Eti mtu ana hela sema kaona uvivu kwenda nunua msosi analalamika njaa.
Ishawahi niuma njaa kama 6 days sili msosi wa kueleweka nikamkuta mshikaji anakula muhindi wa kuchoma njiani (mkoani njombe huko) nikamuomba na akanipa.
Kuna siku nina njaa natembea from ubungo to Mbagala Kongowe nikamkuta jamaa amekaa pembeni ya roli hafu ana maji uhai lita moja kapiga nusu nikamfuata nikamsalimia kistaarabu nikaomba maji akanipa.
Kuna siku nilikuta washikaji wanachimba mtaro wa kupitisha nyaya za internet nadhani mkoani iringa/mafinga sasa wakawa break wanakula ugali na maharage nikaenda nikazuga naomba maji ya kunywa wakasema karibu tuliunge aisee nilikula knm kwasababu uhakika wa kula kesho yake nilikua sina.
Na chuo aisee hahahaa chuo anajua Mungu tu ngoja nikaushe vyuoni kuna siri nyingi sana.