Nisome kozi gani ambayo inaajira kwa baadae?

ledson

Member
Joined
Feb 24, 2014
Posts
5
Reaction score
2
Jaman magreat thinkers ninaombeni msaada wenu. Nimemaliza kidato cha nne mwaka jana na kwa bahati mbaya nimepata 4 ya 32 na inanipasa kwenda chuo sio form 5. Je ni kozi gani itakayo kua na ajira hapo badae?
 
Xo kla alnfeli alikua hasikilizi wengne inaweza ikawa ni matatizo yanayo harib xaikolijia kama mimi!
 
Jaman magreat thnkers ninaomben msaada wenu nimemaliza kidato cha nne mwaka jana na kwa bahati mbaya nimepata 4 ya 32 na inanpasa kwenda chuo sio form 5 je ni coz gan itakayo kua na ajira hapo badae!

mkuu ledson, kwanza nikuulize uko mkoa gani?

pili, ningeomba kufahamu, ungependa kusoma nini ?

tatu, umejiaandaaje kwa gharama za masomo kama ada, usafiri, chakula na malazi?
 
Last edited by a moderator:
Nko mkoa wa iringa na nnapenda sana kusoma compyuta na kuhusu gharama nadhan ntaziweza ila ningependa kujua coz zitakazo kua na ajira zaidi.
 
Nko mkoa wa iringa na nnapenda sana kusoma compyuta na kuhusu gharama nadhan ntaziweza ila ningependa kujua coz zitakazo kua na ajira zaidi.

reply with quote ili nijulishwe, sawa mdogo wangu?

mbona naona una mkanganyiko kichwani? unataka computer huku unawaza koz zenye ajira?

ajira ndugu yangu zimebaki kwenye ualimu.. tena bado tu wanasumbuliwa kama unavyoona, udaktari na course nyingine za sayansi..

chagua moja kwanza.. naweza kukwambia ukasomee nursing kwa sababu ina ajira lakini wewe ukawa uko kwingine! si utaua watu rafiki yangu?
 
Dogo unapenda computer kusoma na unataka upate ajira haraka sasa mimi kwa ushaur wangu tu fikiria juu ya fani hizi kwa sasa Elimu,Afya na Kilimo na mifugo ukitaka makuu utaishia kuingiza nyimbo kwenye simu na kuchoma CD
sawa bro tell me more
 
Dogo unapenda computer kusoma na unataka upate ajira haraka sasa mimi kwa ushaur wangu tu fikiria juu ya fani hizi kwa sasa Elimu,Afya na Kilimo na mifugo ukitaka makuu utaishia kuingiza nyimbo kwenye simu na kuchoma CD

asipofata ushauri wako mkuu, basi asahau kula mema ya nchi hii maskini.
 
Dogo unapenda computer kusoma na unataka upate ajira haraka sasa mimi kwa ushaur wangu tu fikiria juu ya fani hizi kwa sasa Elimu,Afya na Kilimo na mifugo ukitaka makuu utaishia kuingiza nyimbo kwenye simu na kuchoma CD

Umempa ushauri mzuri sana kwa wakati muafaka
 
Jaman magreat thinkers ninaombeni msaada wenu. Nimemaliza kidato cha nne mwaka jana na kwa bahati mbaya nimepata 4 ya 32 na inanipasa kwenda chuo sio form 5. Je ni kozi gani itakayo kua na ajira hapo badae?

Soma ENGLISH COURSE
 
alokwambia ualim grade hyo wanachukua point hiyo nan? Labda ualimu wa awali(nursery teacher)
Kwa hiyo waalimu wa awali ndio wanakuwa vilaza mwanzo mwisho!!!! Mi nikadhani hawa ndio wanatakiwa wawe vichwa sana maana pale mtoto ndio anapoanzia kupata msingi. Leo nimegundua kumbe watoto wanaanza kuharibiwa mapema sanaaaaaa.
 
Jaman magreat thinkers ninaombeni msaada wenu. Nimemaliza kidato cha nne mwaka jana na kwa bahati mbaya nimepata 4 ya 32 na inanipasa kwenda chuo sio form 5. Je ni kozi gani itakayo kua na ajira hapo badae?

Nenda Karume ( Malinzi ) Football Academy Pale TFF au Symbion Sports Academy Ambayo Jana Tu Mtani Wangu Malinzi Ameitangaza na Utapata Mafunzo Mazuri Ya Kucheza Mpira na Hata Elimu Ya Masuala Mengine Pia, Kazi Kwako.
 
Jaman magreat thinkers ninaombeni msaada wenu. Nimemaliza kidato cha nne mwaka jana na kwa bahati mbaya nimepata 4 ya 32 na inanipasa kwenda chuo sio form 5. Je ni kozi gani itakayo kua na ajira hapo badae?

Performance yako ipo je kwenye masomo ya Biology, Chemistry, physics na Mathematics? Je unapenda kuwa Mwalimu, Nurse, bwana shamba, Afisa mifugo? Kama unataka ajira ya haraka basi pitia huko nilikokutajia otherwise kama mtoto wa kishua kamua course yeyote then ajira utamuomba mzazi wako ndio akusimamie. Four ya 32 kwa taratibu za ufaulu wa miaka ya nyuma ni sawa na four 26 kwakuwa three mwaka huu imeishia 31. Kisha tizama kama unazo credit 3 na combination ipo yenye CCD au CCC nenda private ukasome advance ukitoka form six utakuwa sawa tu na aliyechaguliwa kusoma government akiwa na one, only kama utasoma kwa bidii na kufaulu form six. Kwakuanzia weka matokeo yako au fuata ushauri wangu kama utaona shida kuyaweka hapa.
 
Huo uandishi wako tu ndio maana ulifeli.Inawezekana hata kwenye mtihani uliandika "Xo" badala ya "So".Uandishi huo wa kisharobaro unaboa sana eti "xaikolojia".P****fu sana!

Sijui nani mchawi wa hawa vijana kuandika wakidhani ni vifupishi kumbe ujinga tu: xo, xixi, xiyo, xijui, wengine wanaandika 'co' wakimaanisha 'so' hatari sana isitoshe na kwenye mitihani wanaandika hivohivo mfano 'da2' wakimaanisha 'dada'.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…