Nje ya Bunge hakuna Katiba ya Wananchi

Nje ya Bunge hakuna Katiba ya Wananchi

Paul Makonda

Member
Joined
Jul 8, 2011
Posts
97
Reaction score
186
Uadui kwa taifa ni pamoja na kunyamaza wakati unajua ukimya wako unaangamiza wengi

Watanzania, Ni siku nyingine tena ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwamba taifa bado ni moja na lina umoja ule tunaoufurahia. Tunayo amani Upendo na Furaha si kwamba vitu hivyo vilishuka kama mvua, kuna watu walifanya kazi, wapo wanaofanya kazi na ili kuendela kuwa navyo sisi sote lazima tufanyie kazi. Uvumilivu wa kisiasa sitaha na ustahimilivu wa yale tunayoona ni maumivu kwetu na tusingependa tuyasikie ndivyo vinavyotufanya tuwe katika utendaji kazi utakaoendeleza tunu hizi za taifa. Si jambo jepesi kuwa na amani, umoja na mshikamano tulio nao. Ni vitu adhimu.

Wiki iliyopita niliandika kuhusu makosa kumi ya Msingi UKAWA wameyafanya kabla na baada ya kutoka nje ya Bunge. Kususia kwa bunge kumetengeneza makosa ya Msingi kwa kuwa yote waliyoyasema waliyasema ndani ya Bunge. Lakini kuna hoja ya kuyafanya makosa yao kuwa ni JINAI kwa sababu kwa wao kutoka nje ya bunge ama wanakwamisha mchakato wa katiba kwa makusudi ama wameamua kupotosha taifa. Wanalihalifu taifa kwa kuwa wanajiaminisha kuwa bila wao hakutakuwa na katiba. Wameshau kuwa kanuni zilizotengenezwa zinawezwa kurekebishwa na kuwezesha mchakato kuendelea bila wao. Uhalifu mkubwa utakuwa na umeonekana pale walipoamua kuanza kutumia maneno waliyyoyazungumza wakiwa na kinga bungeni huku hadharani.

ukomavu wa kisiasa umeonyeshwa na Mzee Edwin Mtei Muasisi na Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA kwa kuonyesha dhahiri kukerwa na kejeli zote dhidi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Huo ndio ukomavu kisiasa.

Demokrasia maana yake kuongea, nje ya mazungumzo hakuna Demokrasia. Mazungumzo ni kukaa na kukubali kusikiliza na kusikilizwa. Kama hauko tayrai kusikiliza, umezuia hata sauti yako kusikilizwa. Masharti ya kusikilizwa ni kusikiliza principally binadamu akiongea maneno matano anatakiwa asikilize kumi ndo maana akapewa mdomo mmoja masikio mawili, siyo urembo wa kichwa huo.

Tanzania tumesifika duniani kote kwa tunu ya amani na utulivu. Amani na utulivu wa tanzania ndiyo nguzo ya utahbiti wa Afrika. Tanzania ndiyo nchi pekee Afrika ambayo ilitengenezwa na waafrika wenyewe, nyingine zote zilitengenezwa na wakoloni tu. Jina Tanzania lenyewe ni la kipekee (exceptional).

Dunia nzima inaitazama Tanzania kama kitovu cha umoja na mshikamano wa Afrika. Na nguvu ya Afrika inaitegemea sana Tanzania tangu enzi za mataifa mengi kuwa Makoloni ya wazungu hata baada ya uhuru. Tanzania ilihusika kwa kiwango cha juu kabisa kwa ukombozi wa bara la Afrika na ikabaki kuwa ndiye mlinzi wa amani. Hadi sasa Tanzania imekuwa tegemeo kwa ajili ya vikosi vya Umoja wa Mataifa kulinda amani ya dunia kama kule Lebanon, Sudan kusini, Libya, Somalia, Ivory Coast, Siera Leone, Liberia, Msumbiji, Angola, Congo DRC na hata sasa huko Jamhuri ya Afrika ya Kati Tanzania itategemewa sana.

Tanzania imekuwa Mpatanishi wa Migogoro mingi iliyoshindikana barani Afrika. Tuna wanadiplomasia waliofanya kazi zao kwa ustadi mkubwa kiasi cha kuifanya Tanzania iheshimike pote duniani. Rwanda na Burundi Arusha ndiko nyumbani kwao kwa Mapatanisho toka miaka ya 1990s. Na kwa jinsi hii, Arusha imekuwa kituo cha Upatanishi wa Afrika hata kuitwa GENEVA OF AFRIKA. Hii ni sifa ambayo Tanzania tunayo na haikuja ghafla au kushuka kama Mana au Mvua bali imetengenezwa.

Ikiwa Tanzania tumekuwa wapatanishi wa mataifa mengi Afrika, tumeshughulika na ulindaji amani ya dunia hii, tuna swali moja la kujiuliza, Je hao tuliowapatanisha au kuwalindia amani yao wanatupenda kutuona tukiwa na utulivu na amani hivi? Huko nje ya Tanzania na nje ya Afrika, wapo wanaouliza "Hivi Tanzania kuna nini; mataifa mengi ya kiafrika yamepalaganyika na kupigana wao kwa wao lakini imekuwa ngumu kutokea Tanzania kwa nini? Swali hili mtu akiuliza ama ana mantiki hii, Ni nini mataifa mengine yanaweza kujifunza kutoka Tanzania; ama ni mbinu gani wanatumia kuwa wamoja hivyo na ili waweze kufikisha chokochoko za kutusambaratisha wafanye nini. Kwa mantiki ya kwanza hakuna shaka hao wanalitakia mema bara la Afrika. Kwa mantiki ya Pili, wamegundua kuna ugumu wa kuisambaratisha Afrika yote kwa pamoja kama Tanzania bado ni Jamhuri ya Muungano inayodumu.

Maadui wa Tanzania wamegundua njia pekee ya kutusambaratisha Tanzania na Utanzania wetu, ni kutufanya tuusambaratishe Muungano. Nje ya Muungano Tanzania itasambaratika kuliko Sudan Kusini ama Somalia. Watanzania tuna nguvu sana ndani ya Muungano, nje ya Muungano ni kama mboga ya "Mrenda".

Maadui wa Tanzania na Afrika kwa ujumla wamegundua kuwa hoja yoyote waliyowahi kuijenga kwingineko Afrika, hapa haifanyi kazi. Maana huko kwingine walifanikiwa tu kwa kujenga chuki miongoni wa watawala wa tabaka la juu na lile la chini, walipofika Tanzania wakakuta kuna ushirikiano na heshima kubwa kati ya matabaka hayo. Wakajaribu kutengeneza chuki miongoni mwa wananchi kwa itikadi zao za kisiasa, wamegundua hilo halifanyi kazi maana watanzania hawawezi kugombana kwa itikadi wakati wanaishi pamoja. Chokochoko za kidini nazo zimegonga mwamba. Wamegundua, lililo baki ni moja tu, nalo ni Muungano.
Wamegundua nje ya Muungano, hakuna nguvu maana nje ya Muungano hakuna Zanzibar, kuna Unguja na kuna Pemba. Nje ya Muungano kuna Wazanzibari ORIJINO na Wazanzibari AKADEMIA. Na ukifika hapo ni akzi rahisi kuwavuruga watanzania wa sasa kuliko wakiwa wamoja.

Namna pekee ya kufikia adhma ama njema ama mbaya, ni kupitia mchakato huu wa katiba. Niliwahi kusema "BAPHOON" ni Mtu asiyejali usalama wa nyumbani kwake bali anajali maslahi ya wanaomtuma kuharibu nyumbani kwake kwa Ujira mdogo. Neno hili Baphoon lilitumiaka sana Zimbabwe mwaka jana wakati wa Uchaguzi Mkuu, wazimbabwe wakilitumia kumuwakilisha Morgan Tshangirai ambaye alitumiaka kwa maslahi ya Wazungu kuiangamiza Zimbabwe. Uwezo wa wazimbabwe kuligundua hli walimdhihirishia katika kura, na eti matokeo ya Zimbabwe, yanayohusu Zimbabwe na Wazimbabwe Marekani wanasema si halali.

Wapo Baphoon Tanzania ambao wako tayari kupokea kitu chochote kutoka huko Magharibi ili waliangamize Taifa. Wamekuja na staili eti wanatetea katiba ya wananchi na wameamua kutetea nje ya uwanja halali wa kutetea. Wanataka wawainue wananchi wakasirike ili wakisha kasirika, basi kuwe na mfarakano utakaoyumbisha muungano. Na wakifanikiwa kwa hilo, basi Muungano utakuwa umefika ukingo wake. Zanzibar inatumika kama kichaka cha siasa za kidhalimu na wadhalimu. Mantiki iko wapi, ufanyie mkutano Dodoma ili ikitokea unaamua kurudi bungeni iwe karibu ama Zanzibar? Wapi karibu, Iramba kwa Tundu Lissu ama Zanzibar au kutoka Tabora kwa Lipumba ama Hai kwa Mbowe ama Zanzibar. Ipo namna.

Kauli zote za Wajumbe wa kundi la UKAWA wakiwa nje ya Bunge maalum la katiba hazitakuwa na maana yoyote maana mwisho wa siku rasimu ya katiba lazima kwanza itoke mle Bungeni kabla ya kwenda kwa wananchi ambao wao UKAWA wanadai wanawakilisha.

Ili Kuwa na mchakato ulio halali, haijalishi utakuwa na ugumu upi, mahali pekee pa kujadiliana kwa mahali tulipofikia na mchakato wetu ni bungeni Dodoma. Ratiba iko wazi tulianza kwa kutengeneza sheria ya mabadiliko ya Katiba, tukaunda tume, tukatengeneza mabaraza ya katiba, tukakusanya maoni na kuyapitia, tume ikatengeneza rasimu ya kwanza na yapili, tukaunda bunge maalum la katiba kwa mujibu wa sheria, bunge limekutana tukasiki maelezo ya tume na tume kazi yake imekwisha. Tukimaliza Bunge hili tunakwenda sasa kwenye kura ya maoni ambako sasa tutapiga kampeni tukishawishi wananchi ama wakubali ama wakatae hiyo rasimu ya Bunge. Na hiyo ndiyo itakuwa Katiba ya Wananchi. nje ya Mchakato huu hakuna Katiba

Mungu Ibariki Tanzania

Paul C. Makonda
Mjumbe Bunge Maalum la Katiba
makondapaul@gmail.com
 
Nilipo sikia kuwa Tanzania iko miongoni mwa mataifa 10 ya Afrika ambayo raia wake wana IQ ya chini mno nilijiuliza sampling hiyo wameifanyia wapi sasa nimepata jibu kuwa no ndani ya UVCCM na Wajumbe wa Katiba wale wasio ndani ya UKAWA. Kama wewe hapa ulitaka kumaanisha nini? Au wewe baada ya kuandika ukisoma tena unaelewa?
 
SDC10849.JPG


Paul Christian Makonda, "UVCCM acheni kutapatapa!"

Paul Christian Makonda said:
Natoa tamko ambalo litekelezwe ndani ya siku saba kuanzia leo (yaani hadi jumatatu ijayo tarehe 3/4/2011) liwe limetekelezwa;
Paul Christian Makonda said:
  1. SEKRETARIET YOTE ya UVCCM iitishe press conference kama hii iwaombe radhi watanzania kwa matusi yaliyosababisha chama kudhalilishwa;
  2. SEKRETARIET ya UVCCM TAIFA yote iachie ngazi kwani imeshindwa kufanya yale ambayo UVCCM umeundwa kwayo
  3. KAMATI YA UTEKELEZAJI yaUVCCM TAIFA yote, nayo iachie ngazi
  4. BARAZA KUU la UVCCM lote LIJIVUNJE

Kwa tamko hili, baada ya siku saba kupita UVCCM ibaki katika ngazi ya wilaya tu (ambako vijana wapo) mpaka hapo taarifa mbadala itakapotolewa.
PAUL CHRISTIAN MAKONDA

Mjumbe Wa Mkutano Mkuu Wa CCM Wilaya ya Moshi Mjini

Mwanachama Wa UVCCM

Simu: 0754754417; 0717213600

makondapaul@gmail.com
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI





Huyo ndiye Paul Christian Makonda,
Mjumbe Bunge Maalum la Katiba
...
Homa huanza pole pole,
wenda wazimu huja taratibu.

 
Paul Makonda

Kwanza nikukaribishe na hakikisha hukimbii mjadala.

Tafadhali lipe jukwaa heshima yake kwa kutoa ushirikiano.

Halafu tukuulize tena, upo nasi au umetumwa tu kutua mzigo?

Kama umetumwa kila la heri, kama upo nasi twaomba ututoe wasi wasi ili tuweke kambi ya uhakika hapa mahala pako ulipofikia.

Tafadhali pata karanga na chai, tumetoka kidogo tukirudi tutaongea vema kuhusu safari ya Dodoma na bango kitita lenye randama uliotujaalia.

karibu




Ahsante Sana.
 
Paul Makonda
Kwanza nikukaribishe na hakikisha hukimbii mjadala.
Tafadhali lipe jukwaa heshima yake kwa kutoa ushirikiano.
Nguruvi3

Nashani atakuwa Ametumwa kutua mzigo tu, maana mpaka sasa angekuwa amesharudi, lakini si mbaya acha tumpe Muda,ili akija tuzungumze nae kidogo.
 
Katiba ya wananchi mlishaikataa kabla hata UKAWA came to being. Kwa sasa ni bora tu msubirie kuja tafunwa na dhambi ya kukataa mapendekezo ya rasimu.

Ni dhahiri kwamba hauji hapa kujadiliana na wananchi wenzako kwa hoja bali kujenga CV kwa wakubwa wako kwamba na wewe "unasema sema huko nje" kutetea chama, hata kama ni kwa mambo ya kipuuzi yasiyo na tija kwa wananchi walio wengi.

Kwa vile hautaki kujibu hoja, ni vyema haya ungeyapeleka huko magazetini. Umealikwa na Nguruvi3 kwenye mjadala, kama una uthubutu wa mijadala, karibu, lakini sioni uwezo huu kwako. Unachoweza ni kupiga porojo kwenye microphone mle bungeni, na kuita press conference kutukana wazee wako kama njia ya kutafuta umaarufu na kujijenga.

Umepotea mdogo wangu, ipo siku nitakuja kukumbusha nilikuwa nina maana gani. Vinginevyo kwa njia hiyo uliyopotea, naomba nikupe hongera za uteuzi wa Ukuu wa Wilaya, in advance. Una miaka miwili tu ya career ya maana kisiasa ikiwa hautabadilika. Mark my words - Two Years!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,
Nashani atakuwa Ametumwa kutua mzigo tu, maana mpaka sasa angekuwa amesharudi, lakini si mbaya acha tumpe Muda,ili akija tuzungumze nae kidogo.
Wakati anajikusanya tungempa dondoo kwa uchache ili akija ajiandae na mashoka, visu na mapanga. Tangawizi kasema kuna milima, kona n.k.
Paul Makonda , ni mwenyekiti wa chipukizi wa CCM.
Maneno uliyotumwa kuyaleta jamvini hayakukusudiwa hapa, yalikusudiwa kwa chipukizi wenzako.

Hujaweza kutueleza mfumo wa serikali 2 ni kitu gani, na kwanini unadhani ni muafaka.
Umekuja na hoja za amani na utulivu ingawa hujui amani na utulivu ni kitu gani.

Paul waambie waliokutuma kuwa Tanzania hakuna amani wala utulivu, kuna ukimya.
Amani na utulivu ni zao faraja, upendo na matumaini katika maisha.

Kwa miaka 50 chini ya muungano wa S2 na CCM,rasilimali lukuki n.k. Watanzania wanaishi chini ya dola mbili kwa siku.

Wale wachache wanaoishi kwa dola 100 kwa siku wapo ndani ya chama chako wakiiba na kutia saini mikataba inayolipiwa na nduguyo Morogoro anayeishi kwa dola 2 kwas siku.

Wapo Watanzania ndani ya chama chako wanaenda India na South Africa kuchekiwa blood pressure(si kuumwa) wakati kuna mzazi yupo juu ya tenga la baiskeli akitoka Matombo kuja Morogoro usiku wa manane. Kama utamkuta hai Morogoro hospitali basi ni kudra za maanani.

Wakati mapapa wezi ndani ya chama chako wakiwa na utulivu na amani kwa kupeleka wake zao Appolo kutibiwa chunusi zinazoongezeka na sasa ni 10, kuna nduguyo alifanyiwa referal kutoka Morogoro kuja muhimbili amelala sakafuni akitibiwa kwa Panadol wakati anasubiri kuhitimisha safari yake.

Ndugu yako huyo aliyelala muhimbi akiugulia maumivu ameacha mke ana watoto ambao ile dola 2 wanayopata kwa siku wanatoa kiasi fulani kwenda kulipia umeme wa ziada ambao ima ni deni la muungano kutoka znz au ni deni la Tanesco lililosainiwa na makada wako maarufu kama mafisadi.

Unaposimama na kusema muungano umeleta amani na utulivu, wakati kuna mtu hana amani kwavile anasubiri asubuhi nduguye ahamishiwe chumba cha maiti, si kuwa unaitukana jamii yako, lakini pia unatueleza ilikuwaje ukawa kiongozi ukitokea katika BML.

Nani alikuchagua na huyo aliyekuchagua yeye alitumia vigezo gani.
Unaitukana familia yako ambayo kwa muda huu inagawana vipande vya mgagani huku watoto wakikabwa na mlenda hadi utakaporudi na laki 3 pengine wale mkate kwa mara ya kwanza tangu mwaka huu uanze.

Hao chipukizi wanaokusubiri kiongozi wao wapo katika mateso makubwa. Ni uhalifu mkubwa chipukizi na makinda ya nchi hii kuwa chini ya uongozi wa raia mwema kama wewe.
Chipukizi wanahitaji maono, si njozi zinazotisha na wala si hafifu. Mungu wanausuru chipukizi

Kuhusu suala la Mugabe, ungejua kitu kinaitwa economy tunegeweza kuongea, nachelea nikiongelea GDP unawaze kunifaikisha kwa Moderator kwa kukukutukana. Naomba niishie hapo.

Ili tu kukupa neno la leo, hiyo Zimbabwe unayoongelea huijui. Leo Wazimbwabwe wana zamia malori kuja Tanzania.
Unaongea nini paul!!!

Wakati unafungwa kibebwe ili uje tuongee napenda nikuulize Tanzania bara ni nchi gani, ilitokea wapi na kwa njia zipi.

Kama hutatokea hapa basi uwe mwisho wako, na waambie waliokutuma umeingia maliwato bila kuangalia jinsia.

Ahsante mheshimiwa mbunge wa BMLK.
 
Last edited by a moderator:
Katiba ya wananchi mlishaikataa kabla hata UKAWA came to being. Kwa sasa ni bora tu msubirie kuja tafunwa na dhambi ya kukataa mapendekezo ya rasimu.

Ni dhahiri kwamba hauji hapa kujadiliana na wananchi wenzako kwa hoja bali kujenga CV kwa wakubwa wako kwamba na wewe "unasema sema huko nje" kutetea chama, hata kama ni kwa mambo ya kipuuzi yasiyo na tija kwa wananchi walio wengi.

Kwa vile hautaki kujibu hoja, ni vyema haya ungeyapeleka huko magazetini. Umealikwa na Nguruvi3 kwenye mjadala, kama una uthubutu wa mijadala, karibu, lakini sioni uwezo huu kwako. Unachoweza ni kupiga porojo kwenye microphone mle bungeni, na kuita press conference kutukana wazee wako kama njia ya kutafuta umaarufu na kujijenga.

Umepotea mdogo wangu, ipo siku nitakuja kukumbusha nilikuwa nina maana gani. Vinginevyo kwa njia hiyo uliyopotea, naomba nikupe hongera za uteuzi wa Ukuu wa Wilaya, in advance. Una miaka miwili tu ya career ya maana kisiasa ikiwa hautabadilika. Mark my words - Two Years!



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mchambuzi, I agree with you asilimia zote, nimesoma lines zako kwa kijana nahisi I was reading on your way ndio maana nadhani nimeelewa nini unamaanisha. Sina nyongeza ila bado navuta subila huenda akatokea
 
Last edited by a moderator:
Wakati anajikusanya tungempa dondoo kwa uchache ili akija ajiandae na mashoka, visu na mapanga. Tangawizi kasema kuna milima, kona n.k.
Paul Makonda , ni mwenyekiti wa chipukizi wa CCM.
Maneno uliyotumwa kuyaleta jamvini hayakukusudiwa hapa, yalikusudiwa kwa chipukizi wenzako.

Hujaweza kutueleza mfumo wa serikali 2 ni kitu gani, na kwanini unadhani ni muafaka.
Umekuja na hoja za amani na utulivu ingawa hujui amani na utulivu ni kitu gani.

Paul waambie waliokutuma kuwa Tanzania hakuna amani wala utulivu, kuna ukimya.
Amani na utulivu ni zao faraja, upendo na matumaini katika maisha.

Kwa miaka 50 chini ya muungano wa S2 na CCM,rasilimali lukuki n.k. Watanzania wanaishi chini ya dola mbili kwa siku.

Wale wachache wanaoishi kwa dola 100 kwa siku wapo ndani ya chama chako wakiiba na kutia saini mikataba inayolipiwa na nduguyo Morogoro anayeishi kwa dola 2 kwas siku.

Wapo Watanzania ndani ya chama chako wanaenda India na South Africa kuchekiwa blood pressure(si kuumwa) wakati kuna mzazi yupo juu ya tenga la baiskeli akitoka Matombo kuja Morogoro usiku wa manane. Kama utamkuta hai Morogoro hospitali basi ni kudra za maanani.

Wakati mapapa wezi ndani ya chama chako wakiwa na utulivu na amani kwa kupeleka wake zao Appolo kutibiwa chunusi zinazoongezeka na sasa ni 10, kuna nduguyo alifanyiwa referal kutoka Morogoro kuja muhimbili amelala sakafuni akitibiwa kwa Panadol wakati anasubiri kuhitimisha safari yake.

Ndugu yako huyo aliyelala muhimbi akiugulia maumivu ameacha mke ana watoto ambao ile dola 2 wanayopata kwa siku wanatoa kiasi fulani kwenda kulipia umeme wa ziada ambao ima ni deni la muungano kutoka znz au ni deni la Tanesco lililosainiwa na makada wako maarufu kama mafisadi.

Unaposimama na kusema muungano umeleta amani na utulivu, wakati kuna mtu hana amani kwavile anasubiri asubuhi nduguye ahamishiwe chumba cha maiti, si kuwa unaitukana jamii yako, lakini pia unatueleza ilikuwaje ukawa kiongozi ukitokea katika BML.

Nani alikuchagua na huyo aliyekuchagua yeye alitumia vigezo gani.
Unaitukana familia yako ambayo kwa muda huu inagawana vipande vya mgagani huku watoto wakikabwa na mlenda hadi utakaporudi na laki 3 pengine wale mkate kwa mara ya kwanza tangu mwaka huu uanze.

Hao chipukizi wanaokusubiri kiongozi wao wapo katika mateso makubwa. Ni uhalifu mkubwa chipukizi na makinda ya nchi hii kuwa chini ya uongozi wa raia mwema kama wewe.
Chipukizi wanahitaji maono, si njozi zinazotisha na wala si hafifu. Mungu wanausuru chipukizi

Kuhusu suala la Mugabe, ungejua kitu kinaitwa economy tunegeweza kuongea, nachelea nikiongelea GDP unawaze kunifaikisha kwa Moderator kwa kukukutukana. Naomba niishie hapo.

Ili tu kukupa neno la leo, hiyo Zimbabwe unayoongelea huijui. Leo Wazimbwabwe wana zamia malori kuja Tanzania.
Unaongea nini paul!!!

Wakati unafungwa kibebwe ili uje tuongee napenda nikuulize Tanzania bara ni nchi gani, ilitokea wapi na kwa njia zipi.

Kama hutatokea hapa basi uwe mwisho wako, na waambie waliokutuma umeingia maliwato bila kuangalia jinsia.

Ahsante mheshimiwa mbunge wa BMLK.

Kiongozi, Nguruvi3, nadhani hapa kijana ndio umemfukuza kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Mbombo ngafu!

Makonda.

Kwani kazi ya bunge maalum la katiba ni kuandika rasimu mpya ya katiba au kupitia Rasimu ile iliyoletwa na Tume ya kukusanya maoni ya Katiba mpya?

Au kwa kifupi tudadavulie nini kazi ya Tume ya jaji Warioba ? na Nini kazi ya Bunge maalum la Mh Samwel Sita?
 
Kwa mtazamo wangu sii vizuri hata kidogo kuanza na mashambulizi kwa mtoa mada badala ya kujadili mada iliyopo kwani hii inalifanya jukwaa hili lisiwe na heshima zake. Inapotokea mtu kutokubaliana a mtoa mada basi ni busara kuzungumzia vifungu ama zile sehemu ambazo hukubaliani na wewe unaamini lipi ili mtoa mada aweze kurudi na majibu aidha kufafanua zaidi ama kujibu hoja zilizotolewa. Sii ungwana kabisa kuanza kumfikiria mtu azma ya mada yake wakati sisi wenyewe tunaweza kuwa ni miongoni mwa wale wale walokuja hapa kwa kutumwa vile vile.

Binafsi zipo sehemu nakubaliana na Mtoa mada japo sii zote kutokana na kwamba hakuzungumzia wala kuchambua sababu za hawa UKAWA kujitoa ila ameonyesha kulaani kitendo hicho kwa kusifia yaliyopo sasa ndani amuungano huu wa serikali 2. Nakubaliana na mwandishi ktk swala la UKAWA kujitoa bungeni kwa sababu maamuzi hayo hayatokani na MWANANCHI bali ni maamuzi yao wao wenyewe ambao awali ya yote baada tu ya kuteuliwa na rais wajumbe hawa wote walidai kwamba HAWAKUTUMWA na WANANCHI ila kujadili changamoto za rasimu hiyo hadi kufika maamuzi ya kuuandika katiba inayotokana na wananchi (KATIBA YA WANANCHI) kupitia maoni ya wananchi yalokusanywa ktk rasimu ya WARIOBA. Hizi ndizo zilikuwa kauli za wajumbe wateule wa baraza hili la katiba hivyo katika baadhi ya vikao vyao wakasisitizana kila mmoja wao awakilishe MAWAZO YAKE na sii ya chama ama vinginevyo. Kama nakosea naomba kusahihishwa!

Hivyo, wanapofikia kuondoka Bungeni (kwa msimamo wa vyama) kwa madai ya kwamba wanaitaka Katiba ya wananchi najiuliza ni katiba ipi hiyo? maana wao ndio waandishi wa katiba ya wananchi na kama kuna vikwazo ama imeshindikana kuandika katiba hiyo, sisi wananchi ndio tunatakiwa kuwahoji wao maana ktk changamoto ambazo wangekutana nazo ni pamoja na kutokubaliana katika vifungu vya sura, ibara ama sehemu za ibara kwa nia njema ambayo wana hakika wananchi wangeikubali. Hivyo kanuni zao zingelinda uchama na matokeo kama haya ili kuiwezesha katiba hiyo isikwamishwe na kundi la watu ambao wapo pale kwa maslahi binafsi ama ya chama.

Kazi yao ilikuwa kupitia rasimu ya Warioba vifungu kwa vifungu kwa kila sura na Ibara na kutoa mapendekezo yao mahala wasipokubaliana ama wamekubaliana na kuyapigia kura kupitisha ama kutopitisha na pengine kuzifanyia marekebisho kama wanavyoona wao inafaa. Kwa hiyo hakuna kitu kilichokuwa wao ndio wanahitimisha unadishi wa katiba, bali kuchambua mapendekezo yale na kukubaliana ktk msingi wa wengi wape na kwa nia njema kabisa, na kibaya zaidi kanuni za uendeshaji wa bunge hili wamezitunga wenyewe na wamekubaliana wenyewe iweje hali hii itokee wakati walijua toka mwanzo wapo pale kuwakilisha mawazo yao?.

Kwa mtazamo wangu, hawa UKAWA (vyama vya Upinzani) toka mwanzo hawakutakiwa kukubali mwaliko (uteuzi) wa wao kushiriki kutunga katiba na wakieleza sababu zao kwani toka mwanzo CCM ilikuwa na wajumbe wengi kuliko wajumbe wa mabaraza (taasisi) yote. Wao waliamini wapo pale kama watu binafsi wenye mawazo binafsi (siii kweli) Ukweli ni kwamba tumeshuhudia kulikuwepo na wajumbe wa CCM na wale wa Vyama vya Upinzani ktk uandishi wa katiba ya wananchi. Hawa hawa UKAWA waliaminishwa kupewa mamlaka ya utunzi ambao hata kipofu angeweza kuelewa nje ya matakwa ya CCM hakuna KATIBA na hii ilianza toka awali hadi uchaguzi wa Mwenyekiti wa bunge hilo. Wao wenyewe walimwagia sifa Mwenyekiti wa Bunge hilo kuwa na uzoefu wa kuendesha Bunge tena bunge la serikali 2, ndio kusema hawakujua au?

Na katika Ufunguzi wa bunge hilo Kiongozi Sitta alisema wazi na kuwaaminisha ya kwamba wataifanya kazi hiyo kwa ufanisi kwani inahitaji uvumilivu mkubwa, busara, na ukomavu wa ksiasa, hizo sifa walijiona wanazo hivyo mwenyekiti akapigiwa makofi mengi sana, nasi wananchi tukaweka matumaini yetu juu yao kuwa kazi imeiva. Mambo yakaanza kuharibika kwenye Posho! tukashuhudia ubinafsi wao lakini yakapita japo inatugharimu lakini tuliitaka katiba mpya haraka iwezekanavyo.

Sasa nirudi ktk hoja kuu ya serikali 3. Wanabodi Watanzania wenzangu, unapotaka kuandika upya katiba na kuifanya iwe mwongozo wa Taifa ama kuonyesha msingi na nguzo iliyopo haifai ni batili, ni muhimu kwa upande wa Ukawa na rasimu ya Warioba kujieleza wazi kwa nini tunahitaji kuwa na serikali 3 badala ya 2. Nini mapungufu ya serikali 2 na hizo serikali 3 zitafanya kazi vipi dhidi ya mapungufu hayo. Lakini badala ya bunge hili kuzungumzia mapungufu ya serikali 2 wakaanza kuzungumzia kero za miaka 50 ya serikali 2 ama muundo huu umetuletea nini? kana kwamba wao wanafahamu miaka 50 kwa serikali 3 zingeweza kufanikisha kadhaa wa kadhaa - Hawakutupa takwimu ila kwa kuzungumzia kero za muungano.

Wakaendelea kutumika kuhoji hata Hati ya Muungano kuwa sii halali, wakamsema hadi muasisi wetu mwl. Nyerere kuwa ni mlaghai aliyejitungia yeye muungano siku moja alipoamuka asubuhi na kadhalika. Hii ilikuwa kashfa kubwa kwa Taifa hili na hasa ukizingatia kwamba Muungano wetu unapakwa picha ya kughushiwa! Sii halali wala haikupitishwa na wajumbe wa pande zote 2. Haya yote yametokea ndani ya Bunge la Katiba halafu watu hawa leo walitaka Mheshimiwa JK atakapo kuja kutoa hutuba yake awe upande wao!.

Na inasikitisha zaidi kuwasikiliza wajumbe wa bara na vyama kama Chadema wakisimama na kuunga mkono hoja za viongozi wa Hizbu kuwa ndio ukweli ambao hata wao wanaukubali halafu walipokuja hakikishiwa ukweli ni upi wakaendelea kudai watahakikisha vipi kuwa Hati hiyo ni HALALI?. Jamani jamani kweli nyie mpo pale kuandika katiba ya wananchi wa taifa hili au taifa gani? hata kama mimi ningekuwa upande wa UKAWA nikikubaliana na serikali 3, kwa ushahidi wao wa mapungufu ya serikali 2 waloutoa bungeni ilikuwa ni aibu tupu na sidhani kama hapa swala lilikuwa tena muundo wa serikali 3 bali kuukana Muungano wenyewe. Sasa ni katiba gani walotaka kuandika ikiwa hata hati ya Muungano wenyewe hawaikubali wala kuitambua!

Nitakomea hapa mwenye maswali ama hoja tuelezane na sii kuvuana nguo (matusi).. Karibuni tafadhali..
 
Mkandara;10021972]Kwa mtazamo wangu sii vizuri hata kidogo kuanza na mashambulizi kwa mtoa mada badala ya kujadili mada iliyopo.Wewe unaamini lipi ili mtoa mada aweze kurudi na majibu aidha kufafanua zaidi ama kujibu hoja zilizotolewa.
Mkuu Mkandara , hivi umesoma habari ya makonda ukajiridhisha kabisa kuwa kuna mada na hoja!!
Mkandara;10021972:Nakubaliana na mwandishi ktk swala la UKAWA kujitoa bungeni kwa sababu maamuzi hayo hayatokani na MWANANCHI bali ni maamuzi yao wao wenyewe ambao awali ya yote baada tu ya kuteuliwa na rais wajumbe hawa wote walidai kwamba HAWAKUTUMWA na WANANCHI ila kujadili changamoto za rasimu hiyo hadi kufika maamuzi ya kuuandika katiba inayotokana na wananchi (KATIBA YA WANANCHI) kupitia maoni ya wananchi yalokusanywa ktk rasimu ya WARIOBA. Hizi ndizo zilikuwa kauli za wajumbe wateule wa baraza hili la katiba hivyo katika baadhi ya vikao vyao wakasisitizana kila mmoja wao awakilishe MAWAZO YAKE na sii ya chama ama vinginevyo. Kama nakosea naomba kusahihishwa!
Mkuu hapa sijui ulikusudia ujumbe gani. Nikijibu naweza kwenda nje ya mada labda kama utafafanua. Kwa jinsi ilivyo ni ngumu kuielewa
Hivyo, wanapofikia kuondoka Bungeni (kwa msimamo wa vyama) kwa madai ya kwamba wanaitaka Katiba ya wananchi najiuliza ni katiba ipi hiyo? maana wao ndio waandishi wa katiba ya wananchi na kama kuna vikwazo ama imeshindikana kuandika katiba hiyo, sisi wananchi ndio tunatakiwa kuwahoji wao maana ktk changamoto ambazo wangekutana nazo ni pamoja na kutokubaliana katika vifungu vya sura, ibara ama sehemu za ibara kwa nia njema ambayo wana hakika wananchi wangeikubali. Hivyo kanuni zao zingelinda uchama na matokeo kama haya ili kuiwezesha katiba hiyo isikwamishwe na kundi la watu ambao wapo pale kwa maslahi binafsi ama ya chama.
Kwani uchama umeanza leo?
Si unakumbuka mswada wa sheria ya mchakato ilipitishwa kwa akidi ya watu 100 tena kwa kutumia nguvu.

Mkandara, aliyetoa msimamo wa chama ni nani kama si Pinda, Bilal, Sheni na kuhitimishwa na Kikwete siku ya kufungua bunge? Kikwete alisema nini kama si msimamo wa chama chake? Ni mara nganpi amesema vyama vinaruhusiwa kukaa kama caucus tena wakakaa na kuamua kura ya wazi. Leo kote huko hukuoni unaanzia na UKAWA.
Nilidhani ungekuwa fair ili tuwe na mjadala endelevu kwa faida ya wasomaji, kwa makengeza unayojitia, nimepoteza matumaini.
Kazi yao ilikuwa kupitia rasimu ya Warioba vifungu kwa vifungu kwa kila sura na Ibara na kutoa mapendekezo yao mahala wasipokubaliana ama wamekubaliana na kuyapigia kura kupitisha ama kutopitisha na pengine kuzifanyia marekebisho kama wanavyoona wao inafaa.
Mkandara alitoa pendekezo la kujadili suara ya 1 na 6 ni nani?
Si Samwel Sitta kwa kutumwa na CCM. Mkuu mbona unadorora kiasi hiki.

UKAWA walisema kipitiwe kifungu kimoja hadi kingine. Aliyeunda kamati kwa makusudi ya kutoa majority ni Sitta. Majority iliposhindikana ndipo ikaundwa mbinu ya kurudi kupigia vifungu hivyo kura ya wazi na siri. Huo mlolongo wa ulaghai mkuu huuoni. Nini kinakupelekea unapoteza dira kiasi mkuu!!
Kwa hiyo hakuna kitu kilichokuwa wao ndio wanahitimisha unadishi wa katiba, bali kuchambua mapendekezo yale na kukubaliana ktk msingi wa wengi wape na kwa nia njema kabisa, na kibaya zaidi kanuni za uendeshaji wa bunge hili wamezitunga wenyewe na wamekubaliana wenyewe iweje hali hii itokee wakati walijua toka mwanzo wapo pale kuwakilisha mawazo yao?.
Mkandara, naona labda niishie hapa kwasababu kadri ninavyokusoma nashindwa kukuelewa. Huenda ndio maana umefikia kiwango cha kuelewa mada za Makonda ambazo hazipo ab initio.

Mkandara suala la katiba halina wengi wape wakati wa kuandika.
Lazima uelewe kuwa tunatakiwa tueondoke hapa tulipo katika siasa za majitaka ya uchama,twende mbele na ku shape future ya watoto na wajukuu zetu.

Hili suala la wengi wape lipo mitaani, wakati wa kuandaa nyaraka muhimu kama hii, unaposhauri wengi wape inasikitisha.
Mkandara wewe una exposure ya huko ulipo, hakika tumia hiyo kulisaidia taifa. Kwa mwendo huu ninaouona, unakatisha tamaa.
Samahani inabidi nikueleze ukweli tu.

Tunaposhindwa kuona tofauti kati yako na Makonda lazima fahamu kuna tatizo kubwa sana.
Hapa nakueleza mubashara, mkuu hoja ya wengi wape ni too low.

Ni kauli inayotumiwa sana na hoodlums, nincompoop and the likes wanapokuwa hawana mawazo wala hawana hoja.

Hivi kiwango cha wabunge wetu unakijua?
Pili, wengi wape si ndio imetengeneza katiba ya 1977 kwanini leo tunaandika tena?

Kwamba wengi wakiamua kuwa Rais anaweza kuuza mkoa ikibidi basi ndiyo wengi wape yenyewe.
Katiba inapigiwa kura na wengi, haiandaliwi na wengi. Inaanza kwa ellite halafu inaishia mitaani.

I am sorry I have to tell you. Mkandara, never say it again.
Mkuu you're way better than this. Please, never say it again.

Naomba niishie hapa nisijeingia eneo nisilotarajia hata kama nina mengi. Inasikitisha sana
 
Mkuu Mkandara , hivi umesoma habari ya makonda ukajiridhisha kabisa kuwa kuna mada na hoja!!
Nimemsoma vizuri na ndio maana nimezungumzia tu sehemu ambazo mimi naafikiana naye kwa sababu mada yake inahusu UKAWA pale baadhi ya wajumbe wa katiba kususia kushiriki kwa sababu zao wenyewe bila kutazama makosa yao wenyewe. Makosa hayo nimeyaorodhesha vizuri tu na wangefanya nini toka mwanzo pia nimeelezea.

Mkandara;10021972: Mkuu hapa sijui ulikusudia ujumbe gani. Nikijibu naweza kwenda nje ya mada labda kama utafafanua. Kwa jinsi ilivyo ni ngumu kuielewa
Bila shaka ni ngumu kwako kuelewa kwa sababu hufuatilii kabisa hoja za wabunge wenyewe toka walipoteuliwa kujiunga na bunge la katiba hadi walipokuwa bungeni, walianza kusambaratika wakati gani! . Nayoyasema sii yangu miye bali ni maneno yao wenyewe, walidai ya kwamba hawapo pale kuwakilisha wananchi (it's on record) na wameteuliwa wao kutokana na uwezo na sifa zao hivyo kila mmoja wao alitakiwa kutumia mawazo binafsi yasiyofungamana na chama, taasisi ama makundi ua kijamii of which contradict the all purpose!

Wajumbe wote hawa waliteuliwa na rais toka vyama na Taasisi na makundi ya Kijamii iweje wao wafiirie walichaguliw akwa sababu ya uwezo wao wa kuchambua na kuandika katiba? Ok lets say ndivyo ilivyokuwa sasa walishangaa vipi npale CCM walipoanza kueteta maslahi ya chama chao ikiwa wajumbe wengine walianza kuzungumzia Muungano fake! Kwa hiyo mkuu wangu matokeo ya pale bungeni ni kitu kilichokwisha pandwa toka mwanzo kwa uteuzi ule ambao ulizingatia vyama, taasisi na kadhalika ije kuwa ni watumishi wa wananchi. Lini Mwana CCM akawa mkuu wa shirika amaUsalama mkategema ati hatakuwa bias inapofikia maamuzi dhidi ya chama chake!

Kwani uchama umeanza leo?
Si unakumbuka mswada wa sheria ya mchakato ilipitishwa kwa akidi ya watu 100 tena kwa kutumia nguvu.

Mkandara, aliyetoa msimamo wa chama ni nani kama si Pinda, Bilal, Sheni na kuhitimishwa na Kikwete siku ya kufungua bunge? Kikwete alisema nini kama si msimamo wa chama chake? Ni mara nganpi amesema vyama vinaruhusiwa kukaa kama caucus tena wakakaa na kuamua kura ya wazi. Leo kote huko hukuoni unaanzia na UKAWA.
Nilidhani ungekuwa fair ili tuwe na mjadala endelevu kwa faida ya wasomaji, kwa makengeza unayojitia, nimepoteza matumaini.
Mkuu tatizo lako huwa unaropoka tu husomi hoja ya mtu na kumuelewa sawa na kula nyama pasipo kuitafuna kwanza. na ndio maana haitakukwama tu bali utashindwa kupumua ukaanza kuona makengeza kila unapolazimisha kumeza nyama isotafunwa! Mimi ni mfuatiliaji mzuri sana wa hoja na mada na hasa hilo bunge la Katiba. labda nianze kwa kuuliza hivi, walomchagua huyo Sitta ni kina nani? Je, sisi hatukupendekeza achaguliwe mwenyekiti nje ya viongozi wa CCM nanyi na Ukawa mkasema Sitta ana uzorefu mkubwa kuliko wote? (kumbukumbu zipo)

Sasa haya ya Sitta ati ndiye kaandaa Rasimu ya CCM ipite Bungeni yanatoka wapi wakati wajumbe hawa hawa ndio walomchagua kwa mayowe na vigelelegele kwa kumuamini? mimi sikumuamini Sitta hata kidogo tena niseme wajumbe wote sikuwaamini toka mwanzo wa mchakato wa katiba hii watu walipokwenda kunywesha Juice na Soda Ikulu wakaridhia mfumo mzima wa auandikaji Katiba Mpya. naweza kusema JK kila anapowaita watu huwageuza ma zombie wasijue wamekubali nini au imekuwaje wakakubali visivyokubalika.

Pili, walioanzisha haya sio Pinda na Bilal isipokuwa wajumbe wa Zanzibar ambao waliitaka serikali 3 ya mkataba wakidai Hati ya Muungano sio halali na wakisema hata Saini ya karume ilikuwa Forged ina maana na Nyerere kama sio mtu mwingine. Huu ndio ulikuwa utetezi wa serikali 3 nje kabisa ya swala ama rasimu. Matusi haya hivi kweli wewe ulifikiria Pinda na viongozi wengine wa bara na visiwani kutoka CCM (TANU/ASP) wangeyachukulia kuwa madogo tena on TV kila mwanancjhi anasikiliza. halafu mijinga mingine ilikuwa inachukia Tv zikizimwa kwa sababu walitaka kuendelea kusikia matusi hayo wakidai ati CCM wamevanwa hadi chupi zinawavuka - On our UNION?..

Haya wee twambie sisi, ni wapi ktk rasimu ya Warioba swala la Hati ya Muungano liliwekwa? Ni wapi ktk rasimu ya Warioba kuna kipengele ama kifungu kinachozungumzia Uharamu wa Muungano wetu?. Mapendekezo ya kutaka kuona Uhalali wa muungano uliwekwa sura gani na ibara gani?..Halafu kweli mlitegemea JK angekuja pale bungeni na kuunga mkono muundo wa serikali 3 wakati vita sasa imekuwa juu ya serikali Muungano anayoitawala mwenyewe? Huoni kama Mlitoka nje ya rasimu ya katiba isipokuwa mnachotazama ni reaction ya JK na kukataliwa kwa serikali 3. Nimesema hata kama mimi ningekuwa JK na upande wenu, pale mlipoanza tu ku attack Muungano wenyewe, kuhoji Hati na hata mwanzilishi wa Muungano huo nisingekuwa nanyi hata kwa chembe! tena basi JK alifanya Ubinadamu sana kama miye ningewasweka ndani kwanza kisha majibu wakapewa manachi waliopo nje kuhakikisha kwamba nyie ndio mlotaka kuvuruga Uhuru na Muungano wetu.

Mkandara alitoa pendekezo la kujadili suara ya 1 na 6 ni nani?
Si Samwel Sitta kwa kutumwa na CCM. Mkuu mbona unadorora kiasi hiki.

UKAWA walisema kipitiwe kifungu kimoja hadi kingine. Aliyeunda kamati kwa makusudi ya kutoa majority ni Sitta. Majority iliposhindikana ndipo ikaundwa mbinu ya kurudi kupigia vifungu hivyo kura ya wazi na siri. Huo mlolongo wa ulaghai mkuu huuoni. Nini kinakupelekea unapoteza dira kiasi mkuu!!
Mkuu sasa wewe ulipendekeza waanze na sura gani? kulikuwa na utaratibu gani wa kuanza kupitia rasimu ile amabo wananchi walipendekeza au warioba na tume yake walipendekeza? Iwe Sitta au mwenyekiti yeyote maadam ilishindikana ina maana wajumbe wote walikuwa pale kwa maslahi yao na wakapendekeza pale wanapoona itawagharibu upande wa pili. It was all politics from day one.

Pili, haiwezekani kabisa mjadala wa rasimu ukaanza nje ya muundo wa serikali kwa sababu ndicho kiini cha katiba. Surana ibara nyinginezo zote zilitegemea maamuzi ya muundo wa serikali zetu na pasipo serikali huwezi kuwa na katiba. Kama serikali 3 zingepita basi kwanza ingetakiwa iundwe serikali ya Tanganyika, Katiba yake aidha ibakie hii ya JMT na kufanyiwa marekebisho jambo ambalo sidhani lingekubaliwa kutokana na katiba hii kuwa ni ya CCM. halafu ijengewe mihimili ya nchi ya Tanganyika na kisha ndio tukae tena kujadili swala la serikali nya Muungano ambayo Wazanibar waliitaka ya Mkataba. Kwa hiyo huwezi kuzungmzia lolote la katiba Mpya pasipo kutambua tutakuwa na serikali ngapi sawa na ujenge nyumba pasipo kuamua ni vyumba vingapi, vyoo, jiko na kadhalika sijui ungweza vipi kuchora ramani ya nyumba hiyo.

Anyway sikutegemea wewe utanielewa ila wapo walonisoma na kuuona ukweli kwa sababu tuliwasikia Kina Jussa, Tundu Lissu na wenzake wakiushambulia Muungano wenyewe kwa matusi makubwa halafu walipokuja kuzimwa ikaonekana kwamba CCM na JK ndio wenye makosa. makosa yalifanywa na kundi hili la wahuni walotaka umaarufu kupitia katiba Mpya.

Mkandara, naona labda niishie hapa kwasababu kadri ninavyokusoma nashindwa kukuelewa. Huenda ndio maana umefikia kiwango cha kuelewa mada za Makonda ambazo hazipo ab initio.

Mkandara suala la katiba halina wengi wape wakati wa kuandika.
Lazima uelewe kuwa tunatakiwa tueondoke hapa tulipo katika siasa za majitaka ya uchama,twende mbele na ku shape future ya watoto na wajukuu zetu.

Hili suala la wengi wape lipo mitaani, wakati wa kuandaa nyaraka muhimu kama hii, unaposhauri wengi wape inasikitisha.
Mkandara wewe una exposure ya huko ulipo, hakika tumia hiyo kulisaidia taifa. Kwa mwendo huu ninaouona, unakatisha tamaa.
Samahani inabidi nikueleze ukweli tu.

Tunaposhindwa kuona tofauti kati yako na Makonda lazima fahamu kuna tatizo kubwa sana.
Hapa nakueleza mubashara, mkuu hoja ya wengi wape ni too low.

Ni kauli inayotumiwa sana na hoodlums, nincompoop and the likes wanapokuwa hawana mawazo wala hawana hoja.

Hivi kiwango cha wabunge wetu unakijua?
Pili, wengi wape si ndio imetengeneza katiba ya 1977 kwanini leo tunaandika tena?

Kwamba wengi wakiamua kuwa Rais anaweza kuuza mkoa ikibidi basi ndiyo wengi wape yenyewe.
Katiba inapigiwa kura na wengi, haiandaliwi na wengi. Inaanza kwa ellite halafu inaishia mitaani.

I am sorry I have to tell you. Mkandara, never say it again.
Mkuu you're way better than this. Please, never say it again.

Naomba niishie hapa nisijeingia eneo nisilotarajia hata kama nina mengi. Inasikitisha sana
Mkuu wangu sitopenda kubishana ili mradi tunabishana kama kule mwanzo. sasa nakuuliza wewe maswali machache tu kuhusu hili la Wengi wape ulolikataa wewe msomi mwenye kila sifa na matuzo ya ufahamu.

Ulitegemea hawa wajumbe wangefikia makubaliano vipi ikiwa wote hawa walienda pale kwa maslahi ya vyama na taasisi zao? Wee nambie maana hawa ni watu zaidi ya 300 wenye mawazo tofauti wewe ulifikiri wangefikia vipi suluhisho ya kila ibara ya katiba mpya!..

Na tafadhali usiwe sorry na mimi kwa sababu wewe sii mwelewa ni shabiki na mwenye chuki binafsi. Hutaki kujifunza isipokuw akwa yale ulobatizwa nayo kama muumini wa dini. Nilichokiandika mimi ni kutokana na ukweli uliokuwepo na sijam quote mtu kama yeye ndiye mwanzishi kama unavyofanya wewe kwa kusema ati CCM waliandika rasimu yao na Sitta ndiye aloishinikiza kama vile ulikuwepo ktk vikao vya CCM. Ni mwongo na mtunzi mzuri sana wa hekaya sanifu na ndicvho pekee kinachonivutia kwako japo najua fika Unaongopa!..

Anyway huna haja ya klinisoma lakini UKAWA hawaniwakilishi mimi na haya maneno waliyasema wao wenyewe, na pili walitakaa takataka kuwa Muungano wetu ni haramu na hivyo sijui walitaka kuandika katiba ya nchi gani kama sio Tanganyika na hivyo kudai kwa serikali 3 ilikuwa njama moja na CUF ili Zanzibar iwe huru na Tanganyika iwe kivyake. Upuuzi huu mnao nyie vijana mlozaliwa baada ya Uhuru mlolishwa kwa Umma na vijiko sio sisi tunaofahamu mkazi kubwa ilofanywa na waasisi wa Uhuru na Muungano wetu. Na kwa mwendo huo, mrudi Bungeni msirudi CCM inachukua Uongozi tena mwaka 2015 na nyie wenyewe ndio wa kujilaumu. Nawasikitikia sana wale waloingizwa Mkenge na UKAWA wasijue hivi vyama vimekusudia nini...
 
Mkandara;10025830]Na tafadhali usiwe sorry na mimi kwa sababu wewe sii mwelewa ni shabiki na mwenye chuki binafsi.
Chuki zipi na kwa nani?

Hutaki kujifunza isipokuw akwa yale ulobatizwa nayo kama muumini wa dini.
Kujifunza si pamoja na kujadiliana mkuu. Au kujifunza maana yake ni kukubaliana nawe?

Nilichokiandika mimi ni kutokana na ukweli uliokuwepo na sijam quote mtu kama yeye ndiye mwanzishi kama unavyofanya wewe kwa kusema ati CCM waliandika rasimu yao na Sitta ndiye aloishinikiza kama vile ulikuwepo ktk vikao vya CCM. Ni mwongo na mtunzi mzuri sana wa hekaya sanifu na ndicvho pekee kinachonivutia kwako japo najua fika Unaongopa!..
Kwani waliosema ipo rasimu ya CCM ni nani? Ulitegemea rasimu hiyo iwekwe kwenye vibanda vya magazeti? Nyerere alipoitisha faili la EL ulikuwepo? Vikao vya kamati za CCM unaingia?

Upuuzi huu mnao nyie vijana mlozaliwa baada ya Uhuru mlolishwa kwa Umma na vijiko sio sisi tunaofahamu mkazi kubwa ilofanywa na waasisi wa Uhuru na Muungano wetu. Na kwa mwendo huo, mrudi Bungeni msirudi CCM inachukua Uongozi tena mwaka 2015 na nyie wenyewe ndio wa kujilaumu. Nawasikitikia sana wale waloingizwa Mkenge na UKAWA wasijue hivi vyama vimekusudia nini..
vijana?
CCM kuchukua tena hilo si tatizo, hakuna marefu yasiyo na ncha. Tupo hapa kusimamia masilahi ya Watanganyika.
Kama wewe unakubali wazanzibar wajadili namna tunavyoweza kujenga wodi za wazazi kwasababu tu wana haki ya kuvunja muungano, sisi wengine tunasema hapana. Tuliona wazee wakipigania Uhuru wa Tanganyika. Uhuru huo haukulenga kukibeba kisiwa kidogo na kukipa haki ya kupora, kunyonya na kuamua hatima yetu.

Hao wazee uliowaona wakifanya kazi kubwa leo wasingekubali azimio la Arusha life. Wazee hao wangetushangaa kwanini tunaiuza Tanganyika kwa bei nafuu kiasi hiki. Hata wao wangeshangaa imekuwaje hatuwezi kujadili namna ya kujenga vyoo vya shule eti mpaka wazanzibar 50 wakubali.

Wazee hao wangetaharuki kuona rasilimali walizopigani kwa watoto wao zikitumika nchi jirani ya zanzibar.
Wangetusangaa hivi kweli tulimuondoa mkoloni ili kodi isiende Uingereza na sasa tunapeleka kodi nchi jirani ya znz?
Na mwisho, wazee hao wangeshangaa tuna taifa la aina gani ambalo katiba yake inaweza kuvurugwa na watu 50 wa BLW huku watu milioni 43 wakiwa kimya? Wangejiuliza

Na mwisho utunzi wangu wa riwaya hakika ni mzuri. Niliwaeleza Wazanzibar mwaka 2010 akina Mdondoaji, Takashi na wenzao kuwa kkuitafuta Tanganyika ni matatizo kwao. Utunzi wangu unatimia, si unaona wanavyovurugana?
Utunzi wangu mzuri, niliwaeleza wapinzani CCM haina nia nzuri ya mchakato, yametimia
Utunzi wangu mzuri, nilisema bunge litavunjika, na limevunjika.
Utunzi wangu mzuri, nilisema udhaifu wa kikwete hawezi kusimamia katiba. Imetimia
Niliwaambia Chadema ndani ya miezi 8 watakuwa na mgogogoro mkubwa, yakatokea katika mwezi wa 5
Niliwaambia Chadema, huyu Zitto na kila wana lao jambo, leo tunalijua
Utunzi ni mwingi na nashukuru kila utunzi unakuwa kweli.

Na leo naweka utunzi mwingine, jambo zuri kila ninalotunga linakuwa. Sijui ni coincident au ni utunzi wa ndoto.
 
Makonda,

Unazungumzia katiba ya wananchi wa wapi ikiwa tume mliyounda ninyi wenyewe kwenda kukusanya maoni kwa wananchi leo mmeigeuka hamtaki kuisikiliza?
 
Makonda,

Unazungumzia katiba ya wananchi wa wapi ikiwa tume mliyounda ninyi wenyewe kwenda kukusanya maoni kwa wananchi leo mmeigeuka hamtaki kuisikiliza?
Yaaani ni kujichanganya sana. Ndiyo yale ya watu wanaosema katiba iandikwe kwa msingi wa WENGI WAPE. Hii iliyopo iliandikwa na 100% wengi, leo tunaandika nyingine haionekani kama watu wanajifunza au wana uelewa huo.
Inatisha, inasikitisha na inahuzunisha. Tuandike katiba kwa sababu ya wingi na si mantiki! laah.

Tume wameunda CCM, wanaokana tume CCM kwasababu wengi wape. Kuna hoja na vioja
 
Chuki zipi na kwa nani?
Ndio maana nasema huwa husoma ukaelewa. Wewe hula chakula pasipo kutafuna na hili ndio tatizo lako. Mabandiko yako yote yanahusu chuki zako kwa Wazanzibar na CCM kiasi kwamba unashindwa kuelewa hata makosa mnayofanya na upande wako na ndicho nachozungumzia pasipo upendeleo. Utawachukia vipi Wazanzibar hawa wakati upo nao UKAWA? Kisha unadai Utanganyika wakati hawa hawa ndio wanaotukana hadi Muasisi wa Uhuru wako! Utanganyika upi unaotetea wewe kama sii kipofu alomshika tembo mkia. Mimi nasimama kama mimi au mwananchi, kwa kila hoja huchanganya na za kwangu sifuati mkumbo wa chama wala mtu mwingine. Mtu wangu akifanya makosa ama ujinga namkosoa sitopongeza Ujinga.

Kujifunza si pamoja na kujadiliana mkuu. Au kujifunza maana yake ni kukubaliana nawe?
Sio lazima ukubaliane na mimi isipokuwa uelewa wa yale tunayoandika usitafsiri unavyopenda wewe ktk kujitetea tena nje ya hoja.
Kwani waliosema ipo rasimu ya CCM ni nani? Ulitegemea rasimu hiyo iwekwe kwenye vibanda vya magazeti? Nyerere alipoitisha faili la EL ulikuwepo? Vikao vya kamati za CCM unaingia?
Mkuu ndio yale yale ya kutoelewa. Mimi nimesema haya kwa kuonyesha wewe mtunzi mzuri wa hekaya kwa sababu umeingia hadi ndani ya rasimu ya CCM imeandaliwa vipi kana kwamba ulikuwepo wakati hakuna mahala popote CCM wameeleza hayo. nachofanya mimi ni kunukuu yalokwisha tokea. Ya Lowassa na Nyerere yanazungumziwa kutokana na habari iliyotolewa lakini hakuna mtu alosema nani aliandaa faili la EL na lilikuwa wapi... wewe ndio unayejua haya kwamba Lowassa alikuwa na faili lake Nyerere akaliitisha kutoka wapi unajua wewe. Ndio maana nasema wewe mtunzi mzuri wa riwaya.
CCM kuchukua tena hilo si tatizo, hakuna marefu yasiyo na ncha. Tupo hapa kusimamia masilahi ya Watanganyika.
Kama wewe unakubali wazanzibar wajadili namna tunavyoweza kujenga wodi za wazazi kwasababu tu wana haki ya kuvunja muungano, sisi wengine tunasema hapana. Tuliona wazee wakipigania Uhuru wa Tanganyika. Uhuru huo haukulenga kukibeba kisiwa kidogo na kukipa haki ya kupora, kunyonya na kuamua hatima yetu.
Haya ndo maneno ya vijana mnaotaka kuongoza nchi sasa hivi. Vijana mlokuta Uhuru kamili na hamjui kwa nini kumekuwepo na mageuzi ktk siasa tukawa na demokrasia. Nina hakika kabisa kama wewe ungekuwa CCM ungeuliza kwa nini sera za CCM lazima zipitishwe na Wabunge wachache wa Chadema, au NCCR. Kwa nini bunge letu lina vyama kama Chadema wanatupotezea muda na gharama kwa wananchi wakati tunawalisha kwa mishahara na posho. Nadhani pengine hata hii demokrasia huitaki na ndio maana asilimia 80 ya Watanzania ktk kura zao za maoni walisema hawataki mfumo wa vyama vingi kwa mind set kama hii.

Ni fikra hizi za vijana wa leo ambazo wanashindwa kuelewa ya kwamba wabunge waliopo Dodoma wapo pale kuwakilisha mchango wa itikadi na sera zao tofauti na mtawala ili kukosoana kabla ya kufanya makosa ktk utekelezaji wa sera na utunzi wa sheria. Bunge kazi yake ni kutunga sheria, maswala ya Bajeti na kupitisha ni swala la Kichama hivyo Watanganyika na Wazanzibar wapo pale kupitisha bajeti kichama na sera zao na sio Kizanzibar. Pale ni CCM vs Vyama vya Upinzani. Mzanzibar CCM hana tofauti na Mbara CCM inapofikia maswala haya.

Kama kweli upo hapa kujifunza basi elewa hapakuwa na Uhuru wa Tanganyika pasipo nchi zote za East Afrika na Afrika kuwa huru. Tuliubeba mzigo huo toka mwanzo sasa iwe kosa ama sio ni swala la kujadili leo sio kukana ukweli huo.

Hao wazee uliowaona wakifanya kazi kubwa leo wasingekubali azimio la Arusha life. Wazee hao wangetushangaa kwanini tunaiuza Tanganyika kwa bei nafuu kiasi hiki. Hata wao wangeshangaa imekuwaje hatuwezi kujadili namna ya kujenga vyoo vya shule eti mpaka wazanzibar 50 wakubali.
Huu ni upuuzi mwingine samahani sana kwa hilo..Hivi kweli wewe mkuu wangu unashindwa kutazama impact ya sera mbovu na kuilalamikia CCM na utawala wake wa miaka 50 imeshindwa mnasingizia Muungano na Wazanzibar. Hivi kweli wewe unajua Uhuru wetu ulilenga kuunganisha nchi ngapi? Hao wazee wangetushangaa kuona Afria tumetengana au au sisi kubeba mzigo wa Zanzibar wakati wao waliibeba mingi zaidi sisi tumeitua njiani. I mean huu ni ujinga mkuu wangu, kama kuna failure zozote za maendeleo nchini basi ni CCM walotukwamisha! ni CCM wa kulaumiwa na kutowapa nafasi tena ya kuongoza nchi. Iwe tuna serikali za nchi 2, au 3, tuwe na mikoa 17 au 30 ni CCM wa kulaumiwa na sio hadithi za serikali 3. Kinachopimwa ktk mafanikio ya nchi ni chama tawala na sera zake sio wingi wa serikali, ukubwa wa nchi ama idadi ya watu. Wakati mwingine mkuu unachosha sana.
Wazee hao wangetaharuki kuona rasilimali walizopigani kwa watoto wao zikitumika nchi jirani ya zanzibar.
Wangetusangaa hivi kweli tulimuondoa mkoloni ili kodi isiende Uingereza na sasa tunapeleka kodi nchi jirani ya znz?
Na mwisho, wazee hao wangeshangaa tuna taifa la aina gani ambalo katiba yake inaweza kuvurugwa na watu 50 wa BLW huku watu milioni 43 wakiwa kimya? Wangejiuliza
Na huu ndio ujinga mwingine, rasilimali ni pomoja na watu, Hivyo unaposema rasilimali huoni kama watu wachache kutumikia watu wengi ndio inaweza kuwa tatizo? Zanzibar wanalipa kodi zao na zinakuja bara TRA kwenye watu wengi ambao majority ya nguvu kazi hawana ajira. Tatizo la nchi hii ni kutegemea maliasili na CCM miaka yote imeshindwa kuleta maendeleo kwa fikra hizi badala ya kuwekeza mtaji kwa WATU ( human Capital) ili kuzalisha ajira na uwekezaji wa ndani.

Pasipo Elimu huwezi kujenga nguvu kazi ya kizazi kipya! kizazi kipya sio kutegemea gas na Tanzanite bali vijana wengi zaidi kuhitimu elimu ya juu na uwekezaji ktk elimu na nguvu zao ndani. Kati ya watu 10,000 wa bara ni mmoja tu mwenye elimu ya juu, na kati ya watu 100 hamsini hawana kazi. Walipa kodi halali nchini hawafiki millioni 5 wakati wenye uwezo wa kufanya kazi ni zaidi ya millioni 20, tazama mtaji wa nguvukazi hii inavyopotea na kuoza bure. Mungu atupe nini zaidi isipokuwa sisi kazi yetu kulaumu Zanzibar na Wakoloni.

Na mwisho utunzi wangu wa riwaya hakika ni mzuri. Niliwaeleza Wazanzibar mwaka 2010 akina Mdondoaji, Takashi na wenzao kuwa kkuitafuta Tanganyika ni matatizo kwao. Utunzi wangu unatimia, si unaona wanavyovurugana?
Utunzi wangu mzuri, niliwaeleza wapinzani CCM haina nia nzuri ya mchakato, yametimia
Utunzi wangu mzuri, nilisema bunge litavunjika, na limevunjika.
Utunzi wangu mzuri, nilisema udhaifu wa kikwete hawezi kusimamia katiba. Imetimia
Niliwaambia Chadema ndani ya miezi 8 watakuwa na mgogogoro mkubwa, yakatokea katika mwezi wa 5
Niliwaambia Chadema, huyu Zitto na kila wana lao jambo, leo tunalijua
Utunzi ni mwingi na nashukuru kila utunzi unakuwa kweli.

Na leo naweka utunzi mwingine, jambo zuri kila ninalotunga linakuwa. Sijui ni coincident au ni utunzi wa ndoto.
Mkuu pengine hunifuatii kwa makini. Kila napokusoma umeshindwa kutenganisha Kero na mapungufu yetu. Kama swala ni kero za Wazanzibar hata mimi nimezizungumzia sana huko nyuma na Wazanzibar wanajua. Mbali na hivyo nawajua zaidi yako wewe kihistoria na hali halisi yao leo. Na ndio ktk vijiwe na maneno ya mtaani huwaambia kuhusu Utanganyika kama vile tunavyo bishana ya Yanga na Simba. Ni maneno ya kawaida kwa watu wa Pwani lakini kwa watu kama nyie msojua mnachukulia hasira na kuanza kutukanana kwa matusi ya nguoni. Mimi na hao kina Barubaru, Mdondoaji,Takashi tunaweza kaaa meza moja tukazungumza pasipo kutoana macho lakini sio wewe.

Hizi Kero hazinisumbui bali kinachonisumbua ni kuona maisha ya Watanzania yanazidi kuwa mabaya, Taifa linajenga matabaka ya walokuwa nacho na wasokuwa nacho kutokana na mfumo mbaya wa Utawala na kikubwa zaidi CCM kushindwa kuwaletea wananchi maendeleo kuipeleka nchi yetu mbele, na sio hizi Kero za Wazanzibar! Wao mpia wanaona sisi ni kero vile vile kama mume na mkewe nyumbani haya ni mambo ya kawaida kabisa. Na hata siku moja sintokaa kula meza moja na mtu kama Jussa ambaye fikra zake ni za Kinafiki. Wewe usomjua ndio unambeba kwa ujinga ule ule wa Miafrika kuamini yupo pale kukusaidia.
 
Back
Top Bottom