Sesten Zakazaka
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 10,559
- 19,101
Dhamana ya kwanza ya mkopo niLugha baba!!
1. Uwezo wa kulipa
2. Nia ya kulipa
Hakuna benki au taasisi yoyote ya fedha itaweza kukukopesha kwasababu tu eti unadhamana ya nyumba. Lazima uwe na biashara au wazo la biashara( taasisi chache sana kama zipo ndio zinakubali kukopesha wazo au biashara zinazo anza).
Kama sio hivyo basi lazima uwe muajiriwa wa taasisi rasmi iliyosajiliwa na unalipwa kwa uhakika mshahara wenye kueleweka na hiyo benki au taasisi ya fedha iwe na sera na bidhaa(product) ya kukopesha waajiriwa
Baada ya yote hayo ndio inafuata suala la kuweka dhamana mali inayokubalika kuwekwa dhamana na benki husika. Kila taasisi ya fedha ina sera ya kukubali kupokea aina ya dhamana. Kuna wengine wanakubali nyumba au viwanja vyenye hati kubwa(title deeds), wengine leseni za makazi na wengine hata hati za mauziano tu. Wengine hawakubali kiwanja kitupu hata kiwe Kariakoo au Masaki. Lazima kuwe na jengo hata likiwa dogo au bovu. Wengine wanapokea hata magari au mashine
Kuna dhamana nyingine ina nguvu sana, dhamana ya pesa taslimu. Hii maranyingi inakua kwenye mabenki na unatakiwa uweke pesa kwenye akauti ya muda maalumu(fixed deposit) kisha unaweza kukopeshwa hadi asilimia fulani ya pesa ulizoweka kutegemea na sera za benki husika. Tena bank zingine ukiweka cash wanapunguza mlolongo wa taratibu(procedures)