Njaa kali klabuni na kutoheshimu 'utaalam wa kiufundi' wasababisha wachezaji muhimu wa Yanga SC kupata majeraha makubwa

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Tukiwa tunawaambieni kuwa mna njaa halafu hamna 'wataalam' wa mpira katika klabu yenu ya Yanga muwe mnatuelewa kwani ni aina yenu ya 'ubishi' ndiyo ambayo imekuwa 'ikiwagharimu' na hatimaye mnajikuta mnafanya vibaya katika mechi zenu mbalimbali kisha mnadai Simba SC inabebwa wakati si kweli.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida kabisa huku wakijua kuwa Jumapili ijayo tarehe 27/10/2019 wana mechi ngumu na muhimu sana ya kimataifa, leo klabu ya Yanga imepata 'pigo' kubwa baada ya mchezaji wao ambaye ni mshambuliaji mzuri na 'tegemeo' Kalengo kuumia vibaya wakati Yanga ikicheza mechi ( isiyokuwa rasmi ) na klabu ya Pamba, hivyo kupelekea mchezaji huyo ambaye ni hivi juzi tu ametoka kuwa 'majeruhi' kurejea tena huko huko ambako sasa atakaa nje kwa wiki kati ya 8 hadi 12.

Na inasemekana moja ya sababu kubwa iliyopelekea Yanga SC leo kucheza hiyo mechi (isiyokuwa rasmi ) ni kupata pesa kidogo za kununua chai, vitafunwa na vyakula kwa wachezaji wao huku hela nyingine ikitumika kwa kukodi gari la kunyonya 'kinyesi' katika hoteli waliyofikia hapo mkoani Mwanza ambayo huwa yanajaa kwa haraka kwani hali ya maisha hapo kambini 'kiuchumi' ni mbaya sana.

Yaani una Mechi 'ngumu' na 'Mwarabu' kutoka nchini Misri, Pyramids, badala ya kuwalinda ' wachezaji wako ili wasipate majeraha kuelekea huo mchezo wewe unaendekeza njaa njaa zako kwa kucheza mechi za 'ndondo' ambazo hata kocha mkuu hakutaka ila mmelazimisha tu kwa 'ubabe' wenu kama viongozi na sasa mumempoteza mchezaji wenu muhimu ambaye nina uhakika angekuwepo Jumapili angalau angeweza kuwabebeni na mkabahatisha kushinda.

Ila habari za chinichini zinadai kwamba huyu mchezaji Kalengo anaumizwa 'kiuchawi/ kindumba' na mshambuliaji Mkongo wa Yanga SC, David Molinga, na kwamba hili hata viongozi waandamizi baadhi wanalijua ila wamegawanyika katika kulikabili na kulitatua kwa haraka. Na si kwa huyu tu, bali pia kuna malalamiko hasa kwa wachezaji wa kigeni kuwa hapo Yanga 'wanaumizana' mno kiushirikina, hali ambayo inaweza ikaathiri mwenendo mzima wa klabu/ timu.
 
Mkuu umenichekesha sana, yaani wanaingia gharama ya kupata majeruhi kisa kupata angalau hela ya chai! Mbona kuna mahali nimesoma kila baada ya mechi wachezaji wanakunja kibindoni 10M.
 
Reactions: Lee
Mkuu umenichekesha sana yaani wanaingia gharama ya kupata majeruhi kiss kupata angalau hela ya chai!mbona kuna mahali.nimesoma kila baada ya mechi wachezaji wanakunja kibindoni 10M.
Huyo ni Mbumbumbu hana akili. Match na Pamba imechezwa leo asubuhi kwa ushauri wa benchi la ufundi. Embu muulize match asubuhi tena siku ya kazi mashabiki wanatoka wapi na kubwa zaidi match ilikuwa closed doors bila mashabiki.
 
Mkuu umenichekesha sana yaani wanaingia gharama ya kupata majeruhi kiss kupata angalau hela ya chai!mbona kuna mahali.nimesoma kila baada ya mechi wachezaji wanakunja kibindoni 10M.

Kakudanganya nani Mkuu? Yanga SC wangekuwa na hela (utajiri) leo wangecheza hiyo 'ndondo' ambayo 'imewagharimu' kwa mshambuliaji wao muhimu Kalengo 'kuumia' vibaya hivyo? Na hata hapo hotelini walipopanga, shimo la choo ambalo linajaa sana ni lile la upande vilipo vyumba anamokaa kocha wao mkuu Zahera na cha mchezaji wao David Molinga.
 
Huyo ni Mbumbumbu hana akili,matcha na Pamba imechezwa leo asubuhi kwa ushauri wa benchi la ufundi. Embu muulize match asubuhi tena siku ya kazi Mashabiki wanatoka wapi na Kubwa zaidi match ilikuwa closed doors bila Mashabiki.

Leo Pamba FC wamewaokoa sana kwani hata hela ya 'vitafunwa' mulikuwa hamna. Na hivi michezaji yenu ni 'miroho' mno, leo mngewakoma na si ajabu hata wangegoma kucheza mechi yenu ya Pyramids na wangecheza viongozi wenu watupu tu, Msolla na mwenzake 'Chibonge' Mwakalebela.
 
Huyo ni Mbumbumbu hana akili,matcha na Pamba imechezwa leo asubuhi kwa ushauri wa benchi la ufundi. Embu muulize match asubuhi tena siku ya kazi Mashabiki wanatoka wapi na Kubwa zaidi match ilikuwa closed doors bila Mashabiki.
Mkuu kuna ujinga mwingine umepita level za umbumbumbu
 
Unaweza ukawa una hoja ya msingi kwa mfano hiyo ya viongozi na benchi la ufundi kuamua kuruhusu wachezaji kucheza hiyo mechi ya kirafiki na wakati ni jana tu walitoka kucheza mchezo wa ligi kuu.

Hivyo sisi mashabiki tulitegemea kwa huu muda uliobaki, timu kujikita zaidi katika mazoezi ya kimbinu kwa ajili ya kuwakabili hao Waarabu. Ila kwa makusudi kabisa au kwa bahati mbaya, ukaamua kuileta hii hoja yako kishabiki, kimbumbumbu na kipopoma zaidi.
 
Waliocheza leo ni wale ambao jana hawakucheza kabisa pamoja na wale walioingia Uwanjani kama sub
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Ni vema tukawa tunawatamkia vizuri wale tunaowaongoza.Aden Rage aliposema mashabiki wa simba ni mbumbumbu,na Mo Dewji akasema mashabiki wa simba ni wake zake hakika haya maneno yaliumba.
Ni nani asiyejua kuwa mashabiki wengi wa simba ni mapopoma na mbumbumbu?Angalia hata watu maarufu wanaoshabikia simba utaona wengi wana umbumbumbu fulani hivi.

Mtoa mada anaonekana amebanwa na mkojo na haja kubwa kwa mpigo na ikiwa Yanga itashinda jumapili basi ni wazi tujiandae kupata mrejesho huko Bugando maana mashabiki wa simba ndio wanaoongoza kuzimia.Kuna mechi 2014 tulichapa2-0 walizimia mashabiki wa simba zaidi ya 10.Sasa hawa ikibidi wasiruhusiwe kuangalia hii mechi kwa sababu za kiusalama wa afya zao
 
kalengo kavunjika mguu hadharani kila mtu anaona hajarogwa na mtu yoyote yule
 
kalengo kavunjika mguu hadharani kila mtu anaona hajarogwa na mtu yoyote yule

Kuumia Kwake huko kunatokana na ' Kurogwa ' na Mshambuliaji ' Mchawi ' wa Kikongo David Molinga na haya ' malalamiko ' yako mengi mno hapo Klabuni Yanga labda Wewe tu ' Popoma ' ndiyo huna taarifa.
 
Gilles Muroto - mashabiki mandazi wa Mikia watapata tabu sana kwa sababu ya umbumbumbu wao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…