Nishauri; biashara gani inamfaa kwa sifa hizi;

Nishauri; biashara gani inamfaa kwa sifa hizi;

Kichwa Ngumu

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2010
Posts
1,726
Reaction score
314
Hi JF Members;
nimeoa na ni mtumishi wa umma; mke wangu ni mama wa nyumbani hana kazi yoyote.
naamini nikimwezesha anaweza.
sina kipato kikubwa sana lakini naweza kupata kama 1.5 milioni ili aanzishe biashara yoyote.
naomba wana JF mnishauri ni biashara gani inaweza kufaa kwa mtaji huo
thank you in advance
 
Tueleze Unaishi mkoa gani,intrest za Wife zitasaidia ktk kushauri type of business.
i would suggest aende sido ,wanatoa training za kutengeneza
1-Shampoo ,liquid soap production etc
2 Food packaging
3.Baking-Cake za Harusi ,party etc
 
Mazingira na apendacho shemeji kama jamaa alivyopendekeza hapo juu pia na jamii inayowazunguuka,mkuu.
 
mazingira ya biashara ni muhimu kuyafahamu kabla ya kuamua kufanya biashara mkuu
 
Tueleze Unaishi mkoa gani,intrest za Wife zitasaidia ktk kushauri type of business.
i would suggest aende sido ,wanatoa training za kutengeneza
1-Shampoo ,liquid soap production etc
2 Food packaging
3.Baking-Cake za Harusi ,party etc
Kwa sasa naishi Mkoa wa Tanga, Wilaya ya Korogwe;
kabla sijamuoa alikuwa ananunua nguo na kukopesha
nitafuata ushauri wako tutavisit sido
 
kama unapoishi pana sehemu kuna soko lenye watu wengi, hata duka la rejareja litamfaa ili mradi kuwe na uhakika wa kupata bidhaa kwa bei ya jumla. utafiti muhimu.
 
Tembelea sido kama walivyokushauri na ucheki utakachokiona kinafaa. Ni kitu ambacho mkeo akipende kukifanya sio kumlazimisha cha kufanya.

Kwa 1.5 million unaweza kuanzisha biashara kwa kuzingatia vifuatavyo:

1. Ni biashara gani inayotoka sana ambayo unaweza kuanzisha kwa mtaji mdogo
2. Fanya shughuli unayoipenda kwasababu ukiwa unafanya shughuli unayoipenda hata kama uko katika kipindi kigumu kibiashara unakuwa una motivation kuendelea kuifanya coz unaipenda.
3. Angalia matatizo yanayoizunguka jamii unapoishi na kutafuta solution yake. Hapo unapata idea ya biashara manaake mi naamini biashara ni kuisaisia jamii nayo inakulipa kwa solution unayoipa.

Biashara nazoweza kufikiria kwa haraka haraka ni hizi:

1. Kuanzisha duka dogo la kuuza vocha za simu. Hizi ni bidhaa zinazotoka fasta
2. Kwasasa kuna maeneo hawana umeme so wanategemea mishumaa. Anzisha biashara ya ketengeneza mishumaa nyumbani. Mtaji wake ni mdogo tofauti na watu wanavyofikiri. Jifunze kwa ku click hapa:

[url]http://www.youtube.com/watch?v=FmKa_XJArLY

[/URL]How to Make a Candle: Step-by-Step Instructions for an Easy Candle - YouTubeHome made candles part 1 - YouTube
So nimekupa linki tatu wanatumia njia tofauti tofauti so chagua njia utakayoona inafaa au mix hizo techniques na kutengeneza ya kwako

3. Nunua pikipiki ufanye bodaboda (nadhani hilo ndo neno lake).
4. Anzisha biashara ya matofali ya kuchoma. Tafuta eneo mweke kijana awe anachoma matofali wewe unakuwa unaenda kutafuta wateja.

Nadhani hizo zitakusaidia.
 
Tembelea sido kama walivyokushauri na ucheki utakachokiona kinafaa. Ni kitu ambacho mkeo akipende kukifanya sio kumlazimisha cha kufanya.

Kwa 1.5 million unaweza kuanzisha biashara kwa kuzingatia vifuatavyo:

1. Ni biashara gani inayotoka sana ambayo unaweza kuanzisha kwa mtaji mdogo
2. Fanya shughuli unayoipenda kwasababu ukiwa unafanya shughuli unayoipenda hata kama uko katika kipindi kigumu kibiashara unakuwa una motivation kuendelea kuifanya coz unaipenda.
3. Angalia matatizo yanayoizunguka jamii unapoishi na kutafuta solution yake. Hapo unapata idea ya biashara manaake mi naamini biashara ni kuisaisia jamii nayo inakulipa kwa solution unayoipa.

Biashara nazoweza kufikiria kwa haraka haraka ni hizi:

1. Kuanzisha duka dogo la kuuza vocha za simu. Hizi ni bidhaa zinazotoka fasta
2. Kwasasa kuna maeneo hawana umeme so wanategemea mishumaa. Anzisha biashara ya ketengeneza mishumaa nyumbani. Mtaji wake ni mdogo tofauti na watu wanavyofikiri. Jifunze kwa ku click hapa:

How To Make Candles - Step by Step - YouTube
How to Make a Candle: Step-by-Step Instructions for an Easy Candle - YouTubeHome made candles part 1 - YouTube
So nimekupa linki tatu wanatumia njia tofauti tofauti so chagua njia utakayoona inafaa au mix hizo techniques na kutengeneza ya kwako

3. Nunua pikipiki ufanye bodaboda (nadhani hilo ndo neno lake).
4. Anzisha biashara ya matofali ya kuchoma. Tafuta eneo mweke kijana awe anachoma matofali wewe unakuwa unaenda kutafuta wateja.

Nadhani hizo zitakusaidia.
Duuuuuuu!!!!!!!!!! asante
 
nimeipenda hiyo ya boda boda au bajaji tatizo hizo pikipiki au bajaji zahitaji sh. ngapi kama mtaji.
 
Back
Top Bottom