Nje ya lodge ni mazingira hatarishi kukaa!

Nje ya lodge ni mazingira hatarishi kukaa!

Tafta mazingira tulivu Acha kwenda Lodge za uswazi au za mtaani au zilizo karibu sana na bara bara .........
 
Uoga wako tu kila mtu ana maisha yake,jamsingi katombanie mbali na unapofahamika,kama unaishi kimara katombanie tegeta.
 
Kuna vijana wa hovyo sana nchi hii. Utakuta mijitu imeweka kijiwe nje ya lodge/guest house inapiga stori zisizo na kichwa wala miguu.

Hivi nyie mmekosa mahali pa kwenda mpaka mje mkae hapo nje ya guest na kusababisha watu wanashindwa kutoka humo ndani. Si muende uwanjani au sehemu nyingine mkapigie hizo stori zenu?

Nje ya lodge ni mazingira hatari unaweza kuona vitu/watu ambao hukutakiwa kuwaona ikawa shida tena.

Naomba mjiheshimu
Ukifanya uchunguzi wa kina sana na ulio makini, utagundua kwamba hao watu au vijana wanaopenda kukaa kwenye maeneo kama hayo ni mawakala wa Siri. Utakuta wengi polisi jamii, polisi wa siri, hasa wale wanafanya kazi kwenye idara ya intelijensia ya jinai (CID) au mawakala wa hujuma wa "wazee wa kuvaa Kaunda suti".
Wamiliki wa nyumba za kulala wageni, lodge au mahoteli wanapaswa kusapiga vita sana watu hao wasiwe wanakaa jirani na maeneo yao ya biashara kwani watu hao ni sumu mbaya sana kwa ustawi wa biashara zao.Hao ni watu hatari sana kwa usalama wa biashara zao, usalama wa wafanyabiashara wenyewe na wa wateja wao kwa namna nyingi. Ninayo mifano hai mingi na mibaya sana ya kuwahusu watu hao. Wengi wamekuwa wakitumika katika "kuchora ramani" za watu wateja (targets) ili waweze kuwafanyia njama na hujuma mbalimbali za uhalifu wa kupangwa(targeted crimes). Hata wale ambao kutwa utawaona kwenye maeneo ya starehe wanacheza Pool Table, wengi wao ni miongoni mwa watu wabaya sana kupita kiasi, muwakwepe kama kifo. Mfano, Hao wafanyabiashara wengi ambao mnasikia wameporwa fedha zao, mali zao au kuoprwa madini na "wahusika kutoka vyombo vya usalama" ujue wazi kwamba watonyaji wa mchongo au wasanifu wakuu wa mipango hiyo ni hao watu. Watu hususani wale ambao ni "critics" au "activits" ambao wamekuwa wakidhuriwa kwa kuwekewa sumu, kutekwa, au kuhujumiwa kwa namna nyingine yoyote ile ujue wahusika waliotekeleza mpanho huo ni wao. Kwa kifupi yapo mambo mengi sana mabaya (kwa kiasi kikubwa) ya kuwahusu watu hao, kwa hiyo, "abiria chunga mzigo wako". In short,, I can call them as " THE SNAKES IN SUITS"
So, you must be extremely careful about them.
 
Mnapelekena lodge kufanya nini? Hauna kwako? Au unaishi kwenu? Au ndio mchepuko?
Acha uzinzi!

Mazingira kubadili ni muhim na c kila mwanamke ni wakupelekwa home
 
Kama unachokifanya ni sahihi kwanini uwaogope hao jamaa
 
Ila kweli guest na lodge sio vijiwe.kuna wanawake wengine wana aibu kishenzi unakuta umemlazimisha kakubali.unafika lodge unakuta watu kibao mpka kibenchi wameeka afu ukiwa unaingia woote wanaacha story kukuangalia jinsi unavovutana na mdada kumuingiza ndani [emoji23][emoji23]
 
Kuna vijana wa hovyo sana nchi hii. Utakuta mijitu imeweka kijiwe nje ya lodge/guest house inapiga stori zisizo na kichwa wala miguu.

Hivi nyie mmekosa mahali pa kwenda mpaka mje mkae hapo nje ya guest na kusababisha watu wanashindwa kutoka humo ndani. Si muende uwanjani au sehemu nyingine mkapigie hizo stori zenu?

Nje ya lodge ni mazingira hatari unaweza kuona vitu/watu ambao hukutakiwa kuwaona ikawa shida tena.

Naomba mjiheshimu
Kuwaona wanaotoka na wanaoingia kuna hatari gani? AU kujua mtu fulani anachepuka?
 
Back
Top Bottom