Nishauri kuhusu kozi za TCU

Chungu cha bibi

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2014
Posts
525
Reaction score
166
Habari Zenu Wana Jf......

Ni Hivi Basi Zikiwa zimebaki Siku Mbili Kabla Ya deadline Ya Kutoma Maombi Tcu Nlkua Nahitaji Ushauri Wenu Sana,Hasa Waliopo Chuo Au Waliokwishaa Maliza Hii Elimu...Nmemaliza Kidato cha sita mwaka Huu Kwenye PCM Nina CBC yaan 3-11..Oneni kozi Nilizochaguaa Je Niache Hvyo Hvyo Au Ipi Ikae Juu Ya Mwenzake Au Ipi Haipo Hapo Niongeze Kwa Kutumiaa Uzoefu Wako Wa Chuo Cha muhimu Ni Kupata chuo Na kozi Ambayo Ipo Marketable Kwa Marks Zangu....

1:Geomatics-Ardhi
2:Civil-DIT
3:Civil-Ardhi
4-Civil-Udsm
5-Electrical-Udsm

Ushauri Wenu Muhimu Makaka Na Madada Zangu Maana Siku Zimeishaaaa.....KARIBUNI WOTE
 
Kwanza ujiulize ndoto zako ni zipi na mara baada ya kumaliza chuo unataka kufanya mambo gani baada ya hapo utapata msimo wako wa kozi ipi unadhani kwako ni nzuri ili watakapokuja watu kutoa comment zao na wewe unakuwa na base ya kuchangia ili kuepusha kukuacha kwenye dilemma na kukuchanganya (ngoja waje nina imani baada ya michango yao utafika hatua ya kufanya maamuzi)
 

Asante Mkuu Ngoja Na wengine Waje Kunishauri..
 

Nadhani hiyo ya Civil DIT ungeweka ya kwanza.... upo sahihi kuchagua civil..hii nchi bado inajengwa..hakuna barabara..sewage system wala majengo..ila ni muhimu ujue kitu kimoja..

Ukisoma Civil one thing for sure..hautalala njaa ila..kupata utajiri itachukua muda kidogo..hadi ufungue kampuni yako au ufanye kazi kwenye kampuni kubwa na nafasi ya juu.
 

Ushauri mzuri umempa dogo ila utajiri ni process na kutuliza kichwa tu kikubwa ni kuhakikisha kuna sustainability katika maisha na ukiweza hilo kwanza mengine yanafuata
 

Asante Sana Mkuu..Ushauri Wako Ntauzingatia..
 
naona unapenda civil sana kwanini umeshindwa kuiweka civil udsm ya kwanza kabisa ..kama sio ya pili kama una hofu ya kukosa chuo..kwa mtazamo wangu wakati nasoma mimi kulikuwa FACULTY CIVIL(CEBE UDSM) civil eng kozi kama tatu 1.civil stuctural 2.civil transportation 3. civil water resources siku hizi naona wameiocombine watu watakuwa wanaspecialize mwaka watatu hope
na cut off za civil sio kubwa sana ingawa inategemea sana na ufaulu na maombi ya mwaka husika DEMAND ya watu ila kwa mtazamo wangu cut off zako zinameet vigezo vya kozi zote hizo juu..
mtazamo wangu unaweza weka hivi
1.CIVIL UDSM
2.CIVIL DIT
3.BSC BUILDING ECONOMICS ARDHI'
4.CIVIL ARDHI
5.ELECTRICAL UDSM

Bsc in building economics iko poa ya ardhi university(ndio ma QS maquantity surveyor )..

kumbuka kozi za engineering mara nyingi inategemea na demand ya mwaka ila cut off point huwa sio kubwa sana na ushindani sio mkubwa sana...
kipindi nasoma kwa engineering (UDSM )
TELECOM NA COMPUTER ENG UDSM ndio walikuwa wanachukua kwa cut off point kubwa 1.3 mpaka 1.7
inafuata ELECTRICAL NA CIVIL NA MINING
THEN MECHANICAL NA CHEMICAL PROCESING ENG
huo ndio ushauri wangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…