumbe hai na Uchafuzi wa hewa; kwa kutoa kemikali hatari na sumu ambazo zinachangia uchafuzi wa hewa na matatizo ya afya kwa binadamu pale zinapochomwa.

Kutokana na taka za Plastiki na uchafu unaooza kuwa changamoto kubwa inayoikabili Tanzania, Africa na Dunia kwa ujumla; kupitia Makala hii nimeelezea jinsi nilivyoweza kuchanganya Ubunifu na Teknolojia, kupata suluhisho la kipekee kwa uchafu na nishati kwa ujumla kwa kubuni na kutengeneza kifaa au mashine inayoitwa NISHATI-MIX.

MASHINE YA NISHATI-MIX
NISHATI-MIX
ni mashine inayozalisha umeme pamoja na gesi ya kupikia kwa kutumia plastiki na uchafu unaooza. Mashine hii ya kuvutia inatoa suluhisho la ubunifu kwa matatizo mawili: uchafuzi wa mazingira na upungufu wa nishati, ambayo ni matatizo yanayoikabili jamii ya watanzania ,waliopo mijini pamoja na vijijini kwa ujumla.

TEKNOLOJIA NA MUUNDO WA NISHATI-MIX

Nishati-Mix ni mashine iliyoundwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa na michakato miwili inayosaidia kubadilisha taka za plastiki na uchafu unaooza kuwa vyanzo vya nishati mbadala. Michakato hiyo huitwa "pyrolysis,” Pamoja na ‘’gasification’’ambapo taka huchomwa bila oksijeni,na kuchakatwa na hatimaye kuzalisha mafuta mazito(liquid fuel) Pamoja na gesi. Kifaa hicho kina sehemu kadhaa muhimu:
  • Mfumo wa Kuchoma: Taka za plastiki na uchafu unaooza huingizwa kwenye mfumo wa kuchoma. Hapa, joto kali hutumika kuchoma taka hizo bila kuwepo kwa hewa.
  • Mfumo wa Pyrolysis:Taka zilizochomwa huingia kwenye mfumo wa pyrolysis ambapo mafuta mazito na gesi hutokea. Mafuta mazito yanaweza kutumiwa kama nishati mbadala kwa ajili ya kuzalisha umeme au kwa ajili ya matumizi ya viwandani. Gesi inayozalishwa inaweza kutumiwa kwa kupikia, kuendesha mtambo, au hata kuzalisha umeme.
  • Mfumo wa kutengeneza gesi (gasification);Mfumo huu umeungana na mfumo wa pairolisisi Taka za kikaboni (zinazooza) baada ya kuchakatwa huingia kwenye mfumo huu na husaidia uzalishwaji wa gesi na uhifadhi wa gesi kwa ajili ya matumizi mbalimbali.
  • Mfumo wa Uchujaji:Mfumo huu hutumiwa kuondoa uchafu wowote uliobaki kutoka kwenye mafuta mazito na gesi ili kuhakikisha kuwa nishati inayozalishwa ni safi na salama kwa matumizi,na kuhakikisha hakuna uchafuzi wowote kutoka kwenye mashine.
  • Mfumo wa umeme: mfumo huu umeundwa na sehemu ya injini ,ambayo huweza kutumika kuzalisha nishati ya umeme .

View attachment 2650426
Kielelezo namba 1: muundo wa nishati-mix
View attachment 2650431
Kielelezo namba 2:muonekano wa NISHATI-MIX

MALIGHAFI ZINAZOTUMIKA.

NISHATI MIX hutumia malighafi taka, ambazo ni plastiki Pamoja na taka zinazooza pekee katika kuzalisha umeme na gesi.
Taka hizi zikusanywa, zinaandaliwa na kusagwa na pia kuunganishwa kutengeneza vipande vidogo vidogo (blocks) kwa kilo, vyenye uzito mbalimbali .Vipande hivi ndivyo huingizwa kwenye mashine kwa ajili ya kuzalisha nishati ya umeme pamoja na gesi.

View attachment 2650427
Kielelezo namba 3: malighafi taka katika vipande

UMUHIMU WA NISHATI-MIX

Nishati-Mix ina umuhimu mkubwa katika jamii yetu kwa sababu zifuatazo:

  • Kupunguza Uchafuzi wa Mazingira: Kwa kutumia Nishati-Mix, taka za plastiki na uchafu unaooza ambao ungekuwa chanzo cha uchafuzi wa mazingira sasa unageuzwa kuwa vyanzo vya nishati safi. Hii inapunguza kiwango cha taka zinazoelekezwa kwenye dampo la taka na kusaidia kulinda mazingira yetu.
  • Kuongeza Upatikanaji wa Nishati: Nishati-Mix ina uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha kuendesha shughuli mbalimbali pamoja na gesi, vyanzo viwili muhimu vya nishati. Kwa kuwa inatumia taka za plastiki na uchafu unaooza, kuna chanzo cha nishati kinachopatikana karibu na maeneo mengi. Hii inaleta faida kubwa kwa maeneo yasiyo na upatikanaji wa nishati ya kawaida.
  • Kupunguza Utegemezi wa Nishati ya Mizani: Nishati-Mix inachangia kupunguza utegemezi wa jamii kwa vyanzo vya nishati ya mizani kama mafuta ya petroli na gesi asilia. Hii inasaidia kupunguza gharama za nishati na kuongeza uhuru wa nishati kwa jamii.
  • Kuboresha Maisha ya Jamii: Kwa kuzalisha umeme na gesi, Nishati-Mix inatoa fursa za kuboresha maisha ya watu. Umeme unahitajika kwa ajili ya taa, kupasha joto, na kuendesha vifaa vya umeme, wakati gesi inaweza kutumika kwa kupikia. Hii inasaidia kuongeza ufanisi na kuboresha maisha ya watu.


HITIMISHO
Nishati-Mix
ni hatua muhimu kuelekea maendeleo endelevu na matumizi bora ya rasilimali zetu za asili na ni wazo zuri kutumia mashine kama NISHATI-MIX, ambayo inaonyesha uwajibikaji na nia ya kudumisha utawala bora kwa njia mbili: kwanza, kwa kuchangia katika kupunguza uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na plastiki na taka nyingine; na pili, kwa kutoa nishati mbadala ambayo inaweza kuwa na athari nzuri kwa jamii.

Kwa kutumia vifaa kama NISHATI-MIX unaweza kuchangia katika jitihada za kupunguza matumizi ya vyanzo vya nishati ya kisasa ambayo inaweza kusababisha uchafuzi wa mazingira na mabadiliko ya hali ya hewa. Kwa kugeuza plastiki na uchafu wa mazingira kuwa nishati mbadala, unaweza kupunguza athari za uchafuzi wa mazingira na kuchangia katika kuhifadhi rasilimali za asili.

Mashine hii haijaingia sokoni, lakini ipo kwenye hatua za mwisho za majaribio katika sehemu mbalimbali ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Hivyo basi kupitia Makala hii naendelea kuhamasisha na kuomba ushirikiano katika kupigana na changamoto za plastiki na uchafu kwenye mazingira kwa ujumla, na Pia kuomba taasisi na mashirika mbalimbali kuunga mkono bunifu ambazo zinalenga maendeleo ya nchi yetu ya Tanzania katika nyanja mbalimbali.
Big up to u
 
Kazi nzuri na jitihada nzuri, upatikanaji Wa uwezeshwaji kutoka Kwa Dola utasaidia jamii mahususi,; 👍👍 Big up Kwa jitihada.
 
Back
Top Bottom