Dada
korino pole kwa haya unayopitia. Ni kazi sana kulea ndoa kama alivyosema
Jestina ila nakwambia kazi siyo kuilea bali kazi ni kuamua kuilea ndoa. ushauri wangu kwako ni huu na ukichanganya na wajumbe wengine utapata pa kutokea.
kwanza kwa muda wa mwaka mmoja, bado hujaona ma dia so just keep and wait to see more. Kwanza huyu mama ni miongoni mwa wale wazazi ambao hata kama mtoto wao amekuwa na kuona basi anataka awe contol rum ya hiyo familia ya mtoto wake. Huyu hutamani kuona kila kitu kinafanyiwa correspondence kwake mfano kama kuna mgeni aambiwe, kama kuna mipango ya maendeleo ashirikishwe kitu ambacho huwa sikipendi kabisa. mama huyu hufikia hata kutaka kujua kuwa mumeo anakupa nini na kwa wakati gani.
Tabia nyingine ambayo ni mbaya hapa naiona kwako na kwa mumeo,( nisamehe sana kwa haya na si nia yangu bali tunataka kujenga tu). ninyi sidhani kama wakati mnaoana mlikuwa mmefikia umri wa kuoa kiakili.(samahani initetee). kwanini nasema haya mngekuwa mmekuwa kiakili kiasi cha kufikia mentally kuoa basi jambo la kwanza kabisa mngekuwa na saying juu ya maisha yenu wenyewe. na kama mngelitaka hili mngejifunza kuwa huru kwa kukaa mbali na wazazi wa pande zote mbili. hili wala haliihitaji mtu akuelimishe. mwendo wa dk 10 unaousema na pata picha kuwa ni mtaa mmoja huo. Hapa mlikosea sana na nafikir mlipokuwa mnapanga kuish ahapo mlilenga kupata msaada wa karibu kutoka kwa ndugu wa mume tena naona jins mumeo alivyokuwa anakuaminisha juu ya kupata cheap labour hasa utakapojifungua. hili ndilo kosa kubwa mlilolifanya. hata kama ni kazi mlitakiwa mwende kupanga mbali na hiyo familia wakwe unawaona once in a blue moon.
cha kufanya sasa ongea na mumeo pasi kumficha ila kwa utaratibu kwa nidhamu, na kwa hisia sana ili akuelewa. tena wakati unamuelewesha juu ya hii hali hakikisha uwe vigezo vyako vimewapita hao ndugu wa mume, hapa namaanisha yale ya kwako kama mke uwe umeyatimiza kwa nidham ya hali ya juu. jitahd usikurupuke mweke mumeo kwenye mstari kimahaba kwa muda kidogo hadi ufanikiwe kuiteka akili yake, ukisha fanikiwa basi mweleze tena ukiwa na solution ila dont mention it mpaka yeye apropose. atakacho kipropose yeye basi hakikisha kinakufavour wewe kwa kiasi kikubwa. Ukitaka kumnunua vizuri huyo mumeo basi vijizawadi visikosekane, mpatie hata kama ni vijisoksi tu ili kumteka zaid.
katika solution taka kuhama eneo hilo kapange nyumba mahali ambapo ni mbali zaid na wao na ukienda huko simama wewe na mumeo mjitegemee. hakikisha kila kitu mnafanya wewe na mumeo wala usitake ushauri kwa upande mwingine. pia jiaminishe manake kutakataka misaada ukweni ndipo kunakoleta shida sana kati ya wanandoa.
kuna post niliwah kuandika nikatoa kanuni ya kuish na mama mkwe ni leo nairudia tena kwa ajili yako
- muheshimu kuliko mama yako
-usiwe mchoyo
- usiwe na ukaribu naye hata kidogo
- hakikisha mumeo anatimiza wajibu wake kwa mama yake.
- asijue mambo yako ya ndani hata kidogo chumbani kwako ni siri yako pia.
-umwombe mungu sana manake yeye ndiye atupaye hekima za kuweza kuish katika ndoa zetu
Hebu jaribu haya.