Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Matatizo ni sehemu ya maisha ya mwanadamu,,kwa maana kwamba kama kusingekuwa na matatizo basi huyu mwanadamu asingekuwa na umuhimu wowote hapa duniani
Kwahiyo shida na matatizo ndio yanatufanya tutafakari kwa kina,tuwaze na kuwazua na mwisho wa siku tunapata ufumbuzi
Kuna njia nne kuu za kufuata ili utatue changamoto zozote ambazo utakutana nazo
Mosi, hakikisha unajua shida au tatizo liliopo mbele yako,wataalamu wa mambo wanasema ,ukijua tatizo basi tayari utakuwa umefikia nusu ya suluhisho lake
Mfano,, kama mwanaume anasumbuliwa na nguvu za kiume,basi anatakiwa ajue kwanza je,tatizo ni la kisaikolojia au ni kimaumbile? Akitambua hasa shida ni nini atakuwa amefikia nusu ya sulihisho
Pili, tafuta majibu yote ambayo yanaweza kuwa suluhisho la tatizo husika,andika kila wazo liwe kubwa au dogo ambalo unahisi linaweza kuwa suluhisho
Tatu, waza na kuwazua au tafakari kwa kina kwa kuangalia,kila jibu upande wa hasara na faida,kisha tafuta jibu ambalo faida zake ni kubwa kuliko hasara
Nne, lifanyie kazi hilo suluhisho,ukishaamua kulifanyia kazi hilo suluhisho basi fanya na usianze tena kuwa na mashaka nalo,hata kama halitakuwa kwa asilimia mia moja lakini utakuwa umefikia hatua kubwa ya kupata ufumbuzi
Ni hayo tu!
Kwahiyo shida na matatizo ndio yanatufanya tutafakari kwa kina,tuwaze na kuwazua na mwisho wa siku tunapata ufumbuzi
Kuna njia nne kuu za kufuata ili utatue changamoto zozote ambazo utakutana nazo
Mosi, hakikisha unajua shida au tatizo liliopo mbele yako,wataalamu wa mambo wanasema ,ukijua tatizo basi tayari utakuwa umefikia nusu ya suluhisho lake
Mfano,, kama mwanaume anasumbuliwa na nguvu za kiume,basi anatakiwa ajue kwanza je,tatizo ni la kisaikolojia au ni kimaumbile? Akitambua hasa shida ni nini atakuwa amefikia nusu ya sulihisho
Pili, tafuta majibu yote ambayo yanaweza kuwa suluhisho la tatizo husika,andika kila wazo liwe kubwa au dogo ambalo unahisi linaweza kuwa suluhisho
Tatu, waza na kuwazua au tafakari kwa kina kwa kuangalia,kila jibu upande wa hasara na faida,kisha tafuta jibu ambalo faida zake ni kubwa kuliko hasara
Nne, lifanyie kazi hilo suluhisho,ukishaamua kulifanyia kazi hilo suluhisho basi fanya na usianze tena kuwa na mashaka nalo,hata kama halitakuwa kwa asilimia mia moja lakini utakuwa umefikia hatua kubwa ya kupata ufumbuzi
Ni hayo tu!