Miaka kama 5 iliyopita nikiwa a bado nina nidhamu ya woga na upendo wa dhati kweri kweriiiiiy, nilitongozwaga na mkaka ambae tulikutana kwenye biashara za magari, nikaweka kipeperushi changu kwenye gari nikasepa mara akaniita, wee dada rudi hapa umeweka nini kwenye gari yangu? Nikamuelezeaaaa , akauliza ofisi zenu ziko wapi nikamjibu.
Akauliza umeolewa nikasema hapana, nipe no zako nimekupenda, kwa ujinga nikamjibu nina mchumba siwezi mimi, alinibembeleza sana huyo kaka akanambia anatakiwa kuoa ndani ya miezi 6, kiukweli nilimkataa na sikumpa no,na vipeperushi vilikuwa na no za ofisi tu.
Sasa baadae mambo si yakaharibika huko nilikokuwa napenda kifala, nikamkumbuka yule kaka, kumbuka mpaka uweke kipepeushi kwenye gari la mtu lazima uangali ni no gani so nikawa nakumbuka no za mwanzo ya mwisho ikagoma.
Nikawaza kwenda tra kuna kaka namjua anisaidie, akaniomba no ya usajili, sikumbuki yote, sikupata msaada maaa ningepata msaada hadi no za simu.
Nikaendelea kukua weeee na kazi nina nyingine nakutana na watu tena wa maana .juzi kwenye msiba wa jpm kabla sijaenda chato, nikaitwa sehemu na waombolezaji wenzangu nikajuana na watu wawili wote nawajua majina , mmoja nina no zake mwingine sina no zaje na siwezi ziomba kwa mwenzake na ninashida kweli kuongea nae.
Plate no yake ina majina yake mfano yaani yamefupishwa J....., sasa nikamcheki jamaa wa tra, ninataka no za hii plate no, majibu yake sasa,
Wee falaa nini, huyu mtu unamjuaje? Nikamwambia ni rafiki ila mimi sina no zake , hata leo tulikuwa nae ila no ya simu noma kuipata ingawa nikimwomba atanipa ila mazingira hayaruhusu[emoji23],akauliza majina yake nikamtajia ndo akaamini namjua. Ofcause hakunipa no yake , akanitaka niende ofisini sikwenda kuna kitu niliwaza si sawa.
Ndo nilijua wenye plate no za majina yao zinalipiwa 5ml kila mwaka, watu wana pesa asikwambie mtu.
So mleta mada, shika vipesa vyako mkononi nenda tra ongea na mtu ila uwe na sababu za maana utapewa kila kitu.