Njia ya PPP yaweza kusaidia pia kwendeleza miradi nchini

Njia ya PPP yaweza kusaidia pia kwendeleza miradi nchini

Kikiwo

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2017
Posts
2,004
Reaction score
1,095
Wana JF nimejaribu kuwaza hivi kwanini nchi yetu haitumii sana njia ya PPP- Public Private Partnership katika kuanzisha miradi ya maendeleo nchini?

Njia hii naona inakuwa na unafuu sana maana sio mkopo bali ni ubia kati ya serikali na mwekezaji wa mradi.
Mwekezaji analeta pesa yote ya mradi na anajenga kwa kutumia wakandarasi wake.

Akimaliza mradi ukaanza kufanya kazi hapo wanaanza kugawana mapato labda kwa asilimia 60% mwekezaji na Serikali asilimia 40% kufuatana na makubaliano yao mpaka pesa za mwekezaji zinarudi zote hata iwe miaka 20, 30 n.k

Uzuri wa njia hii mradi unalipa kodi za serikali kama kawaida. TRA inakusanya kodi since day one- yani siku ya kwanza .
Nafikiri njia hii nayo tuikazanie itatusaidia
 
Wana JF nimejaribu kuwaza hivi kwanini nchi yetu haitumii sana njia ya PPP- Public Private Partnership katika kuanzisha miradi ya maendeleo nchini?
Njia hii naona inakuwa na unafuu sana maana sio mkopo bali ni ubia kati ya serikali na mwekezaji wa mradi.
Mwekezaji analeta pesa yote ya mradi na anajenga kwa kutumia wakandarasi wake. Akimaliza mradi ukaanza kufanya kazi hapo wanaanza kugawana mapato labda kwa asilimia 60% mwekezaji na Serikali asilimia 40% kufuatana na makubaliano yao mpaka pesa za mwekezaji zinarudi zote hata iwe miaka 20, 30 n.k
Uzuri wa njia hii mradi unalipa kodi za serikali kama kawaida. TRA inakusanya kodi since day one- yani siku ya kwanza .
Nafikiri njia hii nayo tuikazanie itatusaidia
Ndugu, haya mambo ya PPP yameongelewa sana na wadau wa maendeleo toka serikali ya Jakaya na kulikuwa na tetesi wakati huo kwamba Barabara ya kutoka Dar hadi Chalinze ingejengwa/kupanuliwa na kuwa njia nne lakini mradi ukaota mbawa. Mimi binafsi nimekuwa na mawazo haya ya serikali kushirkiana na sekta binafsi katika kutekeleza miradi ya maendeleo kuanzia miradi ya kati hadi mikubwa.

1. Kama serikali ingeshirikana na sector binafsi kwenye upimaji wa viwanja leo hii miji yetu isingekuwa na mipangilio ya hovyo ya makazi. Au serikali ingeweka utaratibu mzuri na wa kuaminika kwa wananchi kulipia viwanja vya makazi, biashara, ma taasisi kabla hta ya upimaji wa viwanja vyenyewe lengo likiwa ni kupata fedha kwa ajili Ya kupima viwanja sidhani kama tungekuwa na miji ilipangika hovyo hovyo INANIKERA SANA.
2. Kama serikali ingeshirikiana na sector binafsi kwenye suala la upatikanaji wa maji mijini na vijijini naamini miji na vijiji vingi vingeweza kupata maji ya kutosha hadi sasa.
3. Kilimo
4. Barabara/Madaraja makubwa n.k

HAYO NI BAADHI YA MAMBO MACHACHE SANA NILIYOYAONA LAKINI HATA KWENYE MIRADI MIKUBWA SERIKALI INAWEZA KUTUMIA PPP KUTEKELEZA HIYO MIRADI. CHA MSINGI NI MIKATABA TU IWE INA WIN-WIN SITUATION. KAMA TUTA-IMPROVE KWENYE MIKATABA BASI NAAMINI PPP NI NZURI NA INAHARAKISHA MAENDELEO KULIKO MAWAZO YA UJAMAA YA KUTEGEMEA SERIKALI KUKOPA NA KUFANYA KILA KITU PEKE YAKE.
 
Back
Top Bottom