Nitapata wapi solar panels orginal ambazo zinaweza kusukuma pump ya maji kwa wingi na je zinaweza kuwa pannel ngapi na zitakuwa na gharama kiasi gani?

Ukikosa zaidi taarifa ingia google zipo info nyingi.
Pia waweza agiza china solar pump KWA bei nafuu
 
Kwa kisima cha mita 100 haiwezekani, lazima awe na source ya umeme
Oh !! nimekuelewa!!
, kisima cha mita mia pump inakaa chini ya kisima , sehemu ambayo huwezi weka diesel pump
 
Mkuu hii gharama yake ni kiasi gani kwa ujumla?
 
Kimsingi, unapotaka kujua ukubwa na idadi ya solar panel pamoja na vifaa vyake, unatakiwa uanzie;

1. Kwenye mahitaji yako halisi ya maji, let say kwa lisaa ni lita ngapi.
2. Then ujuwe unakuwa na storage tank au la. Na ukubwa wa storage tank utategemeana na mahitaji yako kwa saa.
3. Kutoka kwenye mahitaji ya maji, utapata uwezo wa water pump inayohitajika kujaza tanki lako.
4. The baada ya kujua uwezo wa water pump inayotakiwa, utajua electrical specifications za pump husika. Hence mpaka hapa utajua solar system yako itahitajika iwe na uwezo kiasi gani kwenye kuendesha pump pekee.
5. Then, toka kwenye ukubwa wa pump, utatakiwa ujuwe unahitaji solar system batteries zenye kuwezo wa kukaa na umeme kwa masaa mangapi zikiwa zinailisha pump yako. Ofcourse, ukubwa wa tank utakuambiwa, kwa pump yenye flow rate ya kiasi fulani, itaweza kujaza tank la lita kadhaa kwa muda fulani. Kwa hiyo, hapa utajuwa umeme kiasi gani unahitajika kuchaji batteries zikiwa zimetukia mpaka mwisho wake (kwenye voltage set value).
6. Mpaka hapa utakuwa umepata umeme unaotakiwa kuchaji batteries na kwa wakati huo huo unaotakiwa kuendesha pump. JUmla ya hizo mbili (power inayohitajika kuchaji batterie na power inayohitajika kuendesha pump) Kwa pamoja, utajua total power inayotakiwa iwe ndo uwezo wa solar system yako kuanzia wires, charger controller na solar panels.
 
Huyo ambaye solar system yake ilikuwa haiwezi fanya kai usiku, hakuwa na backup batteries?

Binafsi, yes, initial cost ya solar system ni kubwa, lakini runing and maintenance cost zipo chini sana. Hata kwenye operation, solar system inahitaji minimum manpower ukilinganisha na diesel engine unayomshauri ainunu.
Kwenye diesel
1. Life time fuel cost.
2. Life time maintenance cost (filters, coolant, air cleaner etc)
3. Life time risk ya kuto-check oil levels, coolant etc

BINAFSI NAMSHAURI AWEKE SOLAR SYSTEM
 
Umeongea kitaalamu sana nahisi ulienda post namba Sita nimeelewa namna gani ukubwa wa shamba ni ekari 40 kilimo ni mpunga hivyo sihitaji tank, kisima ni cha kuchimbwa na mashine chenyewe kipo tayari, walau kwa lisaa nipate lita 40 kama inawezekana na mashine iwake japo masaa 4 tu inatosha kwa siku na shamba likiloa naweza nisiwashe mashine hadi week nzima kuisha, walau pumb isukume maji umbali wa 200m hivi
 
Thanks kwa hili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…