Uchaguzi 2020 Nitaipigia kura CCM 2020 ikiwa..

GHIBUU

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2011
Posts
4,432
Reaction score
3,013
Itarejesha mchakato wa katiba mpya bungeni ambao ulio taarishwa na tume ya Warioba .

Kuidhinisha mfumo wa Serikali tatu na kutekelezwa baada ya uchaguzi.

Kuahidi kusimamia demokrasia kuanzia hivi sasa na sio baada ya uchaguzi.

Kuachiwa huru wale wote waliokamatwa kwa kesi za kisiasa wakiwemo viongozi wa Uamsho.

Demand hizi zianze mwaka huu kabla ya Oktoba uchaguzi mkuu.

Mimi na familia yangu nitakuwa tayari kuipigia CCM na kuhamasisha .

Je, wewe ?
 
Ccm haihitaji kura hata moja ili kukaa madarakani. Inahitaji jeshi linaloitii na tume ya uchaguzi inayoweza kutii matakwa yao. Juzi kulikuwa na uchaguzi wa serikali za mitaa, hao viongozi wake wako madarakani kwa kura?
 
Uamsho waachiwe huru? Kama ni hivyo kura yako baki nayo hukohuko.

Muungano wenu ni wa kipekee sana na hivyo ulivyo una tija sana kwa wanañchi wa pànde zote.
 
Mimi kuipigia kura ccm nitakuwa namkosea mungu wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii listi we kaa nayo na familia yako
Wahusika wana ya kwao....'kwa gharama yoyote' 😂
 
Unaongea nini dogo, nyie mlibaki posho mkala na mkacheza mdumange kuwa mmeandika katiba, iko wapi?

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hii listi we kaa nayo na familia yako
Wahusika wana ya kwao....'kwa gharama yoyote' [emoji23]

🤷🏼‍♂️🤷🏼‍♂️🤷🏼‍♂️🤷🏼‍♂️[emoji1381]‍♂️[emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…