Nitajuaje gari inachemsha?

Ndikwega

R I P
Joined
Feb 1, 2012
Posts
5,979
Reaction score
5,527
Habari ya Majukumu humu Ndani.

Naomba kusaidiwa hiyo hoja. Je, nitajuaje gari yangu inachemsha?

Gari yangu nimeona haya, Je ndiyo Kuchemsha au mwanzo wa Kuchemsha?

1.Maji nikiweka yemejaa Mpaka Juu, nikiwasha gari baada ya muda nikazima nakufungua Radiotor naona maji hayaonekani.

2.Nimetembea na gari Umbali wa kama 5KM, nikafungua Bonet, natazama tena kwenye Mfuniko wa Radiator nasikia ile mfoko wa "fuuuuu" na mvuke kiasi unatoka.

Naomba msaada tafadhali kujua shida kama ipo hapa.

JituMirabaMinne.

Ahsanteni.
 
Una watu wanakutegemea?

Maana ni kama umejichoka hivi.

Hivi unaendeshaje gari na kwenda kufungua mfuniko wa Radiator?

Kuchemsha kwa gari unaangalia kwenye dashboard na siyo huko kwenye engine.
 
Una watu wanakutegemea?

Maana ni kama umejichoka hivi.

Hivi unaendeshaje gari na kwenda kufungua mfuniko wa Radiator?

Kuchemsha kwa gari unaangalia kwenye dashboard na siyo huko kwenye engine.
Ahsante saana Mkuu. Much Respect.
 
Mshale hauoneshi Mkuu. Na Coolant niifungue Mfuniko kujua kama ipo Maximum au naitazamaje?
Msinichoke Mkuu, maana najua ninyi ndiyo Watalaam wenyewe.
Kuna kama kidumu hivi cha kuwekea hiyo coolant (wengi wanaweka maji),kuna mshale wa maximum inabidi iwepo ili usione inapungua kwenye mfuniko ukifungua.

Kama maji(coolant) ipo yakutosha basi angalia kama radiator inavuja mahali au fan kama inafanya kazi.

If vyote viko poa basi inabd ukaisafishe yawezekana imeziba njia zake inazopitisha maji.
 
Boss Wakati Wote Tazama Gauge Ya Jo to La Gari Kama Ipo Sawa
Endapo Gauge Iko Normal Na Maji Yanapotea Ama Mvuke Unatoka

Jaribu Zoezi Hili Tafuta Gari Inayofanana na Yako

Muombe Mfuniko Wake Halafu Uweke Maji Funga. Halafu Endesha Gari Umbali Mrefu Uone Utakafungua Boneti Mvuke Utakuwepo Ama Laa!!
 
Nimekupata Mkuu. Shukrani.
 
Kama inakuteza kuchemsah mnk hata ujataja aina ya gar yenyewe bas Kama inakusubumbua sna funga feni direct yaani kitendo Cha kuweka switch on bas feni inaanza kuzungusha apo Apo na mshale hauwezi kupanda ovyo na itasahau maswala ya kuchemsha kwa gari ikiwa unatka kufany hvyo mtafute fundi waya afunge feni direct gari haiwez kuchemsha ovyo ovyo
 
Shukrani Mkuu.
 
Hizo zote 2 ni hali za kawaida sana wala zisikuumize kichwa.. Iko hivi

1. Unapojaza maji gari ikiwa imezimwa (imetulia) yanajaa kweny tank za radiator na kutulia ila unapowasha gari tayari yanaanza mzunguko wa kupooza engine hapo lazima yapungue sababu yametembea kweny engine yaan yapo kwen mzunguko. Unaweza kugundua kama gari inavuja kwa kukagua mwenyew upande wa chini wa radiator km inadongosha maji pia unaweza kuijaza full ikiwa ingine inatembea ili kujaza mfumo mzima wa kupooza, au unaweza kuangalia kiwango unachoongeza maji kila siku.. ukiona unaongeza maji kila siku au kila mara hapo kuna tatizo.

2. Suala la mfuniko kutoa sauti na kamvuke hapo tambua mfuniko wako uko sawa na unaifanya kazi yake ipasavyo.. Mifuniko ya radiator huwa ina act kama pressure release valve ambayo imesetiwa kweny kiwango flan cha joto na likifika hapo huwa inaachia mvuke wa moto kutoka nje ya radiator ukiangalia mfuniko huo kwa ndani una kitu kama spring na ruber ndo vinavyoruhusu huo mvuke unaouona.

Ikiwa umejaza maji yako kweny radiator gari ikiwa on kabla hujafunga mfuniko wa radiator kwanza angalia maji kama yametulia jua gasket iko sawa ila ukiona kama puvo au babbles zinapanda kutoka kweny radiator na kupasuka zikifika juu jua gasket yako huenda imeshaungua au ina cracks kadhaa.
 
Shukarani saaaaana kwa Maelezo ya Mazuri na ya Kina Mkuu. Ngoja nichek Kesho nifanye hilo zoezi la Mwisho kwenye maelezo yako Mkuu.. Ila kwenye Dashboard hakuna taa yeyote kwa maana ya gari kuchemsha.


Suala la pili ni hili la Kuongeza Maji, kiukweli Asubuhi ninapotaka Kuiwasha huwa naangalia Maji, naona kupungua kiasi cha kama Nusu Lita hivi huwa Naongeza ndiyo yanakuwa yamejaa kabisa pale Juu, sioni Kuvuja kokote ila kesho tena hata kama sijatembelea nakuta hayaonekani juu. Na huwa najaza kweli asubuhi kabla ya kuwasha.
Ila hakuna Kuvuja chini, vinginevyo nimejaza zaidi yanayovujia kwa kutoka juu hayo ndiyo nayaona kabisaaa.
Naomba kama kuna Maelezo ya ziada na tahadhali zozote ninazotakiwa Kuchukuwa.
Ahsante saana Mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…