Nitaishi hivi hadi lini lini?

Nitaishi hivi hadi lini lini?

OmaryElias

Member
Joined
May 3, 2023
Posts
11
Reaction score
34
Sijui nimemkosea nin mwenyezi Mungu mimi kama kuna kosa napiga magoti natoa chozi mbele yako nisamehe nitoe kwenye haya mateso.

Natoa historia yangu fupi, sina elimu ya uandishi maana elimu yangu ya shuleni ni ndogo.

Kwa majina yangu ni Juma Elias Chacha, ni mwenyeji wa Tarime Bomani ndo nyumbani kwa baba mama yangu. Ni mwenyeji wa Singida Nkalakala Wilaya ya Makalama.

Mimi ndio mtoto wa kwanza anafuata mdogo wangu, mimi na mdogo wangu hatukuweza kupata malezi ya mama, mama alituacha baada ya kukosana na baba, baadae baba aliondoka akatuacha nyumbani akaenda mgodi wa Buhemba (Ilasaniro) tukawa tunaishi pale nyumbani mimi, mdogo wangu na bibi.

Maisha yalikua ni magumu sana, baba alikua anatuma hela kwa mbinde. Maisha yanasonga huku nasoma, nikamaliza elimu ya msingi ile nataka kuingia kidato cha kwanza nikapat matatizo ya kiafya ya uvimbe tumboni.

Tukazunguka mahospitali kupata tiba mwishoe nikapata nafuu, niliporudi sikuweza kuendelea na elimu ya sec nikawa nipo nyumban. Jamani mtanisamehe simu yangu ni ndogo haina uwezo wa kubeba maneno yote.
 
Sijui nimemkosea nin mwenyezi Mungu mimi kama kuna kosa napiga magoti natoa chozi mbele yako nisamehe nitoe kwenye haya mateso.

Natoa historia yangu fupi, sina elimu ya uandishi maana elimu yangu ya shuleni ni ndogo.

Kwa majina yangu ni Juma Elias Chacha, ni mwenyeji wa Tarime Bomani ndo nyumbani kwa baba mama yangu. Ni mwenyeji wa Singida Nkalakala Wilaya ya Makalama.

Mimi ndio mtoto wa kwanza anafuata mdogo wangu, mimi na mdogo wangu hatukuweza kupata malezi ya mama, mama alituacha baada ya kukosana na baba, baadae baba aliondoka akatuacha nyumbani akaenda mgodi wa Buhemba (Ilasaniro) tukawa tunaishi pale nyumbani mimi, mdogo wangu na bibi.

Maisha yalikua ni magumu sana, baba alikua anatuma hela kwa mbinde. Maisha yanasonga huku nasoma, nikamaliza elimu ya msingi ile nataka kuingia kidato cha kwanza nikapat matatizo ya kiafya ya uvimbe tumboni.

Tukazunguka mahospitali kupata tiba mwishoe nikapata nafuu, niliporudi sikuweza kuendelea na elimu ya sec nikawa nipo nyumban. Jamani mtanisamehe simu yangu ni ndogo haina uwezo wa kubeba maneno yote.
Pole sana OmaryElias umeeleza maisha yako na mapito pamoja na changamoto zako , tafadhali nenda moja kwa moja unahitaji msaada upi ? Wa kifedha ? Matibabu ? Au kazi ? Ijapokuwa umesema huna uwezo wa kutembea .

Pole sana hujafa haujaumbika lakini usijali bado kuna njia ya kuiendea hakika Mungu ni mwema .

Karibu
 
Back
Top Bottom