Nitaimisi JF kwa muda kidogo

Nitaimisi JF kwa muda kidogo

Shida na raha

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2014
Posts
3,773
Reaction score
3,471
Habari zenu wakubwa zangu, wazee wenzangu mayanki wenzangu kwa vile vizee vilivyomo humu shikamooni.

Ni kawaida yangu mimi kushinda jf maana naona ndo sehemu pekee inayonipa burudani na kunielimisha pia.
Kawaida yangu nimezowea kujiunga kifurushi cha mwezi hadi mwezi line special ambazo zinauzwa dola kumi kwa GB 10 basi nainjoi mnoo.

Sasa juzi line imemaliza mda wake na kila nikifatilia naambiwa hazipatikani na kutumia vi mb kila siku ni cost kwakweli.
Unaweza kutumia dola 20 kwa wiki mbili kwa mimi ambae nashinda kwenye mitandao.

Kwa ufupi ni hivyo ndugu zanguni kwa wale mabest zangu mkiona hamnioni Mara kwa mara mjue tatizo ndo hill mpaka ntakapofanikisha kuipata maana ina shida sana kupatikana.
Najua nitapitwa na mengi sana ila nitakua najaribu kuchungulia kidogo kidogo.

The list: nakuomba usiuchambe uzi wangu maana najua hiyo michambo ntakutana nayo.
Povu linaruhusiwa lakini lisiwe la kupitiliza.

Cha mdeko: nitakua napitwa na vijimambo vyako maana si kwa masifa yale pengine hauna lolote kitandani ni gogo la mnazi.

Ushimen: nitakosa vitabia vyako ambavyo vinawekera wengine ila mimi havinikeri maana naona kama burudani kwangu.

Mamndenyi: kwako sitii neno maana ni mtu ambae unajiheshim sana na mimi nakuheshim kama mama yangu.

Mzigua: ukiamua kuwapotezea watu pm wape na nasaha, maana wanakuja huku na mahasira yao mpaka wanaharibu nyuzi za watu.
Uzi unageuka kuwa kijiwe cha pombe kwa matusi ya watu uliowatosa.
Chonde chonde kanya watu wako huko huko ili vurugu lipunguwe.
 
Weka namba yako hapa nikurudhie salio
 
Aiseeee naona umeamua kweli week hii

Point niliyopata hapo ni kwamba upo US unajipigia promo [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Aiseeee naona umeamua kweli week hii

Point niliyopata hapo ni kwamba upo US unajipigia promo [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
Kesho kutwa nakuja Dodoma ili tuonane kidogo japo kwa macho.
 
Mmh vyuma vyako vimekaza sana, Pole
 
Hapo kwa Ushimen nami pananihusu. Huwa comment zake zinanifurahisha sana. Kumbe wengine wanakerekwa nazo!!!
 
Pole shida na raha. Ila ungebadilisha hiyo user name mpendwa. Ni kama inachangia kukuletea hizo "shida"
 
Back
Top Bottom