Nishati Safi ya Kupikia (PPP tunayohitaji Kuingia)

Nishati Safi ya Kupikia (PPP tunayohitaji Kuingia)

Logikos

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
15,460
Reaction score
24,233
Private Public Partnership inafaa pale tu ambapo kuna mtu binafsi ana kitu ambacho serikali haiwezi kufanya, au anaweza kukifanya kwa ubora; Win Win Situation. Sasa katika Suala la Nishati Safi ya Kupikia kuna majiko ya kisasa ya Induction Cooker ambayo yana ufanisi wa percent 90; Yana Ufanisi zaidi ya mara mbili ya Jiko la gesi; Hivyo kwa mtu anayepikia tuseme kwa gesi kwa elfu sitini; ufanisi wa hili Jiko ni kama ataweza kupikia chini ya elfu 30 (Na hapo ni kwa gharama ya 192/= kwa Unit kwa mijini) kwa vijijini atakuwa ni kama anaweza kupika kwa elfu 10 (Gharama za Units kwa 100/=) kwahio, wakati jirani yake anatoa elfu 56 mpaka sitini yeye anatoa elfu 10/=

Gharama ya Majiko
Sababu teknolojia hii sio ya zamani sana hivyo gharama ipo juu kidogo kama watu watakwenda kununua madukani na pia inahitaji vyombo / chombo ambacho ni cha chuma (ferromagnetic) na sio sufuria za kawaida.

Nimeangalia kwa haraka haraka hapa nimeona majiko haya nchini ya plate moja yapo mpaka ya Tshs. 140,000/= (Ingawa kama tunaweza kutoa Mitungi bure huenda tunaweza pia kutoa ruzuku ya majiko haya)

Ushauri wa Partnership na Serikali / TANESCO
Kuliko watu kununua kutoka huko nje na baada ya gharama ya usafiri na faida yao hivyo bei kuwa kubwa; Tanesco inaweza kuingia Partnership na Kampuni ya kutengeneza majiko haya na kuagiza in bulk, au kuleta Assembly Plant nchini ili kuhakikisha kuna majiko ya kutosha na mtu wa kawaida anaweza kumudu Pesa za kuyanunulia.

Jinsi ya Mwananchi Atakavyolipa
Kutokana na kwamba TANESCO ndio atakuwa Msambaji wa haya Majiko anaweza akawapa watu kwa mkopo na kila anavyonunua Umeme wanakata Pesa yao ya Malipo ya Jiko hili kulingana na mtu alivyonunua.

Hii wanaweza kufanya sio kwa Induction Cooker pekee, hata vifaa vingine kama Multi Cooker, Rice Cooker, Jug Kettles, Blender n.k.

Hitimisho
Kwa kufanya hivyo wananchi watakuwa wameweza kuingia kwenye Nishati Safi, ya Kupikia kwa Gharama wanayoweza na Kama nchi Taifa tutakuwa tumejizatiti kwenye Usalama na huenda tukawa Taifa linaloongoza kwa Nishati Safi (Percent Kubwa from Renewable Energy)

Tuanzie Tulipo, Tutumie Tulichonacho, Tufanye Tunachoweza...
 
Makala Nyingine za Mtiririko Huu







 
Nishati safi kingali LPG ipo bei juuu. Turudishe crude oil refenery enzi ya TIPER
Kwanini tutumie LPG ? Kwa Mtizamo wangu LPG is out of question, kama issue ni kupikia hizo pesa za kurudisha refinery kwanini tusiwekeze kuwaunganisha watu wote na umeme na kupisha Nishati kwenye Waya....

After all Energy can Never be Created nor Destroyed - only converted from one form of energy to another.

Kwahio hivyo vyanzo vyote vya Nishati kama ni Bei ni Rafiki viende kufua Umeme (TANESCO) na usambazaji unakuwa through Waya na sio Bajaji kuleta Mitungi majumbani..., Kama tungekuwa na Uwezo tungeweza Kutumia Gesi Asilia ya Mtwara na kuisafirisha kwa mabomba mpaka majumbani (ila its cheaper kusafirisha waya na tayari nyumba nyingi zina waya)
 
Kwanini tutumie LPG ? Kwa Mtizamo wangu LPG is out of question, kama issue ni kupikia hizo pesa za kurudisha refinery kwanini tusiwekeze kuwaunganisha watu wote na umeme na kupisha Nishati kwenye Waya....

After all Energy can Never be Created nor Destroyed - only converted from one form of energy to another.

Kwahio hivyo vyanzo vyote vya Nishati kama ni Bei ni Rafiki viende kufua Umeme (TANESCO) na usambazaji unakuwa through Waya na sio Bajaji kuleta Mitungi majumbani..., Kama tungekuwa na Uwezo tungeweza Kutumia Gesi Asilia ya Mtwara na kuisafirisha kwa mabomba mpaka majumbani (ila its cheaper kusafirisha waya na tayari nyumba nyingi zina waya)
Lpg haikwepeki brooo umeme unakatika hapo vipi
 
Lpg haikwepeki brooo umeme unakatika hapo vipi
Kama umeme unakatika kwanini tusihakikishe haukatiki (ulizia mababu zako zamani umeme ndio ulikuwa source ya kupikia watu walikuwa wanaogopa gesi kwamba zitalipuka)

Vilevile Tungekuwa Algeria tunaozalisha LPG hapo sawa ndio maana wenyewe wanatumia LPG mpaka kwenye magari (Using one's own Strength)

Sasa sisi tuna Vyanzo vya Umeme vya kumwaga alafu uniambie tukanunue LPG nchi za nje sababu Umeme unakatikakatika unaona hilo ni jambo sustainable ?

Sasa na hio LPG kesho ikipanda bei huko Ughaibuni inakuwaje tunaendelea kutumia Kodi zetu kama ruzuku ?

Pia kama LPG ni very cheap kwanini tusiipeleke kwenye kufua umeme ili hio Heat Energy ibadilishwe kuwa electric energy ?
 
Lpg haikwepeki brooo umeme unakatika hapo vipi
Mkuu nasubiri Rebuttal... , Umesema LPG haiepukiki nimekujibu hapo juu sasa nasubiri jibu la jibu ili nitoe jibu (Huenda kuna kitu umekiona ambacho mimi sijakiona)
 
Ushauri wa Partnership na Serikali / TANESCO
Kuliko watu kununua kutoka huko nje na baada ya gharama ya usafiri na faida yao hivyo bei kuwa kubwa; Tanesco inaweza kuingia Partnership na Kampuni ya kutengeneza majiko haya na kuagiza in bulk, au kuleta Assembly Plant nchini ili kuhakikisha kuna majiko ya kutosha na mtu wa kawaida anaweza kumudu Pesa za kuyanunulia.
👍
 
Mkuu watu wenye akili kama wewe hawatakiwi ndani ya nchi hii
Watu wenye kuleta teknolojia ya kuwarahisishia watanzania maisha hawatakiwi na serikali hii CCM
 
Mkuu watu wenye akili kama wewe hawatakiwi ndani ya nchi hii
Watu wenye kuleta teknolojia ya kuwarahisishia watanzania maisha hawatakiwi na serikali hii CCM
Hii issue inabidi sisi wananchi ndio tuje juu sababu huko tunapoelekea kutatugharimu sana..., yaani kwanini mtu ununue mtungi elfu 56 mpaka 60 kwa maisha haya magumu wakati kuna uwezekano wa kila mtanzania kuzalisha umeme wa solar na kupewa credit hivyo kama wananchi mtu anaweza kupikia nishati safi ya umeme bila kulipia gharama yoyote....

Na ukizingatia sasa hivi vijijini wanatumia nishati bila kutoa hata senti moja (kuni za kuokota) itakuwa rahisi kuhamia kwenye umeme na kutumia kwa kuanzia gharama ya Tshs 0/=


 
Kama umeme unakatika kwanini tusihakikishe haukatiki (ulizia mababu zako zamani umeme ndio ulikuwa source ya kupikia watu walikuwa wanaogopa gesi kwamba zitalipuka)

Vilevile Tungekuwa Algeria tunaozalisha LPG hapo sawa ndio maana wenyewe wanatumia LPG mpaka kwenye magari (Using one's own Strength)

Sasa sisi tuna Vyanzo vya Umeme vya kumwaga alafu uniambie tukanunue LPG nchi za nje sababu Umeme unakatikakatika unaona hilo ni jambo sustainable ?

Sasa na hio LPG kesho ikipanda bei huko Ughaibuni inakuwaje tunaendelea kutumia Kodi zetu kama ruzuku ?

Pia kama LPG ni very cheap kwanini tusiipeleke kwenye kufua umeme ili hio Heat Energy ibadilishwe kuwa electric energy ?
Mali inapotea hapa
Screenshot_20241031_090647_Photos~2.png
 
Naam na hii huwa inatokea sana tena uvujaji wa gesi ya aina hii ni uchafuzi wa hali ya juu wa mazingira bora hata wanaotumia vijikuni vya kuokota okota.....

Pili kama tungeweza kutandaza mabomba kama maji kutoka source mpaka kwa mtumiaji hio ingekuwa ni hatua bora sababu kungepunguza overheads lakini uwezo wa kutandaza hio kitu sidhani kama tunayo ila tunaweza kutandaza bomba moja mpaka sehemu ya kufua umeme au kutandaza bomba moja mpaka kwa jirani tuwauzie gesi.

Kwa Tanzania narudia tena na tena yaani tunaweza kutumia Umeme na kwa Usimamizi wa Tanesco kila raia anaweza kuwa mzalishaji wa umeme

 
Naam na hii huwa inatokea sana tena uvujaji wa gesi ya aina hii ni uchafuzi wa hali ya juu wa mazingira bora hata wanaotumia vijikuni vya kuokota okota.....

Pili kama tungeweza kutandaza mabomba kama maji kutoka source mpaka kwa mtumiaji hio ingekuwa ni hatua bora sababu kungepunguza overheads lakini uwezo wa kutandaza hio kitu sidhani kama tunayo ila tunaweza kutandaza bomba moja mpaka sehemu ya kufua umeme au kutandaza bomba moja mpaka kwa jirani tuwauzie gesi.

Kwa Tanzania narudia tena na tena yaani tunaweza kutumia Umeme na kwa Usimamizi wa Tanesco kila raia anaweza kuwa mzalishaji wa umeme

Nimesoma makala zako boss, kwa kweli kila kitu kinawezekana, hata kama tukitaka kuzalisha na kutengeneza panel zetu uwezekano upo pia

Tatizo letu kila kitu tunaona hatuwezi na hata kufanikisha ni tabu kwa sababu ya upigaji na ujanja mwingi
Kuna mada nilichangia kuhusu magari ya Umeme
Nilisema kwa sisi bado sana maana magari ndio yameanza sasa na bei zipo juu sana
Je hatuwezi kuwaza sisi kuwa watengenezaji wa batteries za magari ya Umeme?
Kwa kweli leo sisi sio wa kuwa na mgao wa umeme kila leo au kukatika kwa maji mikoani na hata Dar

Vyanzo tunavyo ila tuko hovyo kwa kila kitu
 
Private Public Partnership inafaa pale tu ambapo kuna mtu binafsi ana kitu ambacho serikali haiwezi kufanya, au anaweza kukifanya kwa ubora; Win Win Situation. Sasa katika Suala la Nishati Safi ya Kupikia kuna majiko ya kisasa ya Induction Cooker ambayo yana ufanisi wa percent 90; Yana Ufanisi zaidi ya mara mbili ya Jiko la gesi; Hivyo kwa mtu anayepikia tuseme kwa gesi kwa elfu sitini; ufanisi wa hili Jiko ni kama ataweza kupikia chini ya elfu 30 (Na hapo ni kwa gharama ya 192/= kwa Unit kwa mijini) kwa vijijini atakuwa ni kama anaweza kupika kwa elfu 10 (Gharama za Units kwa 100/=) kwahio, wakati jirani yake anatoa elfu 56 mpaka sitini yeye anatoa elfu 10/=

Gharama ya Majiko
Sababu teknolojia hii sio ya zamani sana hivyo gharama ipo juu kidogo kama watu watakwenda kununua madukani na pia inahitaji vyombo / chombo ambacho ni cha chuma (ferromagnetic) na sio sufuria za kawaida.

Nimeangalia kwa haraka haraka hapa nimeona majiko haya nchini ya plate moja yapo mpaka ya Tshs. 140,000/= (Ingawa kama tunaweza kutoa Mitungi bure huenda tunaweza pia kutoa ruzuku ya majiko haya)

Ushauri wa Partnership na Serikali / TANESCO
Kuliko watu kununua kutoka huko nje na baada ya gharama ya usafiri na faida yao hivyo bei kuwa kubwa; Tanesco inaweza kuingia Partnership na Kampuni ya kutengeneza majiko haya na kuagiza in bulk, au kuleta Assembly Plant nchini ili kuhakikisha kuna majiko ya kutosha na mtu wa kawaida anaweza kumudu Pesa za kuyanunulia.

Jinsi ya Mwananchi Atakavyolipa
Kutokana na kwamba TANESCO ndio atakuwa Msambaji wa haya Majiko anaweza akawapa watu kwa mkopo na kila anavyonunua Umeme wanakata Pesa yao ya Malipo ya Jiko hili kulingana na mtu alivyonunua.

Hii wanaweza kufanya sio kwa Induction Cooker pekee, hata vifaa vingine kama Multi Cooker, Rice Cooker, Jug Kettles, Blender n.k.

Hitimisho
Kwa kufanya hivyo wananchi watakuwa wameweza kuingia kwenye Nishati Safi, ya Kupikia kwa Gharama wanayoweza na Kama nchi Taifa tutakuwa tumejizatiti kwenye Usalama na huenda tukawa Taifa linaloongoza kwa Nishati Safi (Percent Kubwa from Renewable Energy)

Tuanzie Tulipo, Tutumie Tulichonacho, Tufanye Tunachoweza...
Kabla ya kuandika hili bandiko ungeaanza kuwafikiria watumiaji na mahitaji yao kulingana na utamaduni wao. Tanzania inamakabila tamaduni zinazotofautiana sana hasa kwenye mapishi, mengi ya makabila haya hupika ugali wa mwidebe, yaani mpishi mpaka mabega na miguu inamuuma. Mabega ni kwa kusukuma mwiko kusonga ugali kilo tatu na nusu! Na miguu kukanyaga panda yaani upago unaoishika sufuria, kwa upishi huu ni vigumu kutumia jiko la umeme zaidi ya mafiga.
 
Kabla ya kuandika hili bandiko ungeaanza kuwafikiria watumiaji na mahitaji yao kulingana na utamaduni wao. Tanzania inamakabila tamaduni zinazotofautiana sana hasa kwenye mapishi, mengi ya makabila haya hupika ugali wa mwidebe, yaani mpishi mpaka mabega na miguu inamuuma. Mabega ni kwa kusukuma mwiko kusonga ugali kilo tatu na nusu! Na miguu kukanyaga panda yaani upago unaoishika sufuria, kwa upishi huu ni vigumu kutumia jiko la umeme zaidi ya mafiga.
Kwahio alternative ya mafiga ni gesi ? Sababu nachokwambia ni kwamba kuni na mikaa itapigwa marufuku na itakuwa ni kosa kwa mtu kutumia hivyo vitu..., sasa badala ya kumpa alternative ambayo ni cheaper huyu mtu atapewa mitungi ya gesi ambayo ni expensive ili tu madalali wa gesi wapige pesa kwa mgongo wa mwananchi...

Ni kwamba badala tu ya kutumia dollar kuagiza LPG na kuforce mtu atumie almost 300/ kwa unit ya gesi badala ya 100/= unit ya umeme tutakuwa tumesave dollar nyingi sana na kumuachia mpishi chenji za kununulia nyama badala ya kununua LPG ya mtu wa ughaibuni

 
Back
Top Bottom