Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Mkuu Kichuguu na mimi leo nina jambo geni kidogo nimeliona linanitokea kwenye gari....

Gari linaendesheka Vizuri kama kawaida ila nikiwasha AC gari linapungua nguvu sana....nikizima tu AC, hapo hapo unasikia gari linakuwa lepesi sana na linachanganya faster...
Ni ishu mpya kabisa kuwahi kunitokea...
Shida yaweza kuwa ni nini..?
Gari Nissan Note 2005, HR15 Engine, CVT gear box....
 
Pole sana ndugu yangu; kadhia uliyopata inaweza kutokanana na moja ya sababu tano kuu au zote kwa pamoja kama ifuatavyo, yaani sababu moja ikisababisha nyingine.
(a) Bearing za AC Compressor kuwa zimekufa kwa hiyo inazuia injini kuzunguka freely
(b) Solenoid ya AC clutch kuwa imeaungua. Mara kwa mara AC Clutch solenoid ikifa, huunguza pia fuse kwa hiyo unakosa kabisa AC, ila kama fuse iliyokuwamo ni ya amperage kubwa zaidi ya kawaida basi utapata kadhia hiyo kwani AC inakuwa inachukua umeme wote wa gari, na kuacha sehemu nyingine za injini hazina umeme wa kutosha
(c) Alternator inakaribia kuishiwa nguvu, ukiwasha AC basi umeme wote unasihia huko na kuacha sehemu nyingine za injini hazina umeme wa kutosha.
(d) Pressure switch kwenye Compressor imekufa, kwa hiyo kunaweza kuwa na pressure kubwa sana kwenye compressor kiasi cha injini kushindwa kuizungusha.
(e) Piston moja au zaidi ndani ya Compressor zimekwama, kwa hiyo compressor haiwezi kzunguka

Ili kutest sababu (b) na (c) washa AC wakati taa zinawaka uone kama zitazimika; kutest sababu (d) gusa AC compressor kama ni ya moto sana; kutest sababu (a) na (e) inabidi kuifungua AC kukagua sehemu ndani ya compressor yenyewe.
 
Valve guides ndo valve seal mkuu
 
Carina yangu inachafua engine, nikiiosha leo engine baada ya3-4wks,nakuta engine imechafuka na oil imekua nyeusi, fundi akanishauri nibadilishe valve seal
 
Samahani mkuu STP unaweka kwenye tank la petrol au ni unapoweka engine oil mkuu
 
Samahani mkuu STP unaweka kwenye tank la petrol au ni unapoweka engine oil mkuu
Weka kwenye tanki la mafuta; chupa moja ya STP kwa full tank ya petroli; inasafisha hizo injectors kwa kwa kama wiki nzima hivi kulingana na unedeshaji wako.
 
Carina yangu inachafua engine, nikiiosha leo engine baada ya3-4wks,nakuta engine imechafuka na oil imekua nyeusi, fundi akanishauri nibadilishe valve seal
Hizo valve seals zikiharibika, basi oil inakuwa inaingia ndani ya coimbustion chamber na kuchomwa, utakuwa unapata moshi mweupe hivi kwenye exahust. Ila sasa kama injini inachafuka kwa oil, basi itakuwa ni cylinder head cover gasket ndiyo mbovu. siyo hizo valve guides (kwa jina jingine valve seals). Test mojawapo rahisi sana ya kuona kama oil inaingia kwenye combustion chamber ni hivi. Washa gari, halafu weka chukua kipande cha pamba au toilet paper, weka pale kwenye exhaust kama dakika kumi hivi. Kikishika masizi meusi utakayoweza kuona kirahisi kwa macho yako katika muda huo mfupi, basi ni dalili kubwa kuwa valve guides zimepanuka. Daima kutakuwa na masizi kidogo sana lakini siyo mengi ya kuona mpaka yanatia weusi.

Fundi wako pia anaweza kutoa spark plugs na kuzikagua; ukikuta zina unyevunyevu basi ni dalili moja kukubwa kuwa valve guide seals ziko hoi.

Ngoja nikutafutie picha kukuonyesha tofauti zake. Sijui kama picha hii umeielewa, inaonyesha valve zikiwa zimefunguliwa. Sasa hizo rings number 3 ndizo zenyewe. Picha ya kulia ni valve zenyewe zikiwa zimefungwa kwenye clinder head



Picha ya Clynder head gasket ni hii hapa




Oil kuwa nyeusi inategemea sana aina ya oili unayotumia; kuna oils zinazobadilika rangi kuwa nyeusi mapema sana baada ya kupita kwenye injini hata kabla hazijachoka.
 
Ni kweli kamba matumizi ya AC yanaongeza ulaji wa mafuta kwenye gari...??

Kuna mafundi wanasema ukiwasha gari alafu ukienda kuangalia kwenye exhaust ukikuta inatoa maji basi ujue engine ya gari ni nzima sana(kinanda) mpyaaaaa ??

Naomba kujua kazi ya ABS kwenye gari ?
Tyre za gari inatakiwa ubadirishe kwa muda gani,na zinafungwaje mana nimewai kuskia fundi anasema gari haikimbii sana hizo tyre zimegeuzwa kashata sijui
 
Ni kweli kamba matumizi ya AC yanaongeza ulaji wa mafuta kwenye gari...??
Ndiyo; AC inaendeshwa na injini na inahitaji nguvu sana, ndiyo maana ukiwasha AC lazima muunguruma wa gari ubadilike kidogo kwa vile inaaza kunywa mafuta mengi
Kuna mafundi wanasema ukiwasha gari alafu ukienda kuangalia kwenye exhaust ukikuta inatoa maji basi ujue engine ya gari ni nzima sana(kinanda) mpyaaaaa ??
Siyo kweli. Mafuta yakiungua ndani ya injini hutoa Carbon Dioxide na maji katika hali ya mvuke. Wakati gari linawashwa asubuhi lingali la baridi, mvuke huo uifika kwenye exahust huganda na kuwa maji ambayo ndiyo yanayodondoka kutoka kwenye Exhaust. Hiyo itatokea kwa injini yoyote iwe ina matatizo au haina matatzio mradi tu imewaka. Exhaust ikishakuwa ya moto, basi mvuke ule hauwezi kuganda tena na hivyo huwezi kuona maji yakitoka. Ila sasa iwapo gari linatoa maji kwenye exhaust muda wote hata pale ambapo exhaust imeshakuwa ya moto basi ujue kuwa injini ina matatizo makubwa. Ama cylinder head gasket imekufa au engine block ina ufa, kwa hiyo maji ya radiator yanapita moja kwa moja hadi kwenye exahust, na unaweza kuanza kuona kuwa injini inakausha maji mara kwa mara.
Naomba kujua kazi ya ABS kwenye gari ?
Inazuia gari isteleze ukikamata breki ya ghafla. kwenye barabara yenye utelezi ABS huwa inastabilize gari barabarani lakini unaweza kugonja kitu kilicho mbele yako kwa vile gali litaendelea bila kukwaruza barabara mpaka itakaposimama yenyewe. Ukiwa na ABS jiachunge uwe unaendesha kwa makini, breki za ghafla hazifanyi kazi
Tyre za gari inatakiwa ubadirishe kwa muda gani,na zinafungwaje mana nimewai kuskia fundi anasema gari haikimbii sana hizo tyre zimegeuzwa kashata sijui
Fuata maelekzo ya mtengezaji (manufacturer)
 
5w30 ni 56000 pale total mcity boss tena og from france.. hio 80000 itakua castrol ndio wana bei za ajabu za oil nahisi sababu ni brand kubwa wamejitangaza sana..
 
Huu uzi umenipa msononeko kidogo sina gari wala pikipiki,lakini nimejifunza mambo makubwa anyway..
Kuna gari ni automatic transmission ila navyoiendesha sasa kama manual transmission..
Iko hivi
Uki start engine inawaka vizuri ukiweka gear D au L au R inazima sasa nikitaka isizime nashika break.
Navyotaka kuondoka nakanyaga pedal ya mafuta na break kwa wakati mmoja alafu naachia break taratibu gari ndio inakubali kuondoka,nikitembea kidogo inaanza kusinzia nakanyaga break tena hapa inasimama kabisa nakanyaga mafuta mengi huku nimeshika break naachia break taratibu gari inaondoka..
Sijawai kuiendesha kwenye foleni mana ningekua na case ya kugonga gari za watu..
Kuna fundi pump ya kuvuta mafuta ipo mbele kwenye engine imekufa,manake hii gari ina pump kwenye tank na myingine ipo mbele kwenye engine
Mwingine akasema computer inatatizo inashindwa kichambua nini sijui
Mwingine akasema tuliweka mafuta machafu,
Engine ya gari ni D4 inatoa moshi kuna muda ukikanyaga mafuta sana wakati umesimama unakuta nyuma kwenye exhaust imemwaga kama unga mweusi hivi chini
 

Gari yoyote ya Automatic ukiwasha lazima uwe umebonyeza brake ama sivyo haliwezi kuwaka. Brake ile pia hufanya kazi kama clutch, kutenganisha injini na gearbox.
 
Thnxs mkuu,natumia castrol na niko huku mkoani so kidogo gharama zinakua juu kidogo lkn juna sehemu 5w-30 ya total nimeona wanauza Tsh 60,000 ila sijawahi kuitumia mkuu.
5w30 ni 56000 pale total mcity boss tena og from france.. hio 80000 itakua castrol ndio wana bei za ajabu za oil nahisi sababu ni brand kubwa wamejitangaza sana..
 
Kweli mkuu...hata huku Arusha total 5w 30 tunauziwa kuanzia 55000/-...
Castrol inahitaji umakini...zina soko sana...hivyo feki zipo...
5w30 ni 56000 pale total mcity boss tena og from france.. hio 80000 itakua castrol ndio wana bei za ajabu za oil nahisi sababu ni brand kubwa wamejitangaza sana..
 
Wakiuza 60000/- hiyo total siyo mbaya inategemea unaishi wapi coz maeneo mengi inaanzia 55000/
Mimi naitumia na ninaona mashine ya gari inafanya kaxi vizuri....injini inakuwa nyepesi vizuri
Thnxs mkuu,natumia castrol na niko huku mkoani so kidogo gharama zinakua juu kidogo lkn juna sehemu 5w-30 ya total nimeona wanauza Tsh 60,000 ila sijawahi kuitumia mkuu.
 
Gari yoyote ya Automatic ukiwasha lazima uwe umebonyeza brake ama sivyo haliwezi kuwaka. Brake ile pia hufanya kazi kama clutch, kutenganisha injini na gearbox.

Ni kweli mkuu sasà yenyewe inatetemeka kiasi kwamba ikitaka kuzima ili isizime inatakiwa ushike break hadi chini kabisa
 
Wakiuza 60000/- hiyo total siyo mbaya inategemea unaishi wapi coz maeneo mengi inaanzia 55000/
Mimi naitumia na ninaona mashine ya gari inafanya kaxi vizuri....injini inakuwa nyepesi vizuri

mkuu nipo arusha pia napata wapi castrol og au total nataka kwa ajili ya engine ya vtec sport car nadhan 5w30 ndo itafaa kama wadau walivosema apo juu
 
Gari yoyote ya Automatic ukiwasha lazima uwe umebonyeza brake ama sivyo haliwezi kuwaka. Brake ile pia hufanya kazi kama clutch, kutenganisha injini na gearbox.

Kaka mbona huwa nawasha bila kukanyaga brake na linawaka hapa imekaaje?
 
Kaka mbona huwa nawasha bila kukanyaga brake na linawaka hapa imekaaje?
Ni kweli; magari mengi ya zamani yalikuwa hayana tatizo la kukanyaga brake kabla ya kustart, yalikuwa yanakubali tu iwapo upo kweny parking position. Lakini magari ya siku hizi nadhani baada ya 2005 au 2006, hayakubali kustart iwapo hutabonyeza breki; vile vile huwezi kuzima gari na kuondoa ufunguo kabla ya kuliweka kwenye parking position wakati magari ya zamani yalikuwa yanaruhusu tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…