Pre GE2025 Njaa ni mbaya sana: Mbunge amepitishwa, madiwani watasubiri taratibu za kiserikali!

Pre GE2025 Njaa ni mbaya sana: Mbunge amepitishwa, madiwani watasubiri taratibu za kiserikali!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

peno hasegawa

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2016
Posts
14,255
Reaction score
23,949
Madiwani Jimbo la Hai wameliwa vichwa na UVCCM, baada ya Mbunge wao kuwezesha UVCCM kupata posho kufanya kikao cha Baraza.

Madiwani sasa katafuteni mbunge wenu mwingine, mliye naye amewapiga kona.

 
Acha 'wachezeshane' wao kwa wao, wanajuana. Mama yao yupo 'hai' sema baba ndo kafa kiutata
 
Kuna umuhimu wa mbunge wa Jimbo la Hai, kufanya ziara katika maeneo ya vijana ndani yaJimbo lake,badala ya kuita kikundi cha vijana waliochoka kimaisha na kuwapa posho na kurudi makwao kusumbua wazazi wao:

1. Kuelewa changamoto halisi: Kwa kuzuru maeneo ya vijana moja kwa moja, mbunge ataweza kuelewa kwa undani changamoto wanazokabiliana nazo kila siku. Hii inaweza kuwa ni changamoto za ajira, elimu, afya, au hata masuala ya kijamii. Kuelewa haya kutasaidia kuundaa mikakati sahihi ya kutatua changamoto hizi.

2. Kubuni suluhisho changamani: Vijana wenyewe wana uelewa mzuri wa changamoto zao na mara nyingi wanaweza kuwa na mawazo bora ya jinsi ya kuzitatua. Kuwa karibu nao na kuwasikiliza itamsaidia mbunge kubuni suluhisho zenye manufaa na zinazofaa.

3. Kujenga uhusiano na ushirikiano: Ziara kama hizi zitajenga uhusiano mzuri kati ya mbunge na vijana. Vijana watahisi kuwa mwakilishi wao anajali na anataka kushirikiana nao. Hii itaongeza ushiriki wa vijana katika masuala ya kijamii na kisiasa.

4. Kuhamasisha ushiriki wa vijana: Kuona mbunge akitembelea maeneo yao na kushiriki nao moja kwa moja, vijana watavutiwa zaidi kushiriki katika shughuli za maendeleo na siasa. Hii itaongeza uwakilishi wao katika ngazi ya jamii na kitaifa.

Kwa ujumla, ziara za mbunge katika maeneo ya vijana ni muhimu sana kwa ajili ya kujenga uhusiano, kuelewa changamoto, kubuni suluhisho, na kuhamasisha ushiriki wa vijana katika maendeleo ya jamii. Hii itasaidia kuimarisha demokrasia na maendeleo.

Uchawa ni marufuku Jimbo la Hai
 
Jimbo la Hai, ambalo ni Jimbo la kimkakati kwa CCM, lina changamoto kubwa sana za kijamii na kimaisha.

Miongoni mwa changamoto zilizopo ni miradi isiyotekelezeka na ahadi ambazo hazitimizwi na mbunge wa Jimbo hilo.

Kwa mfano, ujenzi wa masoko mbalimbali ni ahadi tupu tu.

Kuhusu ujenzi na ukarabati wa jengo la ofisi ya CCM wilaya, wanaccm wamemsukuma mbunge kwa miaka mitano lakini bado hakuangalia jambo hilo.

Zaidi ya hayo, wanaccm wamechangia fedha lakini vifaa vya ujenzi havijulikani vilikwenda wapi.

Leo mbunge anatutaka tumpige tena kura, huku akishindwa kuunda chama na kujenga ofisi ya chama wilaya.

Hakuna vikundi vya vijana, hakuna ajira, hakuna miradi ya vijana, bado anawakataa madiwani na kusema yeye atachaguliwa tena.
 
Mbunge ana pesa,kagawa mpunga kwa kikundi kinachojiita UVCCM ,ili wampigie debe 2025.

Ilamadiwani wote Jimbo nzima ni walala hoi hawana mpunga,wao hawatapigiwa debe watasubiri taratibu za kiserikali.
Njaa ni mbaya sana mkuu
Sometimes bora eneo lichague madiwani wenye hela. Hawa si warahisi kuwayumbisha. Kuliko wale wenye hela. Ukiwa na hela hata kumzidi mbunge unahamisha upepo, uvccm si bendera fuata upepo
 
Jimbo la Hai, ambalo ni Jimbo la kimkakati kwa CCM, lina changamoto kubwa sana za kijamii na kimaisha.

Miongoni mwa changamoto zilizopo ni miradi isiyotekelezeka na ahadi ambazo hazitimizwi na mbunge wa Jimbo hilo.

Kwa mfano, ujenzi wa masoko mbalimbali ni ahadi tupu tu.

Kuhusu ujenzi na ukarabati wa jengo la ofisi ya CCM wilaya, wanaccm wamemsukuma mbunge kwa miaka mitano lakini bado hakuangalia jambo hilo.

Zaidi ya hayo, wanaccm wamechangia fedha lakini vifaa vya ujenzi havijulikani vilikwenda wapi.

Leo mbunge anatutaka tumpige tena kura, huku akishindwa kuunda chama na kujenga ofisi ya chama wilaya.

Hakuna vikundi vya vijana, hakuna ajira, hakuna miradi ya vijana, bado anawakataa madiwani na kusema yeye atachaguliwa tena.
Kama haya hajafanya anatengeza resistance against him
 
Mheshimiwa Mbunge Jimbo la Hai!

Kama mbunge aliyeteuliwa na CCM, ni jukumu lako muhimu kusimamia na kuhakikisha kuwa miradi inayopangwa na chama chako inatekelezwa ipasavyo kwa faida ya wanachama na wananchi wote.

Kuhusu suala la ujenzi wa jengo la utawala la CCM wilaya, ni kweli kwamba umeshindwa kusimamia ujenzi huo licha ya kuteulliwa na chama.

Hali hii inaweza kusababisha wanachama na wananchi kukosa imani na uongozi wako. Ni vyema utaifiche mkutano na viongozi wa CCM wilaya ili kujadili changamoto unazokumbana nazo na kuelezea mikakati yako ya kuhakikisha jengo hilo linajengwa kabla ya uchaguzi mkuu wa 2025.

CCM pia inapaswa kukuangalia kwa undani na kutathmini utekelezaji wa majukumu yako badala ya kukuondoa ubunge kwa sababu ya kushindwa kutimiza ahadi kuhusu ujenzi huo.
Hii itasaidia kuimarisha demokrazia na uwajibikaji ndani ya chama.

Ni muhimu kutatua changamoto hizi kwa ushirikiano na wanachama wenzako ili kuonyesha uongozi imara na kuwajibika kwa wananchi waliokuchagua. Ninatumaini kuwa mtakuwa na mkutano huo na kufanya maamuzi yanayofaa kwa maslahi ya chama na jamii kwa ujumla.

Mheshimiwa, naomba uwape ccm maoni zaidi kuhusu jinsi unavyoweza kushughulikia hili suala kwa ufanisi. Ili kuepuka kukosa kura za maoni ndani ya chama 2025.
 
Haya ndiyo matatizo ya vijana wa Tanzania, hawatumii akili bali wanatanguliza matumbo yao.

Kwa tamko hili wameibaka demokrasia.
 
Back
Top Bottom