Njombe: Binti afariki baada ya kupigwa na Shangazi yake kwa kuchelewa kurudi nyumbani

Njombe: Binti afariki baada ya kupigwa na Shangazi yake kwa kuchelewa kurudi nyumbani

Adhabu iendane na na kosa la mtoto, Na ilenge kumsaidia siyo kumwadhibu
Zungumza nae nini Sababu za kuchelewa , Muundie Program itakayomfanya awe anawahi nyumbani, Zungumza nae kama ashaanza kuchovywa chovywa, kiurafiki na umpe msaada katika hilo

Televisheni Na Redio Undeni programu za kufundisha malezi kwa watoto ili kusaidia Jamii
 
Kanuni ya Maisha kati ya mtoto na mzazi au mlezi ipo wazi. Mzazi amepewa wajibu wa kumtunza na kumlea pia kumpa mahitaji yake yote kadri ya uwezo wa mzazi/mlezi.

Hata kwenye Sheria zetu za Tanzania kwenye Sheria ya mtoto inampa mzazi wajibu huohuo. Hata kwenye biblia wajibu huo amepewa mzazi/mlezi. Kwa maantiki hiyo mtoto ana Haki ya kupata hayo kutoka kwa mzazi/mlezi bila upendeleo wala masharti kwa sababu ni maagizo.

Lakini Duniani kote hakuna Haki bila wajibu. Katika hayo yote,kanuni hiyohiyo imempa mtoto wajibu wa KUWAHESHIMU WAZAZI/WALEZI na KUWATII. Kwenye hili Mungu aliweka mkazo zaidi akaweka ktk Amri zake kumi.

Ile Amri ya nne inaagiza watoto KUWAHESHIMU WAZAZI/WALEZI. Na Mungu kwenye Amri ile akawapa na ahadi kuwa wakiwaheshimu wazazi wataishi miaka mingi na Heri Duniani. Hii ndiyo Amri pekee yenye ahadi. Tukirudi kwa marehemu,alistahili hiyo adhabu kutokana na kuvunja kanuni ya Maisha,kuvunja Sheria za Tanzania na Amri ya nne ya Mungu. Huyu hata mbinguni hawezi kwenda labda utokee muujiza!
Hakuna adhabu aliyoruhusiwa mzazi au mlezi kwa mtoto wake ambayo hupelekea kifo adhabu iliruhusiwa ni kutumia bakora tu maana hata mkono umekatazwa bakora haiwezi kuua na umepewa tahadhari kabisa usimpige mtoto ukiwa na hasira,
Mtoto alikosea kutotii walezi wake lakini kwa alichofanya mlezi kakosea pia sioni cha kumtetea hapo
 
Hiyo ndo raha yawamama wamikoani wanatoa adhabu pia ,ingekua ,mzaramo,mkwele hivi wazazi wangekua wanafurahi ,yaan mama anauliza amekupa nn mwanangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usimnyime mtoto mapigo
Adhabu iendane na na kosa la mtoto, Na ilenge kumsaidia siyo kumwadhibu
Zungumza nae nini Sababu za kuchelewa , Muundie Program itakayomfanya awe anawahi nyumbani, Zungumza nae kama ashaanza kuchovywa chovywa, kiurafiki na umpe msaada katika hilo

Televisheni Na Redio Undeni programu za kufundisha malezi kwa watoto ili kusaidia Jamii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila binti wa miaka 18 kumwadhibu, ni kofi mbili tu za shavu tena hapo mzazi umekasirika mpaka mishipa imekutoka, huwezi mcharaza jitu zima kama kitoto.
 
Watu tunatembea tumejifia kwa muda huu ni kuwa makini tuu katika utoaji wa adhabu, yote kwa yote kuonya kukemea bado ni jukumu la mzazi huwezi kuona mtoto anakengeuka ukamwacha itakua sio ulezi bora cha msingi adhabu iwe kwa kiasi! R I P Binti pia pole kwa Shangazi yake kwani anaacha pengo kwa familia yake
 
Umeanza vizuri but umemalizia kama nyumbu

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo la sisi waafrika ni uelewa tu..!! Hivi unajua maana ya Amri!?? Amri popote pale haivunjwi mkuu! Yaani hata Amri tu ya mahakama ukiivunja lazima utaadhibiwa.

Tunayozungumzia hapa ni Amri ya Mungu. Huyu amevunja wajibu wake wa kutii wazazi/walezi. Lakini pia amevunja Amri ya Mungu. Amri ya Mungu inasema,waheshimu Baba na mama upate miaka mingi na Heri Duniani.

Hii ndiyo Amri pekee Katika Amri kumi za Mungu,huyu amekufa akiwa na miaka 18 tu. Hii ni kuthibitisha kwamba alishaanza muda mrefu kuvunja hii kanuni muhimu kwenye Maisha!!

Kuna watu ukiwaambia ukweli wanapanic eti unahukumu..!! Mungu hatetewi. Kuna wengine wanadai huyo binti alikuwa na mazuri yake pia..huu ni upuuzi wa hali ya juu.

Mussa ambaye ndo Binadamu pekee aliyeongea na Mungu,alifanya mema mengi mno alipopewa jukumu la kuwakomboa wana Israel kutoka utumwani misri. Lakini alifanya kosa moja tu tena siyo la kuvunja Amri mmojawapo katika zile Amri kumi.

Mungu hakutaka hata kusikiliza ule msamaha wake..na nchi ya Ahadi hata kuiona hakuiona. Wakapewa uongozi watu wengine. Nataka nikuambie,Amri haivunjwi na ukiivunja lazima utaadhibiwa!!
 
Alochofanya huyo shangazi ni mauaji wala hakiusiani kabisa na imani sijui wajibu au nini.Nauko kwa Mungu yeye ndiye atakayechomwa moto.Uyo binti alishafikisha umri wa mtu mzima alichotakiwa kufanya nikukaa naye chini nakuongea naye kwautulivu sio kumpiga.sasa inaonekana shangazi ana matatizo yake yamaisha hasira akaamishia kwa mwingine.Fimbo zakuonya siku zote haziwezi kukatisha uhai wa mtu.
Unajua maana ya neno Amri!?? Huyo alikuwa na miaka 18 kama number lakini alikuwa bado yupo chini ya walezi wake. Alipaswa kuendelea kutii full stop.

Hakuna sababu yoyote ile kwa nn mtoto asimtii mzazi/mlezi wake. Hili ni jambo lazima na limeagizwa na Sheria pamoja na Mungu. Lakini hata ukiacha yote hayo ya Sheria nk. Hivi mtu anakupa chakula,anakupa Huduma zote kwenye Maisha yako,wewe unashindwa kitu kimoja tu Utii!?? Huyu hata hii adhabu ya kifo ni ndogo alistahili kupata adhabu kubwa zaidi kama ingekuwepo.
 
Hakukusudia kuua...anampenda ndio maana alimuadhibu ili asijekuharibikiwa..baadae lawama ikarudi kwa mlezi!
Sema tu pengine bint afya mgogoro au hasira zilimzidi shangazi akapiga zaidi.. na siku zenyewe zilishajiishia tu..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom