Niulize chochote kuhusu siri ya kuwa tajiri

Niulize chochote kuhusu siri ya kuwa tajiri

Shy land

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2013
Posts
6,208
Reaction score
2,767
kutokana na shule nyingi hapa tanzania kushidwa kuwafundisha vijana kuhusu somo muhimu la kuhusu siri ya utajiri.

Naomba kama una malengo ya kuwa tajiri, na unataka kujua siri ya utajiri niulize hapa hapa.

NB:kwa faida ya wengi usitumie lugha ya kingereza maana sitakujibu swali lako.

kama hujalizika na jibu la swali lako usikejeli, kwa kuwa jf wengi ni great thinker najua watakuja wengine kukusaidia kujibu swali lako.


Kumbukeni hili wakuu

sijaandika huu uzi kwa kujinasibu na kujitangaza jf, kwamba eti mimi ninajua sana siri ya utajiri.

lengo langu kuu ni kuweza kujadili hili somo muhimu ambalo hata shuleni huwezi ukalipata,,!

naelewa wazi kwamba jf kuna watu wana uwezo mzuri sana wa kuelezea kupita hata mimi.

mimi naamini kwamba mawazo ambayo mimi nayawaza kila siku hayawezi kulingana na ya kwako, hata na wewe siwezi nikajua unachowaza

karibuni sana kwa mdahalo.
 
Ni kweli ubahili ni moja ya mbinu za kuwa tajiri??kama kweli kwanin na nivip??
 
Tajiri ni nani/mtu wa aina gani?

Nimeshagaa sana kukutana na swali kama hili kwa mtu anayejiita great thinker

swali ambalo unaweza hata jibu lake kulipata hata kwenye kamusi.

Tajiri ni mtu anayemiliki vitu vya thamani, pesa, majumba biashara mbalimbali. pamoja na kuwa ni vyazo vingi vya mapato,.
 
Ni kweli ubahili ni moja ya mbinu za kuwa tajiri??kama kweli kwanin na nivip??

ni kweli ni moja kati siri ambayo itakufanya kuwa tajiri.

Unapotengeza biashara yako unatakiwa kuwa na heshima kubwa sana katika matumizi yako ya pesa.
chukua mfano una mradi ambao umepanga kila siku utakuwa unaingiza tsh 200,
ikatokea kwamba unatakiwa utoe mchango wa harusi wa tsh70 . lazima ufanye ubahili ili kuokoa malengo yako.

ubahili huo unatokana na kuheshimu melengo ulijiwekea.

asante sana kwa swali lako,
 
Nimeshagaa sana kukutana na swali kama hili kwa mtu anayejiita great thinker

swali ambalo unaweza hata jibu lake kulipata hata kwenye kamusi.

Tajiri ni mtu anayemiliki vitu vya thamani, pesa, majumba biashara mbalimbali. pamoja na kuwa ni vyazo vingi vya mapato,.


Na mimi nimeshangaa sana! Kuona mtu uliyejitolea kutoa elimu ukashanazwa na swali lililopo ndani ya mada husika!

Very interesting....
 
Hujanijibu swal langu

hii ni kutokana na kuheshimu malengo ulijiwekea katika mradi wako,

mfano,, umejiwekea kwamba utakuwa unaingiza kipato cha tsh200, ukatokea mchango wa harusi wa tsh70 unatakiwa ufanye ubahili ili kuokoa pato lako kwa siku.

ubahili ni kuheshimu mikakati uliyojiwekea katika mradi.
 
Na mimi nimeshangaa sana! Kuona mtu uliyejitolea kutoa elimu ukashanazwa na swali lililopo ndani ya mada husika!

Very interesting....

Igekuwa vyema sana kama ungeuliza swali!

na swali ngani ambalo limenikamba,?
 
We una utajiri gani, isiwe tunamezeshana theory tu...
Una roadsters ngapi, ile rolls loyce ulinunua pesa ngapi, umeikopesha serikali mara ngapi, umetoa misaada mara ngapi, hata JF umeshindwa kuwa golden member...
 
Je nikiwa na laki moja nifanye biashara gani ili niwe tajiri?
 
Vp kuhusu uchawi katika kupata utajiri!

Unapozugumizia uchawi haya ni maswala ya iman zaidi,

ni sawa na mtu wa dini kumuomba mungu wake amusaidie kuwa tajiri.

na wewe pia unaweza ukaamini chochote kitakachokufanya kuwa tajiri.
 
naomba mbinu za kuwa tajiri

Una umri gani mkuu, je unasoma au hausomi.?
Una kipaji chochote au utalamu fulan?

naomba unijibu maswali hayo ili nipate pakuanzia
 
We una utajiri gani, isiwe tunamezeshana theory tu...
Una roadsters ngapi, ile rolls loyce ulinunua pesa ngapi, umeikopesha serikali mara ngapi, umetoa misaada mara ngapi, hata JF umeshindwa kuwa golden member...

Nina mipango ya kuyakamilisha hayo yote nikifikisha miaka 50,

asante kwa swali lako.
 
Back
Top Bottom