Niyonzima atua Dar, sasa yuko tayari kuanza kazi na kikosi cha Simba SC

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253


Kiungo Haruna Niyonzima ametua Dar usiku na taarifa za ndani zinasema baadhi ya mashabiki wa Yanga walikuwa wanamsubiria kumfanyia vurugu. Jamaa unaambiwa aliwakwepa na kuwaacha kwenye mataa.

Niyonzima sasa yuko tayari kujiunga na kikosi baada ya kuwasili usiku.
Niyonzima ambaye aliendelea kubaki kwao Kigali amewasili na kupokelewa na viongozi wa Msimbazi tayari kuanza kazi.

Nguvu zote zinaelekezwa kwa Simba ni kesho kwenye Tamasha la Simba Day wakati atakapotambulishwa rasmi.
 
Wacha kichaa...mashabiki wa Yanga na ustaarabu wao si wa kufanya vurugu za kipumbavu.
 
Ukiiangalia sura yake inaonekana kujaa Hofu....

sijui anaogopa kupata kipigokutoka kwa mashabiki wa Yanga? Lol
 
Sasa Niyonzima ndo anaweza akatakiwa na timu za ulaya, yuko eneo sahihi! Hajachelewa, yanga wamempotezea sana muda.
 
Reactions: PNC
Umeona ehhh? Amejaa hofu moyoni mwake. Kama utakuwa umewahi kusoma psychology utagundua kwanini Jamaa amebeba mtoto akiwasili Airport.
Kabeba mtoto kama kinga, si umeambiwa mishabiki ya yanga ilienda kuleta fujo? Wee uliluwapo pia bila shaka.
Hivi anaondoka msuva alafu unaleta ngassa, kweli!
Na huwezi jua, msuva asilimia kubwa halinya hewa ikikaa vibaya huko anakuja simba, huku ndo utakuwa mlango wake wa kwenda ulaya.
 
Reactions: PNC
Baadhi ya washabiki wa Yanga fc hawana uvumilivu, wangeweza kumfanyanjia fujo kabisa.
Kuna siku niliwakuta mtaani wakichoma jezi za Niyonzima.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Karibu fundi Niyonzima, usiogope cheza mpira kwa bidii yako yote.
Wao wamemchukua Ajibu, sisi tumekupata wewe.
 
Baadhi ya washabiki wa Yanga fc hawana uvumilivu, wangeweza kumfanyanjia fujo kabisa.
Kuna siku niliwakuta mtaani wakichoma jezi za Niyonzima.



Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu umenena vyema kwa kusema 'baadhi ya washabiki wa Yanga' maana siyo wote.

Nawaomba kama kuna mashabiki wenzangu wa Yanga wanafikiria kumfanyia fujo Niyonzima waache tafadhali. Mchezaji anafanya biashara ya mpira. Mguu wake ndiyo chanzo cha mapato yake. Tumuache Niyonzima acheze kwa watani zenu. Hata Okwi aliwahi kucheza Jangwani japo upande wa pili walinuna lakini hawakumfanyia vurugu. Mchezaji si mwanachama wa Klabu, sisi tubaki na Klabu yetu, mchezaji yeyote anayetaka kuondoka Yanga apewe haki hiyo.

Niyonzima amefanya uamuzi wake ambao umetokana na haki ya binadamu yeyote kufanya uamuzi. Yanga ilianzishwa miaka mingi bila Niyonzima na timu iliendelea kutesa tu uwanjani. Tunamshukuru kipindi chake Yanga imeendelea kutesa tu uwanjani na hata bila yeye Yanga itaendelea kutesa tu.

Kabla Niyonzima hajakuwepo, Yanga ipo. Chonde chonde wana Yanga wenzangu, tuachaneni na Niyonzima, ashindwe mwenyewe tu kucheza mpira.

Kila la heri Haruna Niyonzima, asante sana kwa huduma yako ya miaka 6 Jangwani.

Tutakukumbuka kama 'mhenga' uliyekuwepo uwanjani wakati tunachapwa 5-0.
 
ha ha haa.... nimecheka sana..kama mashabiki wa simba na yanga wangekuwa kama wewe watanzania tungekuwa na siku nying sana za kuishi hasa sisi wanaspoti..umeongea kama mwanamichezo na kama mtani pia hasa kwa ujumbe wako wa mwisho nimeupenda sana.. ni kweli mpira si mapenzi.. ni kazi ile anayefanya mpira mapenzi utamwona anavyohangaika na una mfano mzuri wa ngasa ...

wacha watu wapige kazi na maisha ni popote. yanga ipo kabala ya niyonzima na itaendelea kuwepo.
 
Sasa Niyonzima ndo anaweza akatakiwa na timu za ulaya, yuko eneo sahihi! Hajachelewa, yanga wamempotezea sana muda.
Kama alijua anapotezewa muda si angeshaondoka siku zooote
 
Sikuwahi kufikiria kama mashabiki wa Yanga hawana akili kabisa, ndio maana hii klabu inahusishwa na CCM. Niyonzima sio mama yako mwache atafute maisha
 
Nashangaa sana Simba kujinasibu na Ulaya..Yanga wamemtoa Nonda shabani hadi kucheza Monaco..huyo Samatta anacheza ligi ndogo sana Ulaya..akiweza kucheza.England.Italy.Spain.Germany na France rudini hapa mjisifie..kitimu chenyewe Genk kinatoka pembezoni kama kigoma ..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…