Nitapataje kazi botswana? Wadau naombeni mchango wenu.....

Nitapataje kazi botswana? Wadau naombeni mchango wenu.....

sinande

Member
Joined
Jan 27, 2012
Posts
5
Reaction score
1
Kabla ya yote mimi ni mdau mpya kwenye JF,NAWAPENI HI WADAU WOTE WA JF

Mimi ni dentist,naombeni wadau wote mnipe mchongo inakuaje coz kuna wadau ambao wanauelewa mkubwa kuhusiana na masuala hayo.Mimi nipo peripheral,mambo mengi ni ngumu kuyafaham
 
Jaribu kuingia kwenye website mbalimbali za botswana,hasa zinazohusu ajira kwa wageni unaweza pata mwanga kidogo..
 
Juzi tu Mzee mmoja wa kibongo ka-staafu alikuwa mwajiriwa huko Botswana nikamwuliza khali ya ajira huko vipi? Kasema mambo mazuri yapo hapahapa Bongo,Botswana si ile ya zamani wamesomesha wana wataalamu wa kutosha ajira si bwerere kama enzi hizo! Nikamwuliza mzee mbona huko maisha mazuri na mishahara nasikia iko juu? Akajibu Mishahara mikubwa pia matumizi ni makubwa hakuna ndizi ya sh 200 kama Bongo ndizi moja sawa na buku ya kibongo,vitu vingi wanaagiza toka nje.Labda uwe single utaweza mudu maisha lakini kama unategemewa na familia au ukoo,utakuja rudi Bongo huna hata kiwanja.
Ahsante.
 
Halaf wewe si ndo umegoma?unaacha kusaidia nchi yako na ndugu zako unataka kwenda kusaidia makirikiri??naskia rate ya ukimwi iko juu sana ndo inaadhiri labour force yao.
 
Muulize Jamaa mmoja anaitwa Makupa, anafanya kazi huko Botswana japo hatuelewi anafanya nini? mtafute humu ndani yupo ukitaka kumpata kirahisi angalia thread zinazohusu CHADEMA
 
Siku hizi Botswana sio kama zamani.kupata tu kibali cha kuishi hapa kwa sasa ni kazi sana.Uthibiti wa wageni ni mkubwa sana hadi kero.Kama huna kazi inayokuingia kipato kizuri utaona kero tu kuishi hapa.kwanza wenyeji wenyewe hawana ushirikiano mzuri sana na wageni kama huko Tanzania.Ukipata sehemu yenye maslahi mazuri huko Tz ni bora ukabaki huko.Na endapo utapenda kuja kujionea mwenyewe uamuzi ni wako.
 
Back
Top Bottom