Wadau natumaini mnaendea na harakati za maisha kama kawaida.
Wanasema binadamu tunajifunza kila siku, nakubali bila ya kinyongo. Kwani ni Jambo Jema kwa binadamu kujifunza, tunapunguza ujinga na kuongeza maarifa.
Mdau kaja na wazo zuri mimelipenda, Ila nina wasiwasi kuna vitu vitamshinda kwani hakuna anayejua kila kitu humu duniani.
Unaposema "uliza chochote nitakujibu" bila Shaka unamaanisha una majibu ya kila kitu!
Hatutegemei utupe Majibu yatakayotuachia maswali au yasio jitosheleza. Vinginevyo una lengo la kuwapotezea watu muda.
baadhi ya watu wameanza kuuliza maswali ya kukujaribu au yasiyo na maana! Hii inaonyesha Wazo lako ni zuri Ila lina utata.
NAFIKIRI INGEKUWA VIZURI KAMA UNGESEMA TUKUULIZE SWALI LOLOTE KWENYE KITU ULICHOBOBEA.
Maswali ya kizushi:
1. Hivi baharini kuna samaki wengi kiasi gani?
2. Tumeambiwa yesu atarudi siku za mwisho, je ni siku na tarehe gani?
3. Maandiko mengi yanamrifaa mungu kama mwanaume! Je inawezekana akawa ni mwanamke? Nani alimuona?
4. Je wewe utakufa siku na tarehe gani?
5. Hivi karibuni kumekuwa na mfululizo wa matukio ya uvamizi na watu kutekwa, huko isti afrika! Je ni nani anafanya hayo mambo?
Asante.