Zanzibar 2020 Njama? Mgombea wa Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Maalim Seif awekewa Pingamizi

Hapo ni sawa kusema pambano la ngumi haliwezi kuisha kwa sababu tu mmoja kapigwa ngumi ya KO kazimia huko, hivo kwanini asitibiwe ili arudi ulingoni aendelee na pambano? Kila mchezo unasheria zake msitegee huruma ya mtu kwenye sheria. Maarimu akipigwa KO mtulie tuu ndo mchezo wenyewe 😄😄
 
Ok lakini kosa lisemwalo linahusu tarehe badala ya 7/9 inadaiwa aliandika 7/7 lakini hakuna kitu kama hicho.

Ningekuwa mimi Maalim, simwachii mtu kufanya kazi hii. Najaza mwenyewe, herufi kwa herufi. Namwachia tu Jaji sehemu yake. TraNsparency imeandikwa Trasparency!
 
Wanatukatisha tamaa wapenda mabadiliko. Yaani chama kizima - Maalim, Zitto, Membe... na wanasheria wao, wameshindwa kabisa kujaza fomu 1 kwa usahihi! Hata transparency wanaandika trasparency? Kama wamekosea hili, kwa nini wasikosee tarehe. Pamoja na kuona yote yaliyotokea kwa wagombea udiwani na ubunge? Kama ni kweli amefanya hayo makosa, Wazanzibar hawatamsamehe kabisa. Ndio maana wengine wanasema ni kuuza mechi.
Ok lakini kosa lisemwalo linahusu tarehe badala ya 7/9 inadaiwa aliandika 7/7 lakini hakuna kitu kama hicho.
 
Chama Ni Cha Upinzani.....
Chama Kina Wanasheria Wengi...

Halafu Wanakosea Jambo La Tarehe?!!!

Nasubiri Utetezi Wao wa "kishawishi" otherwise Nitaendelea Kutowaamini Wengi Wa Wanasiasa Wa Upinzani....

[emoji23][emoji23][emoji23]Babu Seeeefuuu...
Mwambie anayekupumulia ashuke kwanza akili yako ipate utulivu.
 
Wajaribu waone ndio utakuwa mwisho wa Zanzibar
CCM inalazimisha vita kwa udi na uvumba
Wanapima upepo!
Hivi ninyi mnadhani Tanzania ni CHADEMA inayoendeshwa kwa mfano wa SACCOS na mjasirimali wa Kiasa, Mbowe, anayetafuna fedha ya chama mnamwogopa kumwuliza!

Siyo ninyi, wafuasi wa mitandaoni, wala viongozi wa CHADEMA wenye ubavu wa kufanya hicho mnachoota au kuingiza WaTz barabarani, kama anavyohamasisha Lissu, Mgombea wenu wa Urais

Kwa taarifa yenu, baada ya uchaguzi huu, mbivu na mbichi zitajulikana kuhusu matukio ya utekaji na mashambulizi mnayodai Serikali ina mkono wake. Msibadili ID zenu.

Kama Lowassa alishindwa na Magufuli akiwa hana nguvu za kisiasa, akilazimika kupita mitaani kuomba wadhamini, nguvu yake kisiasa sasa ni kubwa, marudufu, kuliko Rais na mwanasiasa yeyote Tanzania.
 
Kuna wagombea ubunge wa ACT waliandika jina la chama kama Maalim hapo "ACT Wazalendo". Wameenguliwa kwa kutokuweka "-" yaani "ACT-Wazalendo". Naona Maalim naye hakuweka hako ka-.
Ukiangalia unaweza kusema ni kitu kidogo ila kisheria ni kosa kubwa sana. Wakikomaa wanaweza kumuengua Maalim Seif. Ukiangalia hata katiba ya ACT imeandikwa ACT-Wazalendo na siyo ACT Wazalendo. Angalia hii screenshot hapa nchini.

 
Naam mkuu. Wewe kama unajua kuwa unawindwa tayari lazima uwe makini. Zaidi ya hilo, fomu tunayoiona hapa ambayo inasemekana ni ya Maalim, imeandika Transparency kuwa ni Trasparency. Chama hiki hakina wanasheria? Wanasheria wameona hii ni sawa tu? Lakini Maalim alitakiwa ajifunze kutoka kwa wagombea wake wa ubunge na udiwani walioenguliwa kwa makosa kama haya.
 
kama kweli una nguvu ya mungu iko ndani yakao tazama namber tatu then tena iangalie kwa makini lipo jibu hutapata , asante mungu kwa uwezo huu unipao , sikutafuti invyotakiwa ipo siku sasa ni lazima nikutafute, sasa basi , nakuhitajia sana
 
Tume wanachoitakia nchi hii watakipata tu pasipo shaka!!
 
Magufuli ana nguvu au wanajeshi ndio wana nguvu
 
Mkuu upo sahihi kabisa. Kisheria Maalim amedhaminiwa na chama kisichokuwepo. Transparency ya ACT-Wazalendo na Trasparency ya ACT Wazalendo zinaleta maana mbili tofauti kabisa. Hivyo ni vyama viwili tofauti kabisa. Nami nashangaa kuona chama kinachopigania kushika dola kinakosa wanasheria wa kuwasaidia katika vitu vidogo kama hivyo. Pengine ndiyo maana wagombea karibu wote walienguliwa. Ndugu Zitto mnatia aibu kama chama kufanya makosa ya kijinga kama haya halafu mnakuja mnalialia kuwa mnafanyiwa hujuma. ACT Wazalendo hebu ajirini wanasheria wanaoijua kazi yao vinzuri ili kusudi siku nyingine msifanye makaosa ya kipuuzi kama haya.
 
Siamini Kama kweli hii fomu ni ya maalim Seif hii, inawezekana imeletwa ili tujadili na tuponde tume kuwa inamuonea na kuonesha kuwa hajakosea lakini kumbe aliye ileta hii fomu amejichanganya Kuna makosa makubwa sana hapo kwenye hiyo fomu ambayo wanasheria wakiyakomalia na busara zisipo tumika basi maalim ataenguliwa kweli.
 
Nadhani busara zitatumika hawata muengua, sidhani kama watakomalia sana Sheria hapo. ( Tusubiri huruma ya Tume)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…