Niulize kuhusu fursa ya masomo Sweden

Niulize kuhusu fursa ya masomo Sweden

Nauli unajitegemea mpaka kufika. Ukishafika unarudishiwa gharama zako za nauli.
Nashukuru sana mkuu!!

1. Hapa Tz ukiwa na buku tano unatoboa siku, je huko gharama za maisha zikoje? roughly kwa matumizi ya chakula inaweza cost ngapi kwa siku?

2. Je account unafungulia huko huko kwao au ni hizi zetu?
 
Huwezi ukadanganya kama hauna leadership experience...sijawahi kuwa kiongozi.
Wabongo huwa hawashindwi kitu. Ila mkuu, leadership experience siyo mpaka uwe manager au CEO au Mkurugenzi. Hata kama una NGO au Community organization yoyote iliyosajiliwa na kutambulika hata kama ni kijijini kwenu, na ukawa unaongoza kufanya activity yoyote katika majukumu yako, tayari hiyo ni leadership experience. Bila shaka umenipata mkuu.
 
Nashukuru sana mkuu!!

1. Hapa Tz ukiwa na buku tano unatoboa siku, je huko gharama za maisha zikoje? roughly kwa matumizi ya chakula inaweza cost ngapi kwa siku?

Mkuu, Sweden ni miongoni mwa nchi ambazo kuna gharama kubwa sana za maisha. Kwa mfano chakula mgahawani kwa fedha ya kibongo ni kuanzia TZS 15,000 - 23,000. Hicho ni chakula cha kawaida kabisa. Hata chips kuku tu ni kuanzia 20,000 na kuendelea. Kunyoa Barbershop ya kawaida kabisa ni TZS 60,000. Kiufupi gharama za maisha zipo juu. Ila itoshe kusema kwamba fedha unayopewa inatosha kukidhi mahitaji yote na ukiishi vizuri unabakiza chenji kidogo.

2. Je account unafungulia huko huko kwao au ni hizi zetu?
Wenzetu mambo yao yapo systematic na well organized hakuna ubabaishaji wowote. Unakuta wamekuandalia account na pesa ipo tayari, inabakia kufanya activation tu ambayo ni ndani ya 24- 36 hours inakuwa tayari na unaanza kutumia mpunga wako.
 
Wabongo huwa hawashindwi kitu. Ila mkuu, leadership experience siyo mpaka uwe manager au CEO au Mkurugenzi. Hata kama una NGO au Community organization yoyote iliyosajiliwa na kutambulika hata kama ni kijijini kwenu, na ukawa unaongoza kufanya activity yoyote katika majukumu yako, tayari hiyo ni leadership experience. Bila shaka umenipata mkuu.
Nimekupata vizuri mkuu. Naomba nikutafute inbox nikianza kuapply. Shukrani.
 
Wakuu, imekuwa ni adimu sana kuona Wabongo tukishikana mikono ili kuvuka hatua moja kwenda nyingine yenye mafanikio. Tumezoea kupambana wenyewe na wengi wetu huwa hatupo wazi inapokuja suala la kumueleza mtu mwingine juu ya fursa fulani, tunapenda kuwa wabinafsi na wachoyo.

Kauli hii nimeithibitisha baada ya kutembelea nchi za wenzetu walioendelea (Ulaya) na kuona namna ambavyo Waafrika kutoka magharibi wanavyochangamkia fursa za hapa na pale na namna wanavyoshikana mikono ili kuvuka mahala.

Ni kwa mantiki hiyo basi, ili kuvunja kasumba ya ubinafsi wetu Wabongo, nipo hapa kujibu maswali juu ya fursa ya kimasomo unayoweza kuipata Sweden kwa ngazi ya Shahada ya Uzamili (Masters Scholarship).

Sio masuala ya kuja inbox, wewe uliza hapa hapa public nitakujibu. Sihitaji mtu kuja kunifuata inbox.

Karibuni.
Nakupongeza sana ,
Watanzania tumekuwa watu wakubaniana fursa ni ukweli usiopingia asilimia kubwa ya Watanzania hawapo tayari kuwashika mkono wenzao .
Mtu yupo radhi fursa impite kuliko kumuunganishia mwingine.
Naweza sema imekuwa sababu ya umaskini wetu.
Wenzetu waarabu, wachina na hata wanaigeria wanasupport kubwa kwa jamii yao.
Hii imesababisha hata mtu akitoa fursa anaonekeana mpigaji.

Anyway makofi kidogo kwa mtoa mada.
Kama upo mbele chukua pepsi barid ulipe mwenyewe .jokes

Sent using Jamii Forums mobile app
vp kwa master ilikuwa na uakika wa full funded masters scholarship unatakiwa uwe angalau na GPA ya ngap?
 
vp kwa master ilikuwa na uakika wa full funded masters scholarship unatakiwa uwe angalau na GPA ya ngap?
Sijawahi kuona wakitaja GPA kama kigezo. Japokuwa nadhani ukiwa na atleast Upper second unakuwa kwenye chance nzuri zaidi. Wenzetu hawaangalii sana ufaulu wa kwenye makaratasi. Wanangalia uwezo wa mtu. Hata hivyo kufaulu vizuri ni added advantage.
 
Nadhani TOEFL na IELTS inategemea na chuo bila kujali national language, kuna vyuo vinahitaji hiyo na kuna baadhi ya vyuo havihitaji
TOEFL na IELTS sanasana ni kwa nchi ambazo their first language is English kama vile UK, US, CANADA, Australia n.k

Kwahiyo kwa nchi za Ulaya kama vile Scandinavian (Sweden, Finland, Norway, Denmark) na nchi nyingine za Ulaya kama Austria, France, Germany na Netherlands ambako lugha yao ya kwanza siyo English, hizo mambo za IELTS na TOEFL kwa uzoefu wangu, kwa kiasi kikubwa sijaona wakiomba uwe umefanya hiyo mitihani.

Hivyo, kwa jibu fupi, ili usome Sweden kwa sisi Wabongo ambao tunatumia English kuanzia Sekondari hadi Chuo Kikuu, tunahitajika kuwa tumefaulu English O-level. Hicho ndicho kigezo pekee ninachokifahamu.

Katika swali lako la pili; nchi zilizoendelea(Ulaya) wanathamini sana Utamadumi wao; hivyo lugha ya mawasiliano ni lugha yao. Kwa Sweden wanatumia Kiswidi(Swedish). Hata hivyo; karibia 85% ya Waswid wanazungumza English vizuri kabisa. Ukipata Scholarship, lugha ya kufundishia kwa Masters ni English.

Suala la Ubaguzi naomba nilisizungumzie sana; binafsi sijawahi kukutana na changamoto hii. Sweden na Nchi nyingi za Scandinavian wanajitahidi sana kuthamini utu wa kila MTU. Ila siku zote, mweusi ni mweusi na Mzungu ni Mzungu tu. Japo hutaona Ubaguzi kwa kusikia wala kwa macho, ila kiasili mweupe ni mweupe na mweusi ni mweusi tu.

Generally, nchi nyingi za Ulaya kwa sasa Ubaguzi siyo agenda kubwa. Sanasana labda Ubaguzi utausikia kwa Wazee na Watoto. Ila vijana wamestaarabika. Mwisho kabisa, kwa mtizamo wangu, nadhani Sweden ni miongoni mwa nchi zenye kiwango cha juu cha ustaarabu Duniani.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nadhani TOEFL na IELTS inategemea na chuo bila kujali national language, kuna vyuo vinahitaji hiyo na kuna baadhi ya vyuo havihitaji

Sent using Jamii Forums mobile app
Unajua mkuu mie nili-Generalize kwa sababu nilipata fursa Sweden sikuhitajika kuonesha TOEFL/IELTS certfificate. Hali kadhalika Netherlands pia sikuulizwa, na kwenyewe hawakuhitaji. kuna jamaa yangu kasoma German na yeye anasema hawahitaji. Jamaa zangu wengine kama 10 hivi wanasoma vyuo mbalimbali Sweden na wao hawajawahi kuulizwa hilo. Basi nikawa nime-Generalize, kumbe kuna vyuo specific hata Sweden wanahitaji? Sikujua hili.
 
Mambo ya wenzetu yamenyooka hayana kupindisha. Nyeupe ni nyeupe na nyeusi ni nyeusi with no excuses! Hivyo mambo yalienda smoothly kwa kuwa nilikuwa nikifanya kila kinachohitajika kwa wakati wake kwa kufuata maelekezo.

Changamoto kidogo sana ilikuwa kuambatanisha Passport maana wakati naomba niliweka National ID kwa sababu nilikuwa sijapata Passport. Waliponiuliza nikawaambia nitawatumia ndani ya muda mfupi na nikataja lini itakuwa tayari. Mungu ni mwema nikafanikiwa kuipata na kuituma kama nilivyoahidi.

Requirements zipo nimeambatanisha kwenye link kwenye posts zilizotangulia. Ila kwa ufupi, requirement kubwa ni uwe na experience ya kazi at least 2 -3 years. Na uwe na Leadership experience pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ulipataje passport kabla hujapewa joining instructions maana uhamiaji wanataka invitation letter ili upewe passport.Kingine,kuna fursa za kupiga box ili ukirudi bongo uje na mtaji kama ilivyo marekani na Ulaya magharibi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulipataje passport kabla hujapewa joining instructions maana uhamiaji wanataka invitation letter ili upewe passport.Kingine,kuna fursa za kupiga box ili ukirudi bongo uje na mtaji kama ilivyo marekani na Ulaya magharibi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Passport nilipata kwa sababu nilikuwa na admission letter ya kutoka chuo cha Nchi nyingine ya Ulaya nilikuwa nimepata kabla ya kupata admission ya Sweden.

Fursa za kupiga box zipo mkuu, ni bidii yako tu kama utaweza kuhimili masomo na kazi. Tofauti na mitizamo ya watu wengi, shule ya Ulaya hasa niseme Sweden ambako nina uzoefu nako siyo ya kula bata kama wanavyosema watu. You really have to study very hard to survive. Ila hili pia libaki kwa mtu mwenyewe, maana uwezo wa mtu na mtu pia hutofautiana. Mie naweza kutumia muda mwingi kusoma ili ni-survive, at the same time mtu mwingine kwa sababu ya uwezo labda alionao akatumia nguvu kidogo tu na akatoboa. Ila kwa ujumla shule siyo bata kama wasemavyo. Ni shule shule kweli.

Ukiwa na mpango wa kazi za box Sweden unaweza kufanya maandalizi mapema ya kujifunza Kiswid taratibu maana wanatumia lugha yao kwa kila kitu almost 99.99%. Kitu kingine, ukiwa unafahamu kuendesha gari na una leseni ni added advantage. Japokuwa leseni yetu ya Bongo kwa Ulaya haitambuliki, ila angalau hata ukienda kufundishwa kupata leseni yao angalu hautatumia nguvu kubwa sana.
 
Sorry nikimaliza first degree ni lazima nipate KAZI Kwanza na nifanye Kwa muda kidogo ndo niombe scholarship?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni rahisi mtu mwenye uzoefu wa kazi kuchukuliwa kuliko amabye hana,hata hivyo kama hujapata bado ajira but ufaulo wako upo vizuri napo ni rahisi kuchukuliwa.
 
Passport nilipata kwa sababu nilikuwa na admission letter ya kutoka chuo cha Nchi nyingine ya Ulaya nilikuwa nimepata kabla ya kupata admission ya Sweden.

Fursa za kupiga box zipo mkuu, ni bidii yako tu kama utaweza kuhimili masomo na kazi. Tofauti na mitizamo ya watu wengi, shule ya Ulaya hasa niseme Sweden ambako nina uzoefu nako siyo ya kula bata kama wanavyosema watu. You really have to study very hard to survive. Ila hili pia libaki kwa mtu mwenyewe, maana uwezo wa mtu na mtu pia hutofautiana. Mie naweza kutumia muda mwingi kusoma ili ni-survive, at the same time mtu mwingine kwa sababu ya uwezo labda alionao akatumia nguvu kidogo tu na akatoboa. Ila kwa ujumla shule siyo bata kama wasemavyo. Ni shule shule kweli.

Ukiwa na mpango wa kazi za box Sweden unaweza kufanya maandalizi mapema ya kujifunza Kiswid taratibu maana wanatumia lugha yao kwa kila kitu almost 99.99%. Kitu kingine, ukiwa unafahamu kuendesha gari na una leseni ni added advantage. Japokuwa leseni yetu ya Bongo kwa Ulaya haitambuliki, ila angalau hata ukienda kufundishwa kupata leseni yao angalu hautatumia nguvu kubwa sana.
Asante sana kwa majibu mazuri. Kwenye ishu ya passport tunakwama sana hapo. Kama hutojali ungetupa mbinu za kuipata.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sana kwa majibu mazuri. Kwenye ishu ya passport tunakwama sana hapo. Kama hutojali ungetupa mbinu za kuipata.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbinu muhimu ni kumuomba sana Mungu akujalie ili kila utakachozungumza pale Uhamiaji kiwe na kibali kwao na ufanikiwe. Hiyo ni mbinu muhimu niliyoitumia na nikaona matokeo yake.
 
Nchi zipi huko watu wake wanapewa kipaumbele zaidi kupata scholarships?
Wakuu, imekuwa ni adimu sana kuona Wabongo tukishikana mikono ili kuvuka hatua moja kwenda nyingine yenye mafanikio. Tumezoea kupambana wenyewe na wengi wetu huwa hatupo wazi inapokuja suala la kumueleza mtu mwingine juu ya fursa fulani, tunapenda kuwa wabinafsi na wachoyo.

Kauli hii nimeithibitisha baada ya kutembelea nchi za wenzetu walioendelea (Ulaya) na kuona namna ambavyo Waafrika kutoka magharibi wanavyochangamkia fursa za hapa na pale na namna wanavyoshikana mikono ili kuvuka mahala.

Ni kwa mantiki hiyo basi, ili kuvunja kasumba ya ubinafsi wetu Wabongo, nipo hapa kujibu maswali juu ya fursa ya kimasomo unayoweza kuipata Sweden kwa ngazi ya Shahada ya Uzamili (Masters Scholarship).

Sio masuala ya kuja inbox, wewe uliza hapa hapa public nitakujibu. Sihitaji mtu kuja kunifuata inbox.

Karibuni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom