Niwe mmoja wa WanaJF mwenye nyumba kali

Niwe mmoja wa WanaJF mwenye nyumba kali

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Screenshot_20230513-122108_Gallery.jpg

Screenshot_20230513-122156_Gallery.jpg


Wakuu nataka kuwa moja kati ya wanaJF wenye nyumba kali. Hii ni idea ya kunipeleka huko. Hii ndio nyumba ya kudumu ya mkuu wenu itakayowekwa kwenye kiwanja cha mita za mraba 2,000. Inatakiwa kuwa nyumba kali kushinda zote pale. Iwe kali mpaka watu waseme nimejiunga Freemason, wazushe humo ndani nimevuga majoka. Kisha mimi niseme ni kwa neema tu za Bwana.

Nyumba inatakiwa kuwa bangaloo. Hizo picha mbili zinatakiwa ziungwe (merged) ili kuwa plan moja kali sana.

Pamoja na kuwa itakuwa ni single storey, sio ghorofa lakini inatakiwa kuwa ile upper canopy ya juu kwa ajili kutulia pale juu na kula mema ya nchi. Itafanyikaje,mimi sijui mafundi ndio wanajua.

Fundi mwenye uwezo wa kuweka hizo ideas kwenye ramani moja anakaribishwa tufanye biashara. Wakuu wa kutoa kasoro mnakaribishwa sana ili niweze kuwawakilisha wana Jukwaa la Ujenzi
 
Wewe jenga nyumba yako, usiweke mawazo ya "itakuwa kali kuliko zote", hayo ni mawazo ya "masikini akipata".

Usichokijua ni kwamba, wakati unamalizia nyumba yako, possibility ya kuwepo ujenzi wa nyumba nyingine kali zaidi ni mkubwa coz kila siku watu wanakuja na designs nzuri kuliko za jana na juzi.

Kila la heri, ni pesa za kutosha hapo zinahitajika.
 
Wewe jenga nyumba yako, usiweke mawazo ya "itakuwa kali kuliko zote", hayo ni mawazo ya "masikini akipata".

Usichokijua ni kwamba, wakati unamalizia nyumba yako, possibility ya kuwepo ujenzi wa nyumba nyingine kali zaidi ni mkubwa coz kila siku watu wanakuja na designs nzuri kuliko za jana na juzi.

Kila la heri, ni pesa za kutosha hapo zinahitajika.
Hizo ni swags tu zisikupe taabu sana, maana wengine hamna dogo. Mada hapa ni hiyo design
 
Kwa hiyo niandae bei gani mkuu. Eneo ni tambalale, halafu nina mitambo ya kupunguza gharama za mchanga na kokoto
Nafikiri kuanzia 70m
Na kama umri umesogea, nyumba ya chini kubwa ni nzuri zaidi

Ili usije kuhangaika kupanda na kushuka
Uzee na gorofa hapana
Maana baadae utalazimika uwe unaishia chini tu [emoji1]
 
Hizo ni swags tu zisikupe taabu sana, maana wengine hamna dogo. Mada hapa ni hiyo design
It's a standard house design, kwangu siongezi wala kupunguza kitu. Siku hizi kuna maswali kwa nini kuna public toilets karibu na sitting rooms, imekuwa kawaida.

Hapo kazi ni kupata boq ili ujue kwa design hiyo, mazingira yako, mfuko wako na factors zingine utaweza kuupandisha?

Ila kwa standard ya hiyo ramani, kama ni mjini Dar, inaweza kupita 50m na zaidi.
 
Nafikiri kuanzia 70m
Na kama umri umesogea, nyumba ya chini kubwa ni nzuri zaidi

Ili usije kuhangaika kupanda na kushuka
Uzee na gorofa hapana
Maana baadae utalazimika uwe unaishia chini tu [emoji1]
Mkuu nimefafanua hii ni single storey sio gorofa. Hiyo gorofa hapo juu nataka kutumia upper canopy yake tu na design ya finishing.
 
Gharama za Ujenzi kwa nyumba hiyo haitapungua milioni 180 hadi finishing.

Ukiweza andaa Kitabu kwaajili ya kunakiri matumizi yote utakayotumia site


Kila la kheri Mkuu
Nilitaka kuandika kiwango kikubwa cha gharama nikaona mmh, kuna siku nilichambwa kuhusu hizi gharama. Watu wakasema kwa design ile 30m ingetosha, nikakaa kimya.

Kwa design hiyo(though hajaweka vipimo) hakika gharama sio haba.
 
Back
Top Bottom